KakaKiiza
JF-Expert Member
- Feb 16, 2010
- 11,578
- 8,600
[h=6]Pedeshe mmoja alienda na mkewe muziki, akapita binti mzuri akamsalimia, mkewe akamuuliza ,Yule nani? Akajibu Huyo nyumba ndogo yangu. Mke akaja juu,Nataka talaka yangu. Pedeshe akajibu, Powa ntakupa, lakini kumbuka safari za kwenda Uchina na Dubai ndio zitakuwa basi tena, na ishu za kwenda saluni mara mbili kwa wiki utazikosa, sijui utakuwa unatumia gari gani maana sitakuachia gari hata moja. Mama kakaa kimya. Akapita binti mwingine, Pedeshe kamwambia mkewe Huyo nyumba ndogo ya rafiki yangu. Mke wa pedeshe akasema,Mhhh huyu wala siyo mzuri kama nyumba ndogo yetu[/h]