Pendekezo: Watanzania wote tunyukwe bakora hadharani kwa kulikosea heshima neno "onyesha"

Melki the Storyteller

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,701
9,779
Utaratibu huu wa kutembeza dozi uanzie bungeni. Haiwezekani mwakilishi wa wananchi uwapotoshe wananchi wa jimbo lako na watanzania wote kwa ujumla kwa kushindwa kuelewa vyema maana halisi ya neno "onyesha". Ipangwe siku, ateuliwe mbunge mmoja kwa ajili ya kusikiliza kwa makini wabunge wanaoshindwa kutumia vyema neno " onyesha" ili bunge linapoelekea kuisha tushuhudie jinsi spika wetu anavyotembeza bakora kwa wabunge walioshindwa kuliheshimisha neno "Onyesha"

Hali kadhalika kwenye vyombo vya habari hasa hasa channels za taifa, haiwezekani serikali ikuamini na kukupa kitengo cha usomaji wa taarifa ya habari, mwisho wa siku ulipotoshe taifa kwa matumizi mabaya ya neno "Onyesha". Serikali ipange siku ya marejereo ya taarifa zenu za habari, ikibainika tu, viboko vya mgongoni vitembezwe mubashala

Inasikitisha sana msomi na kitambi chake, amefunga tai yake vizuri na makarabasha mkononi, halafu kwa bahati mbaya amesomea shahada ya Kiswahili anashindwa kuwasahihisha watu wanaotumia neno " Onyesha" wakimaanisha kuonesha, badala yake anakuwa mstari wa mbele kuharibu lugha

Viboko visiishie hapo, badala yake viwafikie wakalimani kwa kishindwa kuliheshimisha neno hilo. Baada ya hapo serikali iangalie utaratibu mzuri wa kutembeza bakora kwa watanzania wote wanaoshindwa kutofautisha neno Onyesha na neno Onesha. Napendekeza jeshi la kulinda taifa kuchukua jukumu hili

TURUDI DARASANI
Neno "Onyesha" si sawa na neno "Onesha"
Neno "Onesha" limetokana na neno "Ona". Lakini neno " Onyesha" limetokana na neno "Onya". Kwa hiyo kauli za waandishi wa habari za " Mwenyekiti wa mtaa amemuonyesha mkuu wa mkoa mifuko ya seruji iliyotolewa na Mhe. Jokate Mwegero" ife, badala yake tusikie "Mwenyekiti wa mtaa amemuonesha mkuu wa mkoa mifuko ya seruji iliyotolewa na mh..."

Nahisi nimeeleweka, neno "Onyesha" limetokana na kuonya, na neno "Onesha" limetokana na "Kuona". Tuweni makini kwa kweli

Kwa hiyo neno lilitakiwa kutumiwa kwenye nyanja hizo ni neno " Onesha" ."..amemuonesha"

Karibuni hapa Kitambaa Cheupe tuumwagilie moyo
 
Hali kadharika kwenye vyombo vya habari hasa hasa channels za taifa, haiwezekani serikali ikuamini na kukupa kitengo cha usomaji wa taarifa ya habari, mwisho wa siku ulipotoshe taifa kwa matumizi mabaya ya neno "Onyesha". Serikali ipange siku ya marejereo ya taarifa zenu za habari, ikibainika tu, viboko vya mgongoni vitembezwe mubashala

Nahisi nimeeleweka, neno "Onyesha" limetokana na kuonya, na neno "Onesha" limetokana na "Kuona". Tuweni makini kwa kweli


Karibuni hapa Kitambaa Cheupe tuumwagilie moyo
Na wasioweza kutumia r na l mfanyweje?

Nahisi ni wenge la pombe, maana hapo mwisho ukajichanganya.
 
Onyesha ni neno sahihi kabisa na lipo hata kwenye kamusi za Kiswahili kwa muda mrefu tu!
 
Na wasioweza kutumia r na l mfanyweje?

Nahisi ni wenge la pombe, maana hapo mwisho ukajichanganya.
Ndio mkuu, nimelewa sana. Lakini hata siku moja siwezi changanya matumizi ya L na R katika maandishi nikiwa na akili timamu
 
Onyesha ni neno sahihi kabisa na lipo hata kwenye kamusi za Kiswahili kwa muda mrefu tu!
Kamusi gani hiyo mkuu? Onyesha inatokana na neno onya ilhali onesha inatokana na neno ona! Labda utueleze umesoma mwaka gani maana nakumbuka haya marekebisho yalifanyika miaka ya 2000’s
 
Kamusi gani hiyo mkuu? Onyesha inatokana na neno onya ilhali onesha inatokana na neno ona! Labda utueleze umesoma mwaka gani maana nakumbuka haya marekebisho yalifanyika miaka ya 2000’s
0196DB14-9C74-4A3B-86B2-871B3EE9D913.jpeg
 
....Hali kadharika kwenye vyombo vya habari hasa hasa channels za taifa, haiwezekani serikali ikuamini na kukupa kitengo cha usomaji wa taarifa ya habari, mwisho wa siku ulipotoshe taifa kwa matumizi mabaya ya neno "Onyesha". Serikali ipange siku ya marejereo ya taarifa zenu za habari, ikibainika tu, viboko vya mgongoni vitembezwe mubashala...
Siku nyingine andika kadhalika.😂
 
Binafsi nakerwa zaidi na matumizi ya "ga-ge-gi-go-gu" mfano badala ya "Huwa" mtu anasema "Huwaga",badala ya "sioni" "sionagi".
Ninapoongea na mtu alafu akawa anatumia hizo "ga-ge-gi-go-gu" huwa namuona kichwani ni 🚮🚮🚮
 
Back
Top Bottom