Hatimaye uchaguzi umekaribia ndani ya CHADEMA,mi naanza kwa kumpigia kampeni Ben Saanane achukue nafasi ya Zitto!
Naamini akiingia kwenye uongozi bila shaka CHADEMA itaimarika!
===================
UPDATE BY BEN SAANANE
===================
Naamini akiingia kwenye uongozi bila shaka CHADEMA itaimarika!
===================
UPDATE BY BEN SAANANE
===================
Nyakageni na WanaJF,
Asante....
1: Uchaguzi ndani ya Chama bado na katiba ya chama ya mwaka 2006 ndiyo itakayotoa muongozo
2:Viongozi waliopo wanaendelea kufanya kazi na tunawasaidia katika ujenzi wa chama
3:Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu inahitaji uzoefu zaidi nje ya vigezo vya taaluma.Ni nafasi inayoshikiliwa na mtu ninayemheshimu kama kiongozi aliyechaguliwa kidemokrasia na ibara inayosimamia uchaguzi wa Naibu Katibu Mkuu ndiyo inayosimamia uchaguzi wa Katibu Mkuu baada ya Mapendekezo.
Ndani ya Chama wapo Kaka na Dada zangu walionizidi umri na uzoefu.Hizi ni tunu ninazozienzi katika utendaji wangu ndani na nje ya taasisi za kisiasa.Uzoefu wao ni wa muhimu zaidi katika kipindi hiki chenye changamoto
4:Nimetoa mchango wangu katika harakati za chama kabla sijawa kiongozi na au mtendaji wa chama makao makuu,siku zote ninaweka mbele maslahi ya chama kwa kushirikiana na wanachama na viongozi bila kujali vyeo
5:Mleta mada Makaura: Asante kwa kuwa na imani nami na wote walioonyesha imani yao kwangu kwa sababu walizo nazo.Mmenitia nguvu zaidi,sitaisaliti imani yenu kwangu kwa kubweteka bali njia pekee ya kuienzi imani hii ni kuebdelea kukitumikia chama na taifa letu kwa bidii kupitia nafasi niliyonayo.Nimeipitia thread hii kwa kina usiku huu
Kuna walionishauri kama wanachama,watanzania wasiokua na vyama au wenye vyama lakini vyama kinzani,kuna walioshauri kama Kaka na Dada zangu walionizidi umri na uzoefu (bila kujali umri).Mungu awabariki
Pia waliotoa mawazo hasi bila kujali itikadi zetu hata kama ni wa upande ule mwingine(CCM),nimewasikia na hii ndiyo demokrasia.Mmenisaidia kujijenga na kuinarisha ngozi yangu izidi kuwa ngumu
Wale waliotunga stori za uongo kwa nia ya kunichafua,wametekeleza wajibu wao waliotumwa/waliojituma.Sina tatizo kwani Ukiwa Mwanasiasa na ukasifiwa na watu hasa wapinzani wako kila siku basi ni bora uache siasa.Waliotunga stori za uongo na matusi,Hakika nao wameingia katika historia nyeusi katika kukuza demokrasia ya vyama vingi
Naomba niseme wazi,tunajiandaa na uchaguzi ndani ya chama.Muda ukifika kwa rehema zake Mwenyezi Mungu nitachukua hatua za kidemokrasia kwa nafasi ambayo nitaona ninaimudu kulingana na mahitaji ya muda na baada ya kutathmini mchango na matokeo ya mimi kuwa katika nafasi hiyo katika kukivusha chama katika kipindi hiki cha ukombozi wa pili endapo wanachama watanipa ridhaa kwa mujibu wa katiba ya chama chetu.
Nitatangaza nia yangu hadharani kama nilivyofanya tarehe 28/04/2011 nilipotangaza Rasmi mbele ya waandishi wa Habari pale Travertine Hotel nilipotangaza nia yangu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Vijana Taifa.Sina woga,napenda uwazi.
JF kama Mwalimu wangu,mlezi na rafiki katika safari yangu katika jangwa atakua wa kwanza kujua hatua nitakayopiga
Asanteni sana kwa kura ya imani (Hasi na Chanya),tuendelee kujenga chama chetu na tumuombe Mungu atutangulie mbele ya safari yetu.Jambo la Muhimu tuweke matumaini mbele juu ya mustakabali wa chama chetu kupitia mamlaka ya kikatiba,ili kiu na ndoto ya kuona Tanzania yenye Neema na ya kujivunia inafikiwa siku za usoni.Mbarikiwe!!!