Pendekezo: Mbunge au Diwani akiachia ngazi,chama kilekile kiteue mbunge/Diwani mwingine

magode

JF-Expert Member
Oct 2, 2014
2,201
3,322
Wanabodi,
Salaam;

Wimbi la viongozi kuhama chama kwa kisingizio cha kumuunga mkono Rais,linaendelea.

Viongozi hawa waliochaguliwa kwa jasho na damu,wanaamua kuziacha nafasi zao na wanaenda kuomba kugombea nafasi zilezile ktk chama kingine. Mfumo huu unatuingiza kwenye gharama kubwa km Taifa.

Serikali inatumia pesa nyingi kufanya chaguzi ndogo ambazo ni chaguzi za kihuni kabisaa! Tunapoteza pesa serikalini,kwenye vyama na wagombea wenyewe. Wananchi nao wanapotezewa muda kwenda kwenye mikutano ya kampeni na kupiga kura..!

Bunge la Tanzania,kwa nn msipeleke mswada bungeni kuweka kipengele cha kufutwa kwa chaguzi ndogo,badala yake iwe chama kilichoondokewa na kiongozi wake,iwe kwa kufa,kufukuzwa au kujiudhuru,kiteue kiongozi mwingine na kisha tume imthibitishe. Hii itapunguza gharama hizi za kipuuzi. Na nna uhakika sheria hii ikipitishwa,hakuna mbunge wala Diwani atakayeachia ngazi...!!

Nawasilisha.
 
kiufupi tunataka wapinzani wawepo baadhi ya vipindi tu! kikikaribia kipindi cha uchaguz mkuu tunawanunua wote! ukiweka sharti hilo watakuambia hio sio demokrasia! huo ni ulaji uliobuniwa kipindi cha hivi karibuni! teh tehe ee.. manyeti hoyee..
 
Wanabodi,
Salaam;

Wimbi la viongozi kuhama chama kwa kisingizio cha kumuunga mkono Rais,linaendelea.

Viongozi hawa waliochaguliwa kwa jasho na damu,wanaamua kuziacha nafasi zao na wanaenda kuomba kugombea nafasi zilezile ktk chama kingine. Mfumo huu unatuingiza kwenye gharama kubwa km Taifa.

Serikali inatumia pesa nyingi kufanya chaguzi ndogo ambazo ni chaguzi za kihuni kabisaa! Tunapoteza pesa serikalini,kwenye vyama na wagombea wenyewe. Wananchi nao wanapotezewa muda kwenda kwenye mikutano ya kampeni na kupiga kura..!

Bunge la Tanzania,kwa nn msipeleke mswada bungeni kuweka kipengele cha kufutwa kwa chaguzi ndogo,badala yake iwe chama kilichoondokewa na kiongozi wake,iwe kwa kufa,kufukuzwa au kujiudhuru,kiteue kiongozi mwingine na kisha tume imthibitishe. Hii itapunguza gharama hizi za kipuuzi. Na nna uhakika sheria hii ikipitishwa,hakuna mbunge wala Diwani atakayeachia ngazi...!!

Nawasilisha.
Japo nakubaliana na wewe kuhusu kuokoa fedha za marudio ya uchaguzi ya mara kwa mara lkn sikubaliani na ushauri wako wa chama kilichopoteza mbunge kiteue mwingine aendelee na Jimbo kwani hiyo hii itakuwa kuwawekea wananchi muwakilishi wasiyemchagua napendekeza yule anayehama chama ahame na ubunge wake lkn anayefariki uchaguzi ufanyike lkn tuangalie uwezekano wa wagombea binafsi ili wasibanwe na vyama vyao.
 
Wanabodi,
Salaam;

Wimbi la viongozi kuhama chama kwa kisingizio cha kumuunga mkono Rais,linaendelea.

Viongozi hawa waliochaguliwa kwa jasho na damu,wanaamua kuziacha nafasi zao na wanaenda kuomba kugombea nafasi zilezile ktk chama kingine. Mfumo huu unatuingiza kwenye gharama kubwa km Taifa.

Serikali inatumia pesa nyingi kufanya chaguzi ndogo ambazo ni chaguzi za kihuni kabisaa! Tunapoteza pesa serikalini,kwenye vyama na wagombea wenyewe. Wananchi nao wanapotezewa muda kwenda kwenye mikutano ya kampeni na kupiga kura..!

Bunge la Tanzania,kwa nn msipeleke mswada bungeni kuweka kipengele cha kufutwa kwa chaguzi ndogo,badala yake iwe chama kilichoondokewa na kiongozi wake,iwe kwa kufa,kufukuzwa au kujiudhuru,kiteue kiongozi mwingine na kisha tume imthibitishe. Hii itapunguza gharama hizi za kipuuzi. Na nna uhakika sheria hii ikipitishwa,hakuna mbunge wala Diwani atakayeachia ngazi...!!

Nawasilisha.
Ni wazo zuri sana litasaidia kuokoa Pesa za walipa kodi. Lakini sio akijiuzulu tu, Bali hata akifariki, chama kilichoshinda uchaguzi mkuu kiteuwe Raisi, Mbunge au hata Diwani mwengine. Kwa maana hiyo Uchaguzi utakuwa ni mara moja kwa Kila Jimbo kwa kipindi cha miaka mitano
 
Hahaha lipumba alijiuzuru uenyekiti CUF, akarudishwa na msajili kwa nguvu, hata hawa madiwani na wabunge mnaona wanarudishwa na Tume ya uchaguzi kwa nguvu.
Ungeshauri wakijiuzuru wahame nchi au wauwawe, wakibaki nchini na wakawa hai watarudishwa kwa nguvu kwa namna yoyote ile isiyo halali.
Inaonekana kujiuzuru haiwezekana kwa namna yoyote ile au maana ya kujiuzuru imebadirishwa Tanzania.
 
No ahame na Cheo chake maana wananchi wamemchagua yeye sio Chama. Chama ni mdhamini tu!
Kama munataka ahame na Cheo chake, kwanza muruhusu mgombea huru bila kudhaminiwa na chama ndio italeta maana wazo lako. Wazo ni kuokoa Pesa za walipakodi kutumika kiholela. kwa maana ikitokea kua Mbunga, Raisi au Diwani kajiuzulu au kafariki, Chama kilichoshinda Uchaguzi mkuu kitateuwa mwengine kuziba Nafasi
 
Japo nakubaliana na wewe kuhusu kuokoa fedha za marudio ya uchaguzi ya mara kwa mara lkn sikubaliani na ushauri wako wa chama kilichopoteza mbunge kiteue mwingine aendelee na Jimbo kwani hiyo hii itakuwa kuwawekea wananchi muwakilishi wasiyemchagua napendekeza yule anayehama chama ahame na ubunge wake lkn anayefariki uchaguzi ufanyike lkn tuangalie uwezekano wa wagombea binafsi ili wasibanwe na vyama vyao.
Mkuu sidhani km athari zake zinalingana na athari za sheria hii tuliyonayo ya kurejea uchaguzi na ccm inapanga ushindi. Chama kilichoondokewa na kiongozi,kitapitia michakato yake na kanuni zake kumpata mtu wa kurithi nafasi hiyo. Mfano mzuri ni hapo SA. Zuma atakapoondoka,baada ya masaa 48 ANC watafanya mchakato wa kumpata mtu atakayeshika madaraka kumalizia kipindi cha Zuma kilichobaki.
 
Kama munataka ahame na Cheo chake, kwanza muruhusu mgombea huru bila kudhaminiwa na chama ndio italeta maana wazo lako. Wazo ni kuokoa Pesa za walipakodi kutumika kiholela. kwa maana ikitokea kua Mbunga, Raisi au Diwani kajiuzulu au kafariki, Chama kilichoshinda Uchaguzi mkuu kitateuwa mwengine kuziba Nafasi
Hii haifai kwa sababu wananchi watawekewa mtu wasiyemchagua tutakuwa tumerudi nyuma kidemocrasia ni bora mtu aondoke na ubunge wake hata km ugombea binafsi utakuwa haujaruhusiwa atakayehama atalazimika kujiunga kwenye chama chochote chenye usajili wa kudumu aendelee kutumikia watu wake.
 
Wanabodi,
Salaam;

Wimbi la viongozi kuhama chama kwa kisingizio cha kumuunga mkono Rais,linaendelea.

Viongozi hawa waliochaguliwa kwa jasho na damu,wanaamua kuziacha nafasi zao na wanaenda kuomba kugombea nafasi zilezile ktk chama kingine. Mfumo huu unatuingiza kwenye gharama kubwa km Taifa.

Serikali inatumia pesa nyingi kufanya chaguzi ndogo ambazo ni chaguzi za kihuni kabisaa! Tunapoteza pesa serikalini,kwenye vyama na wagombea wenyewe. Wananchi nao wanapotezewa muda kwenda kwenye mikutano ya kampeni na kupiga kura..!

Bunge la Tanzania,kwa nn msipeleke mswada bungeni kuweka kipengele cha kufutwa kwa chaguzi ndogo,badala yake iwe chama kilichoondokewa na kiongozi wake,iwe kwa kufa,kufukuzwa au kujiudhuru,kiteue kiongozi mwingine na kisha tume imthibitishe. Hii itapunguza gharama hizi za kipuuzi. Na nna uhakika sheria hii ikipitishwa,hakuna mbunge wala Diwani atakayeachia ngazi...!!

Nawasilisha.
wazo zuri sanaaaaaaaa!!
 
Back
Top Bottom