Kimboka
JF-Expert Member
- Jun 29, 2012
- 353
- 163
Katika pitapita zangu mikoani na kuzungumza na makamanda wanaonesha wazi kuwa ni muda mwafaka kwa Dr Kitila kushika nafasi ya Dkt Slaa ktk nafasi ya Katibu Mkuu,
Sifa za Kitila Mkumbo hazina pingamizi kwa yeyote anaetaka mabadiliko;Kitila ni msomi anaetambua umuhimu wa mabadiliko,Hana makundi ndani ya chama,Kasaidia kutatua mizozo mingi ndani ya chama,Ni msema kweli daima,
Tukumbuke kuwa kitila amelimaliza kisiasa li Gaidi Mwigulu Nchemba uko iramba mpaka sasa halijafika iramba kwa hofu ya kuzomewa baada ya ziara nzito ya kitila mkumbo,Jesca kishoa na David Djumbe.
Tunatambua mchango mkubwa wa Dr Slaa ila kwa sasa tunahitaji mtu atakaepanga mipingo mikakati itakayotekelezeka bila kukigawa chama ktk makundi ili tuweze kuifikia salama nchi ya maziwa na asali.
VIVA MAKAMANDA, VIVA MABADILIKO.
Sifa za Kitila Mkumbo hazina pingamizi kwa yeyote anaetaka mabadiliko;Kitila ni msomi anaetambua umuhimu wa mabadiliko,Hana makundi ndani ya chama,Kasaidia kutatua mizozo mingi ndani ya chama,Ni msema kweli daima,
Tukumbuke kuwa kitila amelimaliza kisiasa li Gaidi Mwigulu Nchemba uko iramba mpaka sasa halijafika iramba kwa hofu ya kuzomewa baada ya ziara nzito ya kitila mkumbo,Jesca kishoa na David Djumbe.
Tunatambua mchango mkubwa wa Dr Slaa ila kwa sasa tunahitaji mtu atakaepanga mipingo mikakati itakayotekelezeka bila kukigawa chama ktk makundi ili tuweze kuifikia salama nchi ya maziwa na asali.
VIVA MAKAMANDA, VIVA MABADILIKO.
Utaratibu wa kumpata Katibu Mkuu wa CDM unajulikana na hii ya kupigiana kampeni kwenye mitandao sio mojawapo.
Mnaleta mijadala ambayo haipaswi kuwepo na kusababisha mitafaruku isiyo na maana na kupoteza muda wa kuidhoofisha CCM.
Nina kazi kubwa ya kuelimisha vijana wetu katika vyuo vikuu na ninaifurahia kazi hii. Mchango mdogo ninaotoa kwa CDM kwa nafasi niliyo nayo sasa unatosha na ninaridhika.