PENDEKEZO:CCM tumtose haraka sana Mwigulu

PENDEKEZO:CCM tumtose haraka sana Mwigulu

Status
Not open for further replies.
Irrevant, Kikwete atamtosa tu mwigulu hana jinsi watanzania wamempa somo kata zote alizokwenda kusimamia uchaguzi kabamizwa
Waungwana tulishajua tu, hali itakwenda mrama tu.
Yaani mwananchi akienda kwenye mkutano mmoja tu wa Mwigulu hatamani kurudia tena kuja kumsikiliza. Ni mambo ya aibu na ajabu kabisa huwa anazungumza.

Toka nimeijua CCM ama TANU sijawahi kuona matokeo mabaya kabisa kwa CCM katika chaguzi ndogo za ngazi ya chini, ila kipindi hiki nimeshuhudia, tena mahali ambapo kampeni zinaongozwa na Mwigulu.

Kikwete huwa ni mzito na mgumu kumfukuza mteule wake ila yakimzidi huwa anawatumua kwa shingo upande.

Tabia ni moja tu, Kikwete akishinikizwa na wanaCCM wenzake huwa anachukua hatua. Alifanya kwa Makamba senior kisha kwa Mukama.
I think soon he will do the same to Mwigulu.
 
Hapana, msimtoe. Ni mtu anayeiweza kazi aliyopewa na mwenyekiti wake na katibu wake. Amefanikiwa kwa asilimia nyingi, Amekuwa mbunge, naibu katibu, waziri, spika, msomi, jaji, hakimu, shahidi wa duniani na mbinguni msemaji wa chama kwa wakati mmoja na amemudu mambo yote. Nashauri mwongezeni na Lusinde kwenye timu yake kwani anaweza pia. Wa kumtoa ni mwenyekiti wake na yupo kimya kwa yote anayofanya, inamaanisha ameridhika na anachokifanya. Msimuonee gere kijana wetu mwacheni apige kazi
Mtajuta mwaka huu na kazi ndo kwanza inaanza,mwigulu eeeeeeeeeeeeeeeeee njoo.......uone .....watu hawalali kwa ajiri yako.
 
Mwigulu anachapa kazi, Chadema acheni fitina zenu, kama angekua hafanyi kazi iramba hamkupata hata kijiji kimoja, katika kata 22 ameshinda 16. na bado, chapa kazi mh. mwigulu na nina amini ccm hajakosea kukupa nafasi hiyo.
 
kwi kwi kwi ! wakiandamana piga! 2015 cdm,kiongozi wakambi ya upinzani bungeni mbatia.
 
Mwigulu anachapa kazi, Chadema acheni fitina zenu, kama angekua hafanyi kazi iramba hamkupata hata kijiji kimoja, katika kata 22 ameshinda 16. na bado, chapa kazi mh. mwigulu na nina amini ccm hajakosea kukupa nafasi hiyo.

shaabani CCM tunarudi nyuma kwa kasi sana wakati wapinzani wetu wanakwenda mbele kwa kasi. Sijui itakuwaje mwisho wa siku.

Takwimu za matokeo kiujumla sio nzuri kwa CCM, wenzetu wapinzani wako mbele kidogo.
Japokuwa tumepata kata 16 lakini tumepungua sana kwani tumepoteza kata 4 kirahisi na kwa aibu kubwa sana.

Tusipofanya kitu sasa tutaendelea kupata maumizi kila siku.
Siasa za Matusi, Hongo, Fujo, Vitisho hazitufai CCM, wananchi wengi hawazipendi kabisa. Ni lazima tuchukue hatua kubadilika sasa, tusiogope kushindwa kwenye Chaguzi kwani kushindwa ni sehemu ya matokeo ya kisiasa, tukazane kuanza kufanya siasa safi tu.
 
Last edited by a moderator:
ccm ni janga mwigulu ni shetan ktk jamiii, na hiii yote ni kutokana na matendo yake
 
Mimi nitahuzunika sana mkimtosa Mwigulu, anatosha kuimarisha upinzani nchini.Siasa zake zimewafanya wananchi waongeze imani kwa CHADEMA na kujua undani wa kukosekana kwa siasa safi kama alivyotaka Mwl.Nyerere ndani ya CCM!
 
Mwigulu anafaa sana.. Huyu ndiye anaweza kupambana na Chadema si unaona wanaccm wooooote wametua zigo kwake. Halafu timu yake imekamilika.. (akina Mtela..) Timu ya ushindi.
 
hivi ilikuaje ccm wakaingia cha kike kumpa jamaa uongozi...?!!!
 
Mimi nitahuzunika sana mkimtosa Mwigulu, anatosha kuimarisha upinzani nchini.Siasa zake zimewafanya wananchi waongeze imani kwa CHADEMA na kujua undani wa kukosekana kwa siasa safi kama alivyotaka Mwl.Nyerere ndani ya CCM!

Nakubaliana na wewe, kupitia utendaji wa mwigulu tabia ya ndani ya ccm inadhiirika, kama mauaji na utesaji ulivyofunuliwa kipindi hichi. Viongozi jamii ya Mwigulu huarakisha kutimizwa kwa unabii, wa mwache aendelee kuwepo na upinzani utaimarika japo itagharimu hata uhai wa watu!
 
Eti sisiemu ina hazina ya Viongozi.... Viongozi wenyewe ndo kina Mwigulu?!
 
Hivi ilikuwaje CCM wakakosea kumpa Mwigulu uongozi? Ka!!!
 
Hivi ilikuwaje CCM wakakosea kumpa Mwigulu uongozi? Ka!!!

Hiroshima mpaka sasa bado sijajua ni vigezo gani hasa Kikwete alitumia kumteua Mwigulu.

Mwanzoni nilidhani kwa kuwa alikuwa msomi wa Uchumi na alikuwa akifanya kazi BOT basi ikawa sababu ya kuteuliwa kuwa mweka hazina wa CCM ikitegemewa kuwa Atafufua miradi ya kiuchumi iliyodorora, atabuni vyanzo vipya vya mapato kwa CCM na mwisho atadhibiti matumizi holela ya pesa za CCM. Lakini toka aliposhika uweka hazina hali ya CCM kiuchumi ikawa mbaya zaidi yaani hata repoti za michanganuo za mapato na matumizi alishindwa kuandika ama kuwasilisha kwa wakati, Sasa CCM imefikia mahali makada wenye nyanzifa tunatoa pesa zetu mifukoni ili kuendesha chama lakini pia tunapitisha bakuli kuomba kwa matajiri na wafanyabiashara wakubwa ili watuchangie.

Kwenye hii secretarieti mpya Mwigulu alikuwa atupwe nje sambamba na Januari Makamba na John Chirigati walivyotupwa lakini kwa sababu bado alikuwa jikoni akiendelea 'kupika' mikakati dhidi ya Chadema(Project ya Mwisho wa Chadema 2013) ilibidi abaki mpaka 'Chakula kiive',
Bahati mbaya Project ya Kwanza muhimu ikashindwa(Masalia), Project ya Pili ikashindwa vibaya(Tamthilia ya Lwekatare) na Project ya Tatu imezaa mauaji na Aibu(China weapons).

Sasa hana ajenda mpya amebaki kulaumu tu kuwa kuna baadhi ya makada wa CCM na vyombo vya dola ndio wamemkwamisha kwa sababu wanashirikiana na Chadema kumhujumu kwa makusudi.
 
Last edited by a moderator:
Hatoswi mtu hapa,kijana anafanya kazi yake vizuri sana. Cdm wanakesha kumfikiria huyu jamaa.

Kweli mkuu itafika wakati Tanzania nzima makaburi yataota kama vichuguu.kwa unyama huu anao ufanya lazima Chadema wamufikirie.
 
Mwigulu anafaa sana.. Huyu ndiye anaweza kupambana na Chadema si unaona wanaccm wooooote wametua zigo kwake. Halafu timu yake imekamilika.. (akina Mtela..) Timu ya ushindi.

Alinda huyo Mwigulu hafai kabisa, Chadema wanapenda kupambana na watu kama Mwigulu kwenye siasa kwa sababu watawashinda kwa urahisi sana kwa hoja.

Hao vijana waliofukuzwa Chadema na kuja kuhifadhiwa CCM, hawana msaada wowote kwa CCM yetu, wamekuja kuganga njaa tu, siku tukiwanyima chakula watatugeuka na kuanza kuropoka maovu ya CCM yanayofanywa kwa siri. CCM tuna vijana wazuri sana walioiva kiitikadi lakini hawapewi nafasi, baadhi yao tayari wameshaanza kutimkia Chadema, kwa mfano Mawazo, Milya nk.
 
Last edited by a moderator:
Mwigulu Nchemba ni naibu katibu wa CCM Tanzania bara(Tanganyika!) na pia ni mbunge wa Iramba magharibi.
Mwenendo wake binafsi wa kisiasa ndio umegeuka kuwa taswira ya mwenendo wa CCM kwa ujumla kwa sasa.

Mimi na baadhi ya wanaCCM wenzangu tunaoamini katika siasa za UTU, AMANI na UUNGWANA ambazo ndio msingi wa siasa za TANU toka enzi hizo, tunapenda kutoa wito kwa mamlaka za juu za CCM kufanya maamuzi sahihi na ya haraka kwa kuamua kumtimua ndani ya CCM Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kwa sababu:

1/Ameharibu na ataendelea kuharibu taswira nzima ya CCM katika jamii kutokana na aina ya siasa anazofanya ambazo ni Matusi, Uzushi, Fujo, Hongo, Vitisho na sasa Mauaji.

2/Hasara za kiuchumi, kijamii na kisiasa ambazo CCM inazipata kutokana na utendaji duni sana wa Mwigulu kisiasa.

3/Hatari mbaya za kisiasa ambazo zinainyemelea CCM kutokana na makosa makubwa ya makusudi yanayofanywa na Mwigulu katika siasa ambayo soon wapinzani wa CCM tayari wameshaanza kuyatumia tena vizuri sana.

*Please wanaCCM wenye kuipenda kwa dhati CCM ya enzi za Nyerere(TANU), tuungane pamoja katika hili.

Tangu lini ulikuwa mwana CCM?

haumjui Mwigulu wewe.....ww wasikilize chadema tu na endelea kuwa mwanachama mwaminifu wa chadema
 
tuliwaeleza chadema kuwa wakipata watu aina ya mwigulu watakoma

sasa NAPE , MWIGULU NA MAKAMBA WANAIUA CHADEMA, TUpa mbali Kinana
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom