masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Pamoja na kumpongeza Nape,jambo ambalo ni jema, ujue visasi ni tabia ya kihutu.Haya Jirani wa pale Kwako Mbezi Beach ukiwa umepakana na Hekalu la Tajiri wa Kihaya Katunzi na Mtoto wa Mjini Nape Nnauye Mungu akupe nini tena Komredi?
Kama kuna Kitu ambacho Waziri Nape utakifanya na Mimi GENTAMYCINE kukifurahia na Kuunga mkono tena kwa 100% ni Kwanza Kumshughulikia Ndugu Paul Makonda ( aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ) kwa Kukufanyia yale Madhila yote ukakoswakoswa Kupigwa Risasi ya Utosini pale maeneo ya St. Peters Oysterbay.
Tafadhali Nape usimcheleweshe huyu 'Gaidi na Fisadi Matege' bali upesi sana andaa Mtu akafungue Kesi ya Kuivamia CMG ( Clouds Media Group ) au Shirikiana na Saed Kubenea ambaye alishaanza Mchakato wa Kumfungulia Kesi ili akamatwe upesi Kesi ianze dhidi yake kisha baada ya hapo tutawaomba na wale Wengine aliowaumiza Kimaslahi ( hasa Kiuchumi ) kwa Kuwaonea akina Yusuf Mehboub Manji warejee Tanzania nao wamfungulie Kesi ili hatimaye akaozee kabisa Gerezani.
Halafu Comrade Nape ukiapishwa tu Kesho hapo Dodoma 'Kudadadeki' ukiingia hapo Ofisini Kwako Wizarani anza Kufyagia hapo Watendaji ( Maafisa ) ambao ni Sita ( 6 ) kwani ni Wanafiki na Kipindi kile 'Ulipotumbuliwa' walifurahi na Kufanya Bonge la 'Pati' maeneo ya Mikocheni na wakawa wanakusema vibaya na Kukuzidishia Uadui na aliyelala mazima pamoja na Wasaidizi wake.
Nape usipodili na Makonda ( hasa kwa Wewe pia Kumlipizia Kisasi kwa aliyokufanyia ) basi 'Ushkaji' nawe utafikia Kikomo kwani Watu tuliokuwa tukikupenda mpaka Kukuunga mkono ( GENTAMYCINE ) nikiwemo tuliumia na Kusikitika mno 'Ulipotumbuliwa' kwa Chuki tu za Mtu ( Watu ) wakati hukuwa na baya na tena ulikuwa ni mpenda Haki na Usawa kwa wana Tasnia na Watanzania wengi.
Hongera mno tu Nape kwa huu Uteuzi!!
Msiturudishe tulikotoka.
Kama kuna kesi ya jinai au madai basi aliye athirika ndiyo aende kudai haki.