Kama mwandishi wa habari Talib Ussi amesimamishwa kazi kwa kutoa ripoti ya corona, ni kwanini Makonda anaendelea na kazi kwa kufanya kosa hilo hilo?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Tulielezwa kuwa wenye mamlaka ya kutangaza wagonjwa wa corona nchini ni watu watatu, ambao ni waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, waziri mkuu Kassim Majaliwa na Rais mwenyewe, John Magufuli

Upande wa Zanzibar, anayeruhusiwa kutoa ripoti yoyote ya wagonjwa wa corona, ni waziri wa afya wa huko, Hamad Rashid Mohammed

Kinachosngaza ni kuwa imetolewa taarifa na wizara ya habari Zanzibar, kuwa imemsimamisha kazi kwa miezi 6, mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Talib Ussi, kwa madai kuwa ametoa ripoti ya mgonjwa wa corona, bila ridhaa yake mwenyewe ugonjwa, ambayo wizara hiyo imesema ni kinyume cha sheria, kwa kuwa huko Zanzibar, anayepaswa kutoa ripoti hizo ni waziri wa Afya wa Zanzibar pekee.

Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa, je sheria zetu zina double standards?

Kwa kuwa siku za hivi karibuni, mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda, alifanya kosa la aina hiyo hiyo, kwa kumtangaza mgonjwa wa corona hadharani, ambaye ni mtoto wa Mbunge wa upinzani, Mheshimiwa Mbowe, lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yake!

Hata waziri wa Afya alipoulizwa baadaye alilisitiza hilo kuwa wenye mamlaka ya kuwatangaza wagonjwa wa corona kwa upande wa Tanzania bara , ni yeye mwenyewe waziri wa afya, waziri mkuu, Kassim Majaliwa na Rais mwenyewe, Mheshimiwa John Magufuli

Ndipo hapo ninapojiuliza, inakuwaje mwandishi wa habari wa Tanzania Daima, asimamishwe kazi kwa kosa tunaloambiwa ni la kumtangaza mgonjwa wa Corona, bila ridhaa yake, wakati Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda, akifanya kosa hilo hilo, lakini akiachwa bila kuchukuliwa hatua yoyote?

Huu utekelezaji wa Double standards wa sheria zetu, kwa maana ya upendeleo kwa baadhi ya watu, ndiyo unaoelekea kuliangamiza Taifa letu la Tanzania
 
Kwa kuwa siku za hivi karibuni, mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda, alifanya kosa la aina hiyo hiyo, kwa kumtangaza mgonjwa wa corona hadharani, ambaye ni mtoto wa Mbunge wa upinzani, Mheshimiwa Mbowe, lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yake!
Hili limewauma sana bavicha, ukweli ni kwamba Mbowe alikua anaambukiza watu kwa makusudi
 
Ni sawa na kusema mbona watu wanaranda randa mitaani Mombasa wakati Rais Museveni ameshatangaza lockdown nchi nzima.

We keep preaching and reminding the citizenry: healthcare IS NOT a union matter.

AFYA SI JAMBO LA MUUNGANO
 
Unawezaje kumsimamisha kazi mtu ambaye hujamwajiri wewe?
Huyu mwandishi ni mwajiriwa wa Free Media Ltd, anasimamishwaje kazi na serikali ya Mapinduzi Zanzibar?

Nyie wasomaji wa magazeti kweni huyo mwandishi alitangaza nini mpaka kupewa adhabu hiyo?
 
Angekuwa wa Uhuru/Mzalendo huenda asingeguswa huyo mwandishi

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini kwa kuwa ni mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, ndiyo sababu ya kuangushiwa lungu lote hilo!

Hii double standards inayoendelea hapa nchini, hakika inalipeleka Taifa pabaya......
 
Hili limewauma sana bavicha,ukweli ni kwamba mbowe alikua.anaambukiza watu kwa makusudi
kabombe
Kama ni hivyo, je huyu aliyetangazwa na mwandishi wa habari wa Tanzania Daima, si alifanya vivyo hivyo kwa kuepusha vifo vya watu wengine?

Je ni haki kuangalia ni nani amefanya kosa fulani ili uchukue hatua?
 
Hili limewauma sana bavicha,ukweli ni kwamba mbowe alikua.anaambukiza watu kwa makusudi
Ndyomaana siwezi tumia sanitizer iliyotengenezwa na wanaCCM maana hawachelewi kuweka ndumba zai ili kufanya watu misukule wa CCM. Ina kama huyu akili yake ni kama msukule tu. Lazima kuna curse mnafanyiwa za kuwapumbaza, sio bure.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom