Pato la Mtanzania mwaka 2020 ni Tsh. 2,653,790

MUSIGAJI

JF-Expert Member
Dec 26, 2014
2,187
2,462
Watanzania wenzangu, hongereni kwa nchi yetu kutimiza miaka 60 ya Uhuru.

Jana katika hotuba Yake kwa Taifa Mh Rais atoa takwimu mbalimbali ya wapi tulipokuwa kipindi tunapata Uhuru na wapi tumefikia baada ya miaka 60 ya Uhuru.

Moja ya takwimu zilizotolewa ni pato la Mtanzania mwaka 2020. Mh Rais ametanabaisha kuwa mwaka 2020 pato la Mtanzania lilikuwa shilingi 2,653,790 kwa mwaka sawa na shilingi 221,149.16 kwa mwezi.

Binafsi takwimu hii, ya pato la Mwananchi limenitafakarisha sana.Ukiangalia hali za wananchi waliowengi achilia mbali kupata shilingi 221,149 kwa mwezi hata kuitengeneza 100,000 ni changamoto kubwa mno, sasa hii ya laki mbili plus kwa mwezi nazidi kutafakari.

Lakini kwa kuwa Mh Rais anazo taarifa kutoka katika ofisini mbalimbali ikiwemo ofisi ya Taifa ya Takwimu, Naomba niwapongeze Watanzania kwa kuwa na uwezo wa kutengeneza 2,653,790 kwa mwaka.

Hongereni kwa Uhuru.
 
Unajua wakati mwingine muwe mnakumbuka hata shule mlivyosoma Kuna hesabu ndogo tu ya wastani sijui kama mnaikumbuka mtoa mada kaandika kishabiki kutaka kumweka mama aonekane hafai mkiwa watu watatu mmoja ana mia mwingine ana ishirini mwingine ana kumi ukiambiwa Sena Hawa watu wana wastani wa shilingi ngapi utasema ishirini? Au utasema mia? Lazima ujumlishe halafu ugawanue kwa idadi Yao lakini mtu anakuja kishabiki bila hata kutumia akili anakejeri kama hukusoma Rudi shule
 
Tatizo vipato vikiongezeka kwao na koo zao basi wanatujumuisha wote, hembu watuache na takwimu zao.
 
Unajua wakati mwingine muwe mnakumbuka hata shule mlivyosoma Kuna hesabu ndogo tu ya wastani sijui kama mnaikumbuka mtoa mada kaandika kishabiki kutaka kumweka mama aonekane hafai mkiwa watu watatu mmoja ana mia mwingine ana ishirini mwingine ana kumi ukiambiwa Sena Hawa watu wana wastani wa shilingi ngapi utasema ishirini? Au utasema mia? Lazima ujumlishe halafu ugawanue kwa idadi Yao lakini mtu anakuja kishabiki bila hata kutumia akili anakejeri kama hukusoma Rudi shule
Mkuu, nia yangu ni njema tu, Nimesema pia Mh Rais anavyo vyanzo vya Takwimu. Sisi tunapaswa kutafakari tu, ukijikuta unaishi chini ya pato hilo ujue wewe ni fukara kabisa na unaishi chini ya Wastan.
 
Unajua wakati mwingine muwe mnakumbuka hata shule mlivyosoma Kuna hesabu ndogo tu ya wastani sijui kama mnaikumbuka mtoa mada kaandika kishabiki kutaka kumweka mama aonekane hafai mkiwa watu watatu mmoja ana mia mwingine ana ishirini mwingine ana kumi ukiambiwa Sena Hawa watu wana wastani wa shilingi ngapi utasema ishirini? Au utasema mia? Lazima ujumlishe halafu ugawanue kwa idadi Yao lakini mtu anakuja kishabiki bila hata kutumia akili anakejeri kama hukusoma Rudi shule
Kuhusu wastani ni sawa Mkuu, kama ulivyoeleza. Ila ukitafakakari vizuri utagundua kuwa hizo data ni za jikoni, na wala hazina uhalisia wowote. Kipato cha 7000+ kwa siku kwa kila mtanzania hata kwa kutumia Wastani ni uongo. Maana yake tunaamimishwa kwamba tunaishi/kutengeneza zaidi ya Dola mbili kwa wastani kwa siku.

Hizo takwimu zimetoka kwa Chef, hata kama Mo Dweji na Bakhresa watakuwa wametubeba kupitia ukwasi wao. Kwa hali ilivyo mbaya, ni aibu kwa Kiongozi kutamka wastani huo tena kwa tabasamu. Wastani wa 2$+ zitoke kwenye ajira gani, viwanda gani, kilimo gani, ujasiriamali gani? Maisha yetu tunayajua wenyewe brother! Hiyo 2$+ ni kejeli.
 
Back
Top Bottom