Kama wewe ni Byesige wa Uganda mwaloni kabisa na Ziwa letu pendwa la Victoria ninakuwa na wasiwasi na hicho unachokizungumzia. Lakini kama ni Byesige wa kuchonga (Mrs) na hasa yule toka pwani ya Bahari ya Hindi, basi itakuwa umeongea ukweli. Ladha ya samaki hutegemea pia na uzoefu wa kuwala hao samaki. Mtu toka Ziwani ukimweleza utamu wa ngisi, nguru, pweza n.k atakushangaa sana. Kadhalika yule atokaye ukanda wa Pwani akiambiwa utamu wa nembe, domodomo, ningu na kamongo atakushangaa mpaka umshangae.