Kwa ninavyoelewa ni kifungo cha nje anachopewa mfungwa anaekaribia kumaliza kifungo chake cha ndani na hupewa hiyo parole iwapo atakuwa ameprove kubadilika tabia na katika kipindi hicho cha parole atakuwa chini ya uangalizi.
parole ni mbadala wa kifungo cha gerezani. kama alivotangulia kueleza mchangiaji wa kwanza, hii hutolewa kwa mfungwa fulani aieonesha kubadili tabia pale gerezani. baada ya kutolewa nje atatazamiwa kwa kipindi maalum. endapo ataonesha kusahihika basi ataachiwa huru. hii inasimamiwa na THE PAROLE BOARD. Aina hii ya kifungo* hutumika zaid nchini MAREKANI. inafanana sana na ile inaitwa PROBATION ambayo kwa TANZANIA inasimamiwa na sheria iitwayo THE PROBATION ACT.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.