Wiki hii imeripotiwa katika taarifa ya habari ya saa mbili ITV kwamba mama mmoja mjane kiwanja chake kimevamiwa na mfanyabiashara maarufu Marijani Msofe au kama anavyojulikana mtaani Papa Msoffe. Mama huyu alisema Polisi walimtoa na kumuomba Waziri Mkuu amsaidie.
Leo tarehe 04/11/2011 taarifa ya habari ya saa mbili ya ITV naona huyu mama akitoa shukrani kwamba Waziri Mkuu amemsaidia kumtoa mvamizi kwakumpa siku 7. Katika taarifa ya habari hiyo watu walichangia na kuelezea jinsi wanyonge wanavyodhulumiwa na watu wenye fedha kwakutumia vyombo vya umma na hasa Polisi. Natumai taarifa hii itarudiwa tena kesho asubuhi saa kumi na mbili au saa moja katika kituo hichohicho cha ITV.
Swali nililojiuliza ni kwamba Polisi waliezaje kumtoa mama wa watu ambaye tunaambiwa alikuwa na documents zote hali ambayo inaniambia ndio maana ikawa rahisi kwa waziri mkuu kutoa uamuzi wa haraka. Mama huyu mjane nampa hongera kwa jinsi alivyopigana kijasiri kwani ni watu wachache sana wanaweza kupitia ngazi zote alizopitia.
Maswali ambayo nabaki nayo ambayo sijapata majibu na naomba wadau wanifumbue macho ni haya?
1. Huyu Papa Msoffe au marijani msoffe ni nani hasa?
2. Amewezaji kutumia Jeshi letu kufanya hayo aliyofanya bila hata Polisi mmoja wa ngazi za juu kuthubutu kukemea, kuwawajibisha polisi waliohusika au hata kutoa tamko?
3. Inawezekanaje serekali inampa mhalifu siku 7 arudishe alichoiba bila hata yakumfungulia shitaka la hata mstari mmoja?!!
4. Mama Tibaijuka ambaye tunamuamini ameweza kumtosa mama mjane na kuwekwa mfukoni na hawa waalifu mpaka waziri mwingine kuingilia na kutoa ufumbuzi?
Tutafika kweli? Labda kuna ambalo limejificha, naomba nipewe mwanga.
Leo tarehe 04/11/2011 taarifa ya habari ya saa mbili ya ITV naona huyu mama akitoa shukrani kwamba Waziri Mkuu amemsaidia kumtoa mvamizi kwakumpa siku 7. Katika taarifa ya habari hiyo watu walichangia na kuelezea jinsi wanyonge wanavyodhulumiwa na watu wenye fedha kwakutumia vyombo vya umma na hasa Polisi. Natumai taarifa hii itarudiwa tena kesho asubuhi saa kumi na mbili au saa moja katika kituo hichohicho cha ITV.
Swali nililojiuliza ni kwamba Polisi waliezaje kumtoa mama wa watu ambaye tunaambiwa alikuwa na documents zote hali ambayo inaniambia ndio maana ikawa rahisi kwa waziri mkuu kutoa uamuzi wa haraka. Mama huyu mjane nampa hongera kwa jinsi alivyopigana kijasiri kwani ni watu wachache sana wanaweza kupitia ngazi zote alizopitia.
Maswali ambayo nabaki nayo ambayo sijapata majibu na naomba wadau wanifumbue macho ni haya?
1. Huyu Papa Msoffe au marijani msoffe ni nani hasa?
2. Amewezaji kutumia Jeshi letu kufanya hayo aliyofanya bila hata Polisi mmoja wa ngazi za juu kuthubutu kukemea, kuwawajibisha polisi waliohusika au hata kutoa tamko?
3. Inawezekanaje serekali inampa mhalifu siku 7 arudishe alichoiba bila hata yakumfungulia shitaka la hata mstari mmoja?!!
4. Mama Tibaijuka ambaye tunamuamini ameweza kumtosa mama mjane na kuwekwa mfukoni na hawa waalifu mpaka waziri mwingine kuingilia na kutoa ufumbuzi?
Tutafika kweli? Labda kuna ambalo limejificha, naomba nipewe mwanga.