Papa Francis kuongoza ibada ya Wakatoliki Misri

Papa Francis kuongoza ibada ya Wakatoliki Misri

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2017
Posts
392
Reaction score
954
_95838385_papa-bbc.jpg


Papa Francis ataongoza misa ya Wakatoliki nchini Misri hii leo katika siku ya pili na ya mwisho ya ziara yake ya Cairo.

Ibada hiyo itafanyika katika uwanja wa wanajeshi, na itaongozwa kwa lugha ya Kiarabu na Kilatino.

Anatarajiwa kurejelea ujumbe wake wa jana ambapo aliwarai viongozi wa dini zote kukemea uhalifu wowote unaotekelezwa kwa misingi ya kidini.

Jana Papa Francis alizuru kanisa moja mjini Cairo Misri ambapo takriban Wakristo 30 waliuawa katika shambulio lililotekelezwa na wapiganaji wa Islamic State mwezi Disemba mwaka jana.

Aliandamana na kiongozi wa kanisa la Coptic nchini humo, Pope Tawadros.
 
Back
Top Bottom