Papa Francis aomba kukutana na Putin, achuniwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Papaa.JPG

Picha ya Maktaba, Rais Vladimir Putin (kulia) alipokutana na Papa Francis, Vatican mnamo Julai 4, 2019.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis amesema kuwa aliomba kukutana na Rais wa Urusi, Vladimir Putin ili kumshawishi kumaliza vita dhidi ya Ukraine lakini hajapata majibu.

Papa Francis wakati vita ikiwa na wiki tatu tangu kuanza Februari 2022 alituma maombi hayo kwa lengo la kutafuta amani lakini hajajibiwa na bado nia yake hiyo ipo.

“Nahisi Putin hatakubali kuwa na mkutano wenye lengo hilo, lakini anaweza kutuma watu wake tukazungumza,” – Papa.

Source: Reuters
 
Aende Urusi atapokelewa hawawezi kumfukuza.
Hakuna mtawala aliwahi kuwa mjuaji mbele ya Vatican.Huu ndiyo uhalisia,sisi huku tunaoishi kwa ulimwengu wa tatu na tukicomment hapa JF tena kwa kutegemea technologia ya huyo huyo tunaejidai kumpuuza tungekaa na kutulia tuone wanaoiendesha Dunia wanasemaje.

Tukiendelea na ujuaji wetu tusijeshangaa hata hiki kijiwe tunachotolea povu kikatoweka,tukabaki kufura na hasira zetu tukiwa kwa Ulimwengu wa giza.
 
Hakuna mtawala aliwahi kuwa mjuaji mbele ya Vatican.Huu ndiyo uhalisia,sisi huku tunaoishi kwa ulimwengu wa tatu na tukicomment hapa JF tena kwa kutegemea technologia ya huyo huyo tunaejidai kumpuuza tungekaa na kutulia tuone wanaoiendesha Dunia wanasemaje.Tukiendelea na ujuaji wetu tusijeshangaa hata hiki kijiwe tunachotolea povu kikatoweka,tukabaki kufura na hasira zetu tukiwa kwa Ulimwengu wa giza.
Mastory ya town tu. Influence ya vatican now sio kihivyo dunia ya leo. Nchi nyingi zinaikataa, hao warusi wenyeww waorthodox, U.K nao ndo Waanglikana, US inasemekana ni ngumu kuwa raisi ukiwa mkatoliki.
Ingekuwa na influence kama zamani, hizi scandal za mapadri zisingesikika.
 
Back
Top Bottom