Papa ateua maaskofu wasaidizi wawili Dar

Papa ateua maaskofu wasaidizi wawili Dar

Mh. Padre Eusebius Nzigilwa na Mh. Padre Salutaris Libena wateuliwa kuwa ni Maaskofu wasaidizi, Jimbo kuu la Dar es Salaam

Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amewateuwa waheshimiwa sana Padre Eusebius Alfred Nzigilwa pamoja na Padre Salutaris Melchior Libena kuwa maaskofu wasaidizi wa Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Askofu mteule Eusebius Alfred Nzigilwa alizaliwa tarehe 14 Agosti, 1966, Jijini Mwanza. Alipata masomo yake ya sekondari Seminari Ndogo ya Mtakatifu Petro, Jimbo Katoliki la Morogoro. Mnamo mwaka 1988 alikwenda mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa mujibu wa sheria na baadaye, alijiunga na Seminari ya Kibosho, Jimbo Katoliki la Moshi, kwa masomo ya Falsafa na yale ya Taalilimungu katika Seminari kuu ya Kipalapala, Jimbo kuu la Tabora.

Alipewa daraja takatifu ya Upadre tarehe 23 Juni, 1995 kama Padre wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Kuanzia mwaka 1995-1996 alikuwa ni Padre mlezi, nyumba ya malezi, Jimbo kuu la Dar es Salaam, iliyoko Parokia ya Mtongani, Kunduchi. Aliwahi pia kuwa ni mkurugenzi wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu kuanzia Mwaka 1996 hadi Mwaka 1997.

Baadaye aliteuliwa kuwa Gombera wa Seminari Ndogo ya Visiga, Jimbo kuu la Dar es Salaam kuanzia mwaka 1997-1999. Akaendelea na masomo ya juu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alikojipatia shahada ya kwanza ya elimu. Baada ya masomo, aliteuliwa kwa mara nyingine tena kuwa Gombera wa Seminari Ndogo ya Visiga, kuanzia 2003 hadi 2008 alipolazimika kwa mara nyingine tena kurudi Chuo kikuu cha Dar es Salaam kumalizia masomo yake katika Sayansi ya Elimu.

Askofu mteule Salutaris Melchiol Libena alizaliwa mnamo tarehe 23 Novemba, 1963 katika Parokia ya Itete, Wilaya ya Ulanga, Jimbo Katoliki la Mahenge, Tanzania. Baada ya elimu yake ya msingi, alibahatika kuchaguliwa kuendelea na masomo ya Sekondari katika Seminari Ndogo ya Kasita, Jimbo katoliki la Mahenge na baadaye alihamia Seminari Ndogo ya Mafinga, Jimbo Katoliki la Iringa.

Alipata majiundo yake ya Kipadre kwenye Seminari kuu ya Mtakatifu Augustino, Peramiho, Jimbo kuu la Songea. baada ya masomo yake ya kipadre, alipewa daraja takatifu la Upadre tarehe 29 Juni, 1991 akawa ni Padre wa Jimbo katoliki la Mahenge, hadi kuteuliwa kwake na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita kuwa Askofu msaidizi wa Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Alibahatika kuwa ni mwalimu na mlezi wa Seminari ndogo ya Kasita, Jimbo Katoliki la Mahenge. Akateuliwa kuwa Paroko na Dekano wa Dekania ya Itete, wakati huo huo akiwa ni Gombera wa kituo cha Malezi cha Mtakatifu Patrick.

Kuanzia Mwaka 1999 hadi 2001 aliendelea na masomo ya juu katika Taasisi ya Liturjia ya Kipapa ya Mtakatifu Anselmo, iliyoko mjini Roma. Kwa muda mfupi aliteuliwa kuwa ni mlezi na mwalim katika Srminari Ndogo ya Kasita, Jimbo Katoliki la Mahenge, kabla ya kuhamishiwa Jimbo katoliki la Bukoba, kuwa Jaalim wa liturjia, Seminari kuu ya Ntungamo tangu 2002-2003.

Mheshimiwa padre Salutaris Libena alihamishiwa Seminari kuu ya Kipalapala, Jimbo Kuu la Tabora kuwa Jaalim, Padre wa maisha ya kiroho na Jaalim wa taaluma seminarini hapo.

Hili ni tukio la kihistoria kwa Jimbo kuu la Dar es Salaam kupata maaskofu wawili wasaidizi kwa mpigo. Jimbo kuu la Dar es Salaam linaendelea kupanuka na idadi ya waamini inaongezeka maradufu.
 
Ni ukweli kaka. Kama una jamaa yako unamfahamu ni padre, mwulize. Ndivyo wanavyoapa.

Na wewe umeapa kusema uwongo? Kuapa kupelekwa popote siyo kuapa kupelekwa 'anyhow'. Huwa kuna matayarisho yake na consultation kwa padre mhusika inabidi akubali mwenyewe. Walau nina 'experience' ya kutosha kwa hili.
 
Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!

Acha kuargue kwa vitu usivyovijua bana. Unafikiri anasoma kwa siri? Mambo ya Kanisa yanaenda kwa mipangilio na wamehakikisha shule atamaliza na appoitment hiyo haitaathiri shule yake hata kidogo. Unajua ni kwanini wameteuliwa wawili? Unajua nani kamtuma asome hiyo shule na kwanini aamriwe aache, kwa manufaa ya nani? what about costs ambazo walishaincur ktk shule hiyo? Mambo yote hayo yapo ktk planning bana,acha story za kijiweni ktk masuala ya Kanisa.
Hongereni wateuliwa tunawatakia kazi njema!
 
Acha kuargue kwa vitu usivyovijua bana. Unafikiri anasoma kwa siri? Mambo ya Kanisa yanaenda kwa mipangilio na wamehakikisha shule atamaliza na appoitment hiyo haitaathiri shule yake hata kidogo. Unajua ni kwanini wameteuliwa wawili? Unajua nani kamtuma asome hiyo shule na kwanini aamriwe aache, kwa manufaa ya nani? what about costs ambazo walishaincur ktk shule hiyo? Mambo yote hayo yapo ktk planning bana,acha story za kijiweni ktk masuala ya Kanisa.
Hongereni wateuliwa tunawatakia kazi njema!

Kweli kabisa!
 
Hata miezi miwili haijapita tangu kuhamishwa kwa askofu Methodius Kilaini kwenda kuwa askofu msaidizi wa Bukoba, Papa Benedict XVI amewateua mapadri wawili kuwa maaskofu wasaidizi wa jimbo kuu la D’Salaam. Wawili hao ni Padri Salutaris Libena na Padri Eusebius Nzigilwa.

Wakati askofu Kilaini alikuwa na Phd. Sasa jimbo limempata professa kwani mmoja wa hao watakaokuwa maaskofu wasaidizi ni Professa (Padri) Salutaris Libena ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa na ni mhadhiri kwenye seminari kuu ya Kipalapala iliyoko nje ya mji wa Tabora. Vilevile alikuwa mkurugenzi wa kiroho au spiritual director wa seminari hiyo. Yeye (Libena) alikuwa ni padri wa jimbo la Mahenge kule kwa askofu Ndorobho nadhani na nimzaliwa wa Itete.

Mwenzake Padri Eusebius Nzigilwa ni padri wa jimbo la D’Salaam na ni mzaliwa wa Mwanza na amewahi kuwa rector wa seminary ndogo ya Visiga iliyoko mkoa wa Pwani karibu na Kongowe.

Hivyo jimbo kuu la D’Salaam sasa linakuwa na maaskofu watatu yaani Kadinali Polycarp Pengo na hawa wasaidizi wake wawili. Aliondoka mmoja yaani Kilaini sasa wameletwa wawili kwa mpigo.

Chanzo: RADIO TUMAINI

Kimsingi Pope anaridhia maombi ya askofu mhusika na jimbo kutaka wasaidizi na kisha ombi hilo kupitia kamati maalumu ya baraza la Maaskofu ndipo hupelekwa majina ya kupendekeza, na kwa kawaida majina ya kwanza ndiyo hupita mradi yana sifa stahiki.
 
Interesting. Yaani askofu bado yuko shule. Sasa atafanya uaskofu au itabidi aahirishe hiyo masters degree. Mapadre hawaeleweki, msishangae akaamriwa na mkuu wake kuwa aache shule, maana nasikia huko kwa wakatoliki ukishakuwa padre unasarenda akili na utashi wako wote kwa mkuu wako!

Mapadre wengi wa kikatoliki wanasoma sana wakiwa mapadre, nenda UDSM, Open, Ardhi, SUA na vinginevyo hukosi mapadre kibao wanasoma!
 
Mapadre wengi wa kikatoliki wanasoma sana wakiwa mapadre, nenda UDSM, Open, Ardhi, SUA na vinginevyo hukosi mapadre kibao wanasoma!

Kweli mkuu, kuna mmoja alikuwa mlezi wa sekondari niliposoma, mwaka jana nilimuona Bugando anasoma udaktari! Wakatoliki na elimu dunia, yaani mtu ni askofu na ni mhandisi!
 
wAACHWE WASOME TU KESHO NA KESHO KUTWA UTASIKIA WALE WA KULALAMIKA WAKISEMA WAMESOMESHWA NA SERIKALI OO WANA MAGARI MAZURI ------------ NA SERIKALI WANA SHULE HOSPITALI ZAO WANANUNUA ARTHI WAMEPEWA NA SERIKALI HUKU WENZAO WANAFIKIRI HAYO SI TWASONGA MBELE
 
nakumbuka wakati
tunajadili suala la askofu kilaini kwenda bk hapa jf, wengi walihoji
iweje apelekwe bukoba amako si hata jimbo kuu kwa qualification na
experience aliyonayo? Tukapata majibu kwamba kanisa katoliki aliendeshwi
kisiasa/kidunia zaidi. Wana taratibu zao na kanuni zao kwamba kondoo wa
bwana wanaweza kuchungwa popote pale, na mchungaji hachagui wapi yalipo
malisho!

Hili limejithibitisha kwa kummteua fr. Nzigilwa ambaye ndio kwanza
anaitafuta masters degree! Wangapi wenye elimu zaidi ya hiyo
wameachwa?
ebana ee tumsifu yesu kristu
 
Katoliki hakunaga padri mbumbumbu,wote ni wasomi tu, hongera sana kwa uteuzi huu na mungu awaongoze
 
Kweli mkuu, kuna mmoja alikuwa mlezi wa sekondari niliposoma, mwaka jana nilimuona Bugando anasoma udaktari! Wakatoliki na elimu dunia, yaani mtu ni askofu na ni mhandisi!

Kuna mmoja ameliza Degree yake ya Actecture hapo Ardhi...
 
Nikweli kabisa. Ukisikia padre amepandishwa daraja nakuwa askofu, nikichwa kweli kweli kwani hawabahatishi
 
Back
Top Bottom