Capt Tamar
JF-Expert Member
- Dec 15, 2011
- 11,747
- 14,649
Salaam wakuu,
Katika hali ya kushtusha leo mida ya saa moja nimepita eneo la Kilombero kuelekea barabara ya Fire na kushuhudia kundi la vijana wakiwa na silaha kama visu na mapanga wakiwa wametanda barabarani huku wakiwapora wapita njia na abiria waliokuwa kwenye magari pamoja na kuwajeruhi baadhi.
Leo barabara hiyo ilikuwa na foleni kubwa hivyo vijana hao bila chembe ya woga walivamia vi hiace vya abiria, magari binafsi pamoja na wapita njia, hali niliyoiona inatisha, nilikuwa kwenye kigari cha kazi na nilinusurika.
Tujipange ili hali hii isishamiri na kufikia ile ya wenzetu wa Dar tuliokuwa tunawashambulia kwa kuwaita wanaume wa Dar.
Katika hali ya kushtusha leo mida ya saa moja nimepita eneo la Kilombero kuelekea barabara ya Fire na kushuhudia kundi la vijana wakiwa na silaha kama visu na mapanga wakiwa wametanda barabarani huku wakiwapora wapita njia na abiria waliokuwa kwenye magari pamoja na kuwajeruhi baadhi.
Leo barabara hiyo ilikuwa na foleni kubwa hivyo vijana hao bila chembe ya woga walivamia vi hiace vya abiria, magari binafsi pamoja na wapita njia, hali niliyoiona inatisha, nilikuwa kwenye kigari cha kazi na nilinusurika.
Tujipange ili hali hii isishamiri na kufikia ile ya wenzetu wa Dar tuliokuwa tunawashambulia kwa kuwaita wanaume wa Dar.