The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,424
Hakuna watu ninawaonea huruma kama wateule wa rais hasa mawaziri.
Anayeteua amechanganyikiwa sawa na wale anaowateua.
Simbachawene aliongea anayopaswa akaishia kutemwa.
Kwa utawala huu, hata ukijikomba hauko salama.
Usipojikomba hauko salama. Uktenda haki hauko salama.
Ukisifia, hauko salama.
Ukilaumu, hauko salama.
Ukikosoa, hauko salama.
Ukiunga mkono, hauko salama.
Ukidhulumu, hauko salama.
Ukiongea, hauko salama.
Ukikaa kimya, hauko salama.
Ukiipenda, hauko salama.
Ukiichukia, hauko salama.
Ukiwa chawa, hauko salama.
Ukiwa na udhu kama mwanangu Joseph Warioba, hauko salama.
Ukisema ukweli, hauko salama.
Ukisema uongo, pia hauko salama.
Naona kuna kitu hakiko sawa.