Pamoja na ujio wa Lowassa CHADEMA, Dr. Slaa ni chaguo sahihi kugombea Urais

lowasa anao wafuasi wengi kupita slaa. slaa alishagombea akashindwa, lowasa apate nafasi ya kwanza kwasababu anao uwezo kuhamasisha, pia ana watu wengi sana. mjini jioni ya leo kila mtu moyo umefurahi na wameshamsahau mzee wa kutudanganya kuwa anao uwezo kuhesabu samaki ziwa victoria na barabara kms,...magufuli amefunikwa kupita maelezo. ccm imekufa kifo cha mende.
Neno watu wote unaelewa maudhui yake au ufuata upepo tu, lowassa hajawa mtu wakupelekea watu wote wawe na furaha
 
maskini slaa .......pesa ya rich lowasa.......imekukata.... .but atakatwa tena...........worry not. team magufuli Oyeeeee
 
lowasa amefanya watu wanyongonyeeeeee..........uchu na uroho wa madaraka.........very sad
 
Yaani watu wako hapa JF wanakurupuka tu. Daah!

Wee ni graduate wa Chuo gani mkuu? Hata Katiba ya nchi ya 1977 hufahamu!
 
Yani wewe katika siasa ujui lolote nyamaza tuu na pia kabla ujapost embu rejea na ujiulize unawaandikia wakina nani!!!!!
 
Kama kuna kosa ambalo CHADEMA na UKAWA kwa ujumla wanaweza kufanya ni kumuacha Dr.Slaa katika kinyang'anyiro cha urais na kumpa nafasi NEW COMER Mh.Edward lowasa.

Niseme tu Dr.Slaa bado ni kipenzi kikubwa cha watanzania kutokana na uadilifu wake, ingekuwa busara kama Edward Lowasa angeongeza nguvu kwenye timu ya kampeni ya Dr. hii ni kutokana na umaarufu wake alionao kwenye jamii kwa sasa

Binafsi nakubali Lowasa ni turufu pia kwenye post ya Urais lakini si afya wala busara kumpa nafasi ya kupeperusha bendera ya Urais haswa ukiangalia mazingira ya kisiasa yaliyopo huko alikotoka na sehemu alipoingia.Na ili kuthibitisha hana uchu wa madaraka Lowasa ni bora ashauriwe akubali asiwe mgombea Urais kupitia UKAWA ila kupitia umaarufu wake atoe support kwa ushindi wa Dr.Slaa.

Ikumbukwe kwa muda mrefu Dr.Slaa amekuwa akiaminiwa na wengi kama Rais wa mioyo ya Watanzania na hata yeye psychologically amekuwa akijiandaa kuwaongoza watanzania,sasa leo iweje apokwe nafasi hiyo kirahisi namna hiyo.

Mwisho narudia tena ili ku-maintain legacy ya CDM nashauri Lowasa asiteuliwe kama mgombea urais
Asikiaye na afahamu.
 
I confer you my Ph.D, nimekuwa nikifikiri hivi toka tetesi za Mzee Ngoyai kuhamia CDM/UKAWA. Hili kuweka hesabu vizuri Na kuwapa chenga ya mwili CCM,kwa kuwaaminisha kwamba mzee leigwanani ndiyo mgombea. Unawapiga goli la tobo,Mzee ngoyai anapanga mashambulizi Na kurusha makombora hatari ambayo yatawanyong'onyesha CCM. Hizi hesabu Ni za ushindi.
 
ni kweli kabisa mkuu yaani hapo bila shaka ccm watakuwa washazidiwa.
najua sasa hivi wanajiandaa kwa makombora ya kumvurumishia lowasa wakifaham kuwa yeye ndie anaye enda kupeperusha bendera ya ukawa.
sasa waki mpa nafasi hiyo slaa hakika mipango yao itakuwa imegonga mwamba itabidi waanze kujipanga upya.
na hakika akipitishwa lowasa wao watapata rahisi sana kumvurumishia makombora kwa kuwa wanamfaham vilivyo hapo cha msingi ni slaa ndio apewe hiyo nafasi harafu lowasa aongoze kampeni za ukawa hivyo kuwapa kazi ya ziada ccm maana watakuwa na kazi zaidi ya 3 kukqbiliana na slaa mda huo huo makombora ya lowasa
 
ni kweli kabisa mkuu yaani hapo bila shaka ccm watakuwa washazidiwa.
najua sasa hivi wanajiandaa kwa makombora ya kumvurumishia lowasa wakifaham kuwa yeye ndie anaye enda kupeperusha bendera ya ukawa.
sasa waki mpa nafasi hiyo slaa hakika mipango yao itakuwa imegonga mwamba itabidi waanze kujipanga upya.
na hakika akipitishwa lowasa wao watapata rahisi sana kumvurumishia makombora kwa kuwa wanamfaham vilivyo hapo cha msingi ni slaa ndio apewe hiyo nafasi harafu lowasa aongoze kampeni za ukawa hivyo kuwapa kazi ya ziada ccm maana watakuwa na kazi zaidi ya 3 kukqbiliana na slaa mda huo huo makombora ya lowasa

Kwa mara ya kwanza nimeiona Point katika suala hili linalojadiliwa kishabiki zaidi bila kupima.
 
Mkuu ninakubaliana na wewe 300%. Dr. Slaa agombee uraisi kwa ticket ya UKAWA. UKAWA inauwezo wa kutwaa nchi hata bila nyongeza za sasa. Lakini tunashukuru kwa Watanzania ambao wameanza kujitambua na kuamua kuungana na uKaWA hasa EL.

EL ni hazina nzuri katika kuidhoofisha ccm, lakini siyo rahisi ataweza kupata ushindi akiwa UKAWA.

Ifahamike kwamba, EL anatuhumu za ufisadi ambazo yeye anakatiza zipelekwe mahakamani. Hivi itakuwaje pale atkapo simamishwa na UKaWA, halafu tuhuma za RUSHWA, UFISADI, KUDHUU WATU ambako ccm wameanza kuvikazania, vikafikishwa mahakamani na akawekewa pingamizi? Watanzania tutalia kilio gani kupoteze penalty dakika ya mwisho?

Sisemi kwamba kufikishwa mahakamani kutakuwa kumemchafua ama kumsafisha. Hatima itajulikana baada ya hukumu. Je vipi kuwa na mgombea mwenye tuhuma za jinai mahakamani? Sheria imekaaje?

Lingine, anaweza kusingiziwa kama waliowekeewagwa mapingamizi kwamba si raia wa TZ, na baada ya uchaguzi kesi zikawa withdrawn huku wamepoteza fursa. Vipi ikitokea na kwake akapelekwa kwa makosa sahihi au ya kubambikizwa, ili ije ionekane hana kosa baada ya uchaguzi? Tutakuwa tumefanya nini?

Ikumbukwe Lowasa ameshirikia uharamia mwingi akiwa ccm kama yeye alivyosema kwamba alipitisha azimio la Richmond bila ridhaa yake. Sheria inasemaje ku endorse uharifu, na ukaleta madhara hata kama hukupenda? Kuna mangapi ambayo hayajulikani ambayo pengine alishiriki kwa mtindo huo huo wa Richmond kama anavyodai yeye ambayo wenzake wanayajua?

Vipi wakiamua kumpeleka kwa ushiriki huo, wakampa na wenzake baadaye wakaanza kuwatoa na kumwacha yeye ajitetee? The moment haya mashauri yanaendeshwa, UKAWA itakuwa katika hali gani? Hatutakuw atumepoteza fursa ya pekee kuiondoa ccm madarakani?

Msisahau kwamba ccm ni shetani mwenye hila. Na Lowasa hana record nzuri isipokuwa zilifichwa kwa mtindo wa kulilndana ambao sidhani ccm wataendelea kumlinda wakijua amewasaliti. Watatumia kila kinachowezekana kummaliza huku wakiandaa goli la mkono. Wanaweza wakafanya uhuni wowote kuhakikisha wanatumia makosa aliyoshiriki akiwa ccm ili kuhakikisha hasimami kwenye uraisi, na kama ndiyo UKaWA wamemsimamisha, kutupotezea maono na ndoto zetu za muda mrefu za kuiondoa ccm kwa njia ya UKaWa.

Ninaomba EL ashiriki katika mabadiliko kwa nyadhifa zingine zozote ziwezekanazo lakini nafasi ya Uraisi apewe Dr. Slaa. Hakuna sababu ya kufanya gambling kwa Lowasa mwenye makando kando mengi na ninaimani mengine hatuyajui lakini ccm wanayajua na hivyo wanaweze kuaytumia kujipatia penalty ya mkono, bila goli kipa kwenye uchaguzi. TUTALIA KILIO GANI WATANZANIA?

Nimewasilisha, naomba mfikirie an hata yeye EL afikirie tena. Kuikomboa nchi siyo lazima awe raisi. Mchango wake katika kuliangusha hili dude linalototolesha ufisadi, rushwa na hujuma kwa Watanzania, no matter anashiriki in which way, utakumbukwa vizazi vyote vijavyo. Uraisi hapana.
 
hahaha.....hatutakiiiiiiii......raisi ni lowasaaaaa.......mbona mnahaha ivo jamani, mmelikoroga kulinywa mnalinywa nyie eti
 
Kachukue buku 7 ukale naona una njaa, unataka uanze kuwagawa wanaukawa mapema ili uendelee kushiba, subiri jina tu
 
Kama kuna kosa ambalo CHADEMA na UKAWA kwa ujumla wanaweza kufanya ni kumuacha Dr.Slaa katika kinyang'anyiro cha urais na kumpa nafasi NEW COMER Mh.Edward lowasa.

Niseme tu Dr.Slaa bado ni kipenzi kikubwa cha watanzania kutokana na uadilifu wake, ingekuwa busara kama Edward Lowasa angeongeza nguvu kwenye timu ya kampeni ya Dr. hii ni kutokana na umaarufu wake alionao kwenye jamii kwa sasa

Binafsi nakubali Lowasa ni turufu pia kwenye post ya Urais lakini si afya wala busara kumpa nafasi ya kupeperusha bendera ya Urais haswa ukiangalia mazingira ya kisiasa yaliyopo huko alikotoka na sehemu alipoingia.Na ili kuthibitisha hana uchu wa madaraka Lowasa ni bora ashauriwe akubali asiwe mgombea Urais kupitia UKAWA ila kupitia umaarufu wake atoe support kwa ushindi wa Dr.Slaa.

Ikumbukwe kwa muda mrefu Dr.Slaa amekuwa akiaminiwa na wengi kama Rais wa mioyo ya Watanzania na hata yeye psychologically amekuwa akijiandaa kuwaongoza watanzania,sasa leo iweje apokwe nafasi hiyo kirahisi namna hiyo.

Mwisho narudia tena ili ku-maintain legacy ya CDM nashauri Lowasa asiteuliwe kama mgombea urais
Asikiaye na afahamu.

Ukiona adui anasifia Silaha zako badilisha mbinu.
 
akuna..slaa hakubaliki aisee..Mamvi ndo mpango mzima, wafuasi anao wengi sana..mbowe awe na cheo chake anaweza ongoza vizuri kama m/kiti
 
Back
Top Bottom