Pamba za masikio ni mbaya.

Aksante babaake!
Kwangu wanapenda sana hizi makitu!...Mtu akiziona tu hata kama masikio ni safi ataanza kujichokonoa tu!
 
Kwa kadri ya reporter wangu, kadai hizi pamba za masikio sio nzuri, kwa kadri unavyozidi kutumia, unaousukumiza kiasi flani cha uchafu katika interior part of the ear. Sasa huu uchafu ukigusa part flani ya sikio kwa ndani(kiwambo-not sure) unasababisha maumivu makali ya kichwa, hata unywe pain killer au mseto, mamumivu hayo hayaishi na huwezi hata kulala. kwa ufupi uchafu wa sikio ukizidi, unajikusanya na unatoka wenyewe auto. So the use of earstick is highly restricted!

Habari ndo hiyo.

Mhh uenda pana ukweli hapo! tunaomba wataalamu muchangie zaidi maana waifu anasumbuliwa na masikio yapata mwezi sasa, tushatumia aina kibao za dawa mpaka vitunguu swaumu, mafuta ya jogooo, cjui nini lakini bado yanauma, je tatizo laweza kuwa ni hizi earstick kweli? maana twazinunua sana home, na kama hizo ndo sababu je tutumie nini sasa? kumbuka hizi hutumika kuanzia kwa watoto wachanga kabisa.

Wataalamu fungukeni zaidi katika hili.
 
lol,u dont know what u ar missing,muulize samito akuambie kwa nini anarembua ,macho!
cotton buds ni adui wa masikio yangu kwa kweli, kila wakati nikijaribu huwa najiskia maumivu fulani hivi(sijui ni uoga ?)
 
lol,u dont know what u ar missing,muulize samito akuambie kwa nini anarembua ,macho!

heheheee hapo mamii labda afanye illustrations, mi navojisikiaga ntaanzaje kurembua? niulizie basi we una chuma cha moto atakuogopa
 
cotton buds ni adui wa masikio yangu kwa kweli, kila wakati nikijaribu huwa najiskia maumivu fulani hivi(sijui ni uoga ?)

Bora uachane nazo mkuu kama ushaanza kusikia maumivu bora uchukue hatua fasta...!!
 
Mimi mwenyew kuna mda mackio yalkuwa yanasumbua sana na kujaa wax,nlitumia sana hizo pamba plus boric acid lakn wapi..mpka cku prof wang alipotutolea mfano darasan kuwa "ng'ombe pia wanatoa wax lakin ushawah muona ng'ombe anachonoa maskio yake na pamba?"..tokea hapo nikaachana na pamba.mpka leo mackio yako poa
 
Mhh uenda pana ukweli hapo! tunaomba wataalamu muchangie zaidi maana waifu anasumbuliwa na masikio yapata mwezi sasa, tushatumia aina kibao za dawa mpaka vitunguu swaumu, mafuta ya jogooo, cjui nini lakini bado yanauma, je tatizo laweza kuwa ni hizi earstick kweli? maana twazinunua sana home, na kama hizo ndo sababu je tutumie nini sasa? kumbuka hizi hutumika kuanzia kwa watoto wachanga kabisa.

Wataalamu fungukeni zaidi katika hili.

We endelea tu ku-refresh page wataalam watafunguka sasa hivi. ila hilo kwa waifu wako hapo, u nid to think abt this also. Sijajua bado solution yake.
 
Ni kweli kabisa kuna Daktari aliniambia kuwa utumiaji wa pamba hizo unauziba tundu za kutolea ute wa kulainishia ngoma ya sikio kwa hiyo madhara yake ni makubwa.
 
Hii ni kweli mimi Doctor aliniambia niachekutumia maana nilipata effect yake
uchafu ulisogea mpka ngoma ya sio, likawa linauma c kawaida
 
dawa ya sikio ni mafuta ya mbegu za bangi. watakaobisha, wao ndugu na jamaa zao hawajapatwa na tatizo la sikio, msiwasikilize.
 
mmh! mi huwa nikionaga pamba za maskion, maskio yanaanza kuwasha najikuta nimechukua naanza kuzungusha taratiibu.. kama unavyojua ukijichokonoa lazima ulegeze macho hata uwe nani.. maana kuna raha flan hivi..! sasa kumbe ni its not advisable?!!

Sipati picha!!!!!!!!
 
Aag mkuu hapa umechakachua!!khaaaaa..
Hahaha mkuu sijachakachua ila hii ni habari zinazohusina maana zote zinahusu kuchokonoa sehemu ya uso (nasisitiza ya Uso ) yenye tundu na kitu kinachoweza kukusababishia madhara kama hizo pamba za masikio.

SiZi hujawahi ona mtu akichokonoa pua anavyozubaa yaani wanavyonikera watu wa aina hiyo hasa awe anafanya hivyo kwenye public then akitoa lile kamasi anapangusia kwenye kitu cha karibu yake kama ukuta, mti au hata kwenye nguo aghrrr..... basi nikimtuona mtu wa hivyo napatwa na kinyaa. kama Mnafahamiana ndio kwanza akuone kumbe wewe ulishamuona akiwa ana dig kwenye nose yake akikupa mkono anakusalimia unaukataa kiaina. hahaha.

Ila kwa masikio kwa kweli watu wengi wamezoea kutumia pamba. binafsi pamba naziogopa ila pale inapobidi sichokonoi kuingiza mpaka ndani nasafisha tu mwanzo mwa sikio tena nailowanisha kwanza na maji ili isinikwangue. kweli tuwe na tahadhali kwa vitu vya kisasa sio kila kingaacho ni dhahabu.
 
Sizinga uko sahihi. Mimi si daktari lakini yamemkuta mtu wangu aliyekuwa akipenda sana kuchokonoa maskio kwa hizo cotton buds. Sasa hivi ana hali ngumu, alipokwenda kwa dr alielezwa kama ulivyoeleza kwenye post yako kwamba hakuhitaji kutoa huo uchafu kwani hutoka wenyewe.

Mbaya zaidi, sikio moja ndilo lililokuwa gonjwa lakini sasa limeambukiza lingine. Amejaribu dawa zote za hosp kwa mabingwa Nairobi nk nk lakini wapi. Mwinshowe ameamua kutafuta mafuta ya kenge baada ya kuambiwa ni dawa. TUWE WAANGALIFU NA MASKIO.

Mwenye maelezo juu ya matumizi ya MAFUTA YA KENGE kama dawa ya masikio atujuze tafadhali.

mkuu pamba za masikioni si nzuri hata kidogo. mi kuna siku nilisoma article kwenye gazeti
wakaeleza kuwa sikioni kuna wax ambayo inatengenezwa na kuta za sikio. mtu atumiapo
pamba basi hiyo wax na unyevunyevu hukaushwa kabisa na pamba na kuacha sikio kavu
hivyo kuufanya uchafu kuwa na uwanja mkubwa wa kwenda moja kwa moja mpaka kwa ngoma
ya sikio na kulisababishia matatizo lukuki. wataalamu hawashauri kabisaaa kutumia pamba za
masikioni kuchokonolea sikio. take care
 
njia nzuri ya kutoa uchafu masikioni kwa wapenzi ni kutiana ndimi masikioni
 
Naomba ushauri nifanyeje nimewashwa na masikio kwa muda mrefu sasa(miaka 5) hospitali nilipewa vidonge na eardrops havikusaidia,pamba za masikio ndo kabisa huniongeza tatizo, naomba ushauri wenu yanawasha kavu kavu hayatoi maji.
 
Back
Top Bottom