GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Kutokana na kile ambacho kinachotokea Duniani hivi sasa cha wananchi kuandamana na kutaka viongozi wao waliokaa muda mrefu waondoke madarakani imethibitika viongozi hao kutaka kuondolewa kwao ni kutofuata demokrasia kwenye chaguzi na kutofuata sheria na taratibu za kuendesha nchi.
Kwa hivyo basi, hali ya siasa ya Tanzania ni tofauti sana na nchi hizo kwani chaguzi huru na za haki zinafanyika japokuwa wachache wenye nia na maslahi yao binafsi na wanaotaka ushindi wa mezani hawataki. Utawala bora unaofuata sheria na taratibu za nchi upo japokuwa kuna wachache wanaotaka kutunga na kujiendeshea sheria zao (note: vurugu za Arusha). Kama ni hivyo basi, nguvu ya umma palipo na demokrasia kama Tanzania haina nafasi na wanaofikiria hivyo wanaota ndoto za mchana.
Kwa hivyo basi, hali ya siasa ya Tanzania ni tofauti sana na nchi hizo kwani chaguzi huru na za haki zinafanyika japokuwa wachache wenye nia na maslahi yao binafsi na wanaotaka ushindi wa mezani hawataki. Utawala bora unaofuata sheria na taratibu za nchi upo japokuwa kuna wachache wanaotaka kutunga na kujiendeshea sheria zao (note: vurugu za Arusha). Kama ni hivyo basi, nguvu ya umma palipo na demokrasia kama Tanzania haina nafasi na wanaofikiria hivyo wanaota ndoto za mchana.