Lucha
JF-Expert Member
- Aug 24, 2018
- 20,324
- 62,218
Jeshi la Polisi mkoani Iringa limemfutia kesi ya kujiteka na kutoa taarifa ya uwongo mtandaoni iliyokuwa ikimkabili Padre Jodan Kibiki wa Kanisa Katoliki Parokia ya Nyololo, Jimbo la Mafinga baada ya uchunguzi wa kitabibu kugundua Padre huyo ana changamoto ya afya ya akili.
Akitoa taarifa hiyo Askofu mkuu wa Jimbo la Mafinga, Mhasham Vincent Mwagala, amesema Padre Jodan Kibiki, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Afya Yololo, alitoweka katika mazingira tatanishi Septemba 18, 2025 baada ya kutelekeza gari lake katika msitu wa Sao Hill mkoani Iringa.
Amesema baada ya kufanya malipo ya shilingi milioni tatu na nusu kwenye tovuti ya biashara mtandaoni ya eBay ndipo alipogundua kuwa alikuwa ametapeliwa imebainika ni kweli Padre huyo ana madeni ya Tsh 2,000,000/ million mbili, ambapo kiasi cha Tsh 500,000/= laki tano aliazima kwa Paroko, Tsh 1,500,000/= milioni moja na nusu aliazima kwa muhasibu wa jimbo, na pesa hiyo alienda kuweka kwenye tovuti ya biashara mtandaoni ya eBay, kwenye uchunguzi ilibainika kafanya Transaction ya Tsh 3.5M kwenye mtandao huo, huko ndipo alipo tapeliwa na kupata msongo wa mawazo uliopelekea atoe taarifa kuwa ametekwa.
Taarifa ambayo ilisababisha Jeshi la polisi limkamate kwa kosa ya kutoa taarifa za uongo hivyo kuzua taharuki kwenye jamii.
Akitoa taarifa hiyo Askofu mkuu wa Jimbo la Mafinga, Mhasham Vincent Mwagala, amesema Padre Jodan Kibiki, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Afya Yololo, alitoweka katika mazingira tatanishi Septemba 18, 2025 baada ya kutelekeza gari lake katika msitu wa Sao Hill mkoani Iringa.
Amesema baada ya kufanya malipo ya shilingi milioni tatu na nusu kwenye tovuti ya biashara mtandaoni ya eBay ndipo alipogundua kuwa alikuwa ametapeliwa imebainika ni kweli Padre huyo ana madeni ya Tsh 2,000,000/ million mbili, ambapo kiasi cha Tsh 500,000/= laki tano aliazima kwa Paroko, Tsh 1,500,000/= milioni moja na nusu aliazima kwa muhasibu wa jimbo, na pesa hiyo alienda kuweka kwenye tovuti ya biashara mtandaoni ya eBay, kwenye uchunguzi ilibainika kafanya Transaction ya Tsh 3.5M kwenye mtandao huo, huko ndipo alipo tapeliwa na kupata msongo wa mawazo uliopelekea atoe taarifa kuwa ametekwa.
Taarifa ambayo ilisababisha Jeshi la polisi limkamate kwa kosa ya kutoa taarifa za uongo hivyo kuzua taharuki kwenye jamii.