Orodha ya wasanii waliotoa hit moja kali kisha wakapotea kimyakimya

Orodha ya wasanii waliotoa hit moja kali kisha wakapotea kimyakimya

Mkuu uko vizuri, hii game ya bongo unaonekana unaijua
waliozaliwa kati ya 1980 hadi 1995 walibahatika kushuhudia enzi ya dhahabu ya Bongo Flava, hasa kipindi cha 2000 hadi 2008 ambapo muziki ulikuwa umefika kileleni kwa ubora. Wakati huo muziki haukuwa wa kuburudisha tu, bali pia ulitoa elimu na ujumbe mzito kwa jamii. Kila msanii alikuwa na ladha yake ya kipekee, na maproducer wengi walikuwa wamesomea sound engineering Ulaya, jambo lililofanya kazi zitoke na ubora wa hali ya juu pamoja na ladha halisi ya Kitanzania.

Enzi hizo hakukuwa na smartphones wala internet labda uende internet café, Sehemu kubwa ya burudani ilikuwa ni muziki. Ilipofika jioni watu wanasubiri kwa hamu Top 10, na mida ya saa moja usiku wanamsubiri Sauda Mwilima kupitia Star TV. Pia kulikuwa na Top 10 ya wasanii wachache walioweza kutoa video, zikionyeshwa kupitia ITV 2, ambayo kwa sasa inajulikana kama East Africa TV. mkikutana mtaani, shuleni, n.k. muziki ulichukua nafasi kubwa kwenye mazungumzo.
 
Mkuu inaonekana kipindi ngoma inatoka ulikua na demu wako wa huko upareni (Gonja) ukawa unamuimbia sana 😀😀😀😀
Hata sikuwa na hizo mambo, ila hy ngoma ilinikaa sana kipindi hiko mpaka nikawa naiimba yote 😂
 
waliozaliwa kati ya 1980 hadi 1995 walibahatika kushuhudia enzi ya dhahabu ya Bongo Flava, hasa kipindi cha 2000 hadi 2008 ambapo muziki ulikuwa umefika kileleni kwa ubora. Wakati huo muziki haukuwa wa kuburudisha tu, bali pia ulitoa elimu na ujumbe mzito kwa jamii. Kila msanii alikuwa na ladha yake ya kipekee, na maproducer wengi walikuwa wamesomea sound engineering Ulaya, jambo lililofanya kazi zitoke na ubora wa hali ya juu pamoja na ladha halisi ya Kitanzania.

Enzi hizo hakukuwa na smartphones wala internet labda uende internet café, Sehemu kubwa ya burudani ilikuwa ni muziki. Ilipofika jioni watu wanasubiri kwa hamu Top 10, na mida ya saa moja usiku wanamsubiri Sauda Mwilima kupitia Star TV. Pia kulikuwa na Top 10 ya wasanii wachache walioweza kutoa video, zikionyeshwa kupitia ITV 2, ambayo kwa sasa inajulikana kama East Africa TV. mkikutana mtaani, shuleni, n.k. muziki ulichukua nafasi kubwa kwenye mazungumzo.
Ni kweli mkuu,

Nakumbuka miaka ile, home tulikua tuna record nyimbo kali za wasanii zinazopgwa redioni kwenye kanda,
Kukosekana kwa nternet wakati ule kulifanya radio na television kuwa kimbilio letu kubwa
Bongo fleva ya miaka ile nlikua naipenda sana
 
Mkuu unaweza ukataja ngoma ingine kali ya stopper ambayo tunaweza weka hapa zikakaa kwenye mzani mmoja
Zinaweza zisiwe kwenye mizania sawa coz kwenye Ngoma zake zote stopa hiyo ndio ngoma yake ya kumalizia show, wasanii wengi wako na Ngoma za namna hiyo.
 
Amini, nyota ft peter msechu. Ni wewe. Amini why mimi ft barnaba na linah,
 
K sal ft ferooz Mwana mkiwa

Hii ngoma ilivuma sana miaka ya 2000, baadaye K sal akatoa ngoma ingine aliofanya na Mandojo & Domokaya inayoitwa starehe na fedha ila haikufanya pouwa baada ya hapo kimya hadi leo

Kali P - Imekaa vibaya

Baada ya hii ngoma sijawahi mskia tena huyu jamaa mpaka leo

Kalapina - Mstari wa mbele

Hili dude la Mwana kikosi cha mizinga ni kali sana, na mpaka leo Kalapina hajawahi tena hit nyingine kama hii, ngoma zote zilizofuata ni average

K basil - Ridhiki

Ni moja ya nyimbo pendwa kwa wakati ule, ila jamaa hakufanikiwa kutengeneza Hit song nyingine mpaka leo

John mjema - Wachumba 30

Jamaa alitoa hit song moja, mpaka anafariki hakuweza kutoa ngoma ingine kali

Ziggy D -Eno mike

Hii ngoma ilivuma sana kipindi imetoka naweza kukiri ni moja ya ngoma nnazopenda hadi leo, ila Ziggy dee hakufanikiwa kutoa ngoma ingine kali kama hii

Fresh P ft Juma Nature Tina

Jamaa alitamba sana mwaka 2006 kipindi hii ngoma inatoka baada ya hapo mpaka leo hajaweza kurudi tena

Richie longomba -Funguo

Hii ngoma ilikua kali sana ule mdundo sijui nani aliupiga ila ni moja ya ngoma iliyovuma sana

Ocg ft Juma nature Aqwelina

Hawa jamaa walikua watatu wakitumia herufi za mwanzo za majina yao ndo wakaunda hilo kundi walifanikiwa kutoa hit song moja iliyotengenezwa studio za Bongo record na producer alikua Soggy doggy

Rich one ft Juma nature Hatuna kitu

Huyu jamaa naona mziki anafanya kama fani tuu, alitoea hii ngoma yake moja ambayo mpaka leo hajaweza kurudi na ngoma ingine

Dolo ft Juma jature Razia

Dolo naye ni kama rich one tuu amebebwa sana na crew yake ya TMK ila uwezo wa kawaida, ndo maana baada ya radhia hakuweza kurudi tena

Mazense crew ft Juma nature - Riziki

Hawa jamaa nao walipata ngekewe kupata chorus ya juma nature ngoma ikawa kali sana ila tangu kipindi hiko hawajaweza kurudi tena

Adili -ft Mandojo & Domo kaya - Peke yangu

Huyu jamaa hii ngoma ilimtambulisha vizuri sana lakini kwa bahati mbaya hajawahi kufanya ngoma ingine kubwa kama hii

Sat B - Fagio la chuma

Hii ngoma ilivuma sana miaka ile ya 2000 baada ya hapo jamaa hakurudi tena

Univeral corner - T.shirt & jeans

Hii ngoma ilifanya watu wakaanza kuvaa T.shirt na jeans ilivuma sana ila jamaa hawakuweza kuja na ngoma ingine

Tng squard - Bongo dotcom

Hii pia ilitikisa sana miaka ile inatoka lakini hawa jamaa ni kama walibahatisha tuu

Man ex ft Duly sykes - Nimechezea bahati

Huyu jamaa alifanya hii ngoma kwa beat ile ile ya wimbo wa Bwana misosi nitoke vipi, ngoma yake ikawa kubwa sana ila hakuweza kurudi tena

Picco - Kikongwe

Huyu jamaa hii ngoma ilipendwa sana miaka ya 2002 baada ya hapo jamaa yuko chalii

Stopper ryames - Mtu tatu ndani ya track moja

Jamaa namkubali sana kwa uwezo wake ila hajaweza kutengeneza heat song nyingine kama hii

H mbizo - mpenzi wangu

Huyu jamaa baada ya kutoa hii ngoma akapotea mazima

Pingu na deso ft Mr blue - Jonita

Hawa jamaa walikua ni member wa Tiptop connection chini ya kaka yake Babu tale, the late Abdu bonge, walifanikiwa kutoa heat song moja wakapotea mazima

Dani msimano - siku nzuri
Huyu jamaa alikua ni rafiki wa karibu sana na Mr ebo & wagosi wa kaya, hii ngoma yake ilipendwa sana, ili akashindwa ku maintain akapotea mazima

Pig black - Nini mnataka

Huyu jamaa alipata bahati ya bit kali sana na ngoma yake ilivuma sana baada ya hapo jamaa akapotea

Mack dizo ft Duly sykes Suger mamy

Hii ngoma ilimtambulisha vizuri sana mack dizo ila hakuweza kuendelea kutoa ngoma nyingine kali

Alcom ft mishi - selina

Huyu ustazi ana roho safi sana watu wanaokaa kinondoni B wanaweza kumuelezea vizuri anaishi jirani na Hardman yule aliyetamba na ngoma ya Tamala,
Alcom baada ya selina hajawahi kufanya hit song nyingine

Chelea man - Msela

Huyu jamaa alishawahi kupita pale tiptop connection, alibahatika kutoa hit moja tuu hii ya msela , baada ya hapo alitoa ngoma ingine inaitwa heshim ft Afande sele ila haikufanya pouwa sana baada ya hapo akapotea mazima

Oten -Nicheki

Hii ngoma ya Oten ilivuma sana miaka ile ya 2000, baada ya hapo alitoa ngoma kadhaa zilifanya pouwa lakini hajawahi kutoa heat song kali kuifunika hii ngoma yake ya kwanza iliyo mtambulisha


JI -kidato kimoja

Ngoma ilitoka 2008 na ilifanya pouwa sana ila mwamba baada ya hapo akapotea mazima

Roho saba - Nakupenda hiphop

Huyu jamaa namkubali sana, nafaham ngoma zake nne
•Nakupenda hiphop
•Waite polisi
•stay
•Focus

Ila zote hizi hazikufikia level ya Nakupenda hiphop, nliskia jamaa ni mwanajeshi na ameacha music

Rado- Usiulize

Hii ngoma ilifanywa studio za Baucha kinondoni, ilikua ni dis truck kwa Fid q, ngoma ilisumbua sana, baada ya hapo rado alitoa ngoma zingine lakini mpaka leo hajaweza kutoa ngoma kali tena na ameshapotea

Sajna - Iveta

Hii ngoma ilifanya pouwa sana, akaja na ngoma ingine akimshirikisha Lina, baada ya hapo kapotea mazima

2 berry ft shirko - Wewe tuu

Hawa jamaa walitia hitsong moja baada ya hapo wakagombana kila mmoja akawa anafanya kazi kama solo artist, Berry black aliweza ku maintain kwa kipindi kifupi akaja kupotea , Berry white hakuweza ku maintain kabisa

Offside trick ft AT - Samaki

Hawa jamaa baada ya hii ngoma hawakufanikiwa kutengeneza hit nyingine

Amini - Bado robo saa

Amini licha ya kua THT baada ya robo saa mpaka leo hajatoa hit nyingine

Vumilia - Utanikumbuka

Huyu dada naye alipita THT, na anaonekana alitokea maisha magumu sana, alifanya ngoma kama mbili ila hii ya Utanikumbuka ndo ilimtambulisha kwenye game baada ya hapo, akatoa ngoma ingine inaitwa tatizo ni umaskini haikufanya poa sana, na kuna ngoma alifanya na Ney wa mitego pia haikufanya vizuri, akapotea mazima

Edru g ft barnaba - Scola

Baada ya scola alifanya ngoma zingine lakini hakuna iliyopenya akapotea mazima

Mataluma -Mama mbaya

Huyu jamaa naye alibahatisha ngoma moja na akapotea

Top c ft Ali kiba -Ulofa

Ngoma ilitengenezwa chini ya studio za Bob junior magomeni, ngoma ilipendwa sana hii, ila top c hakuweza kutengeneza hit nyingine safari yake ikaishia hapo

Spince ft Ali kiba - Ayaya

Huyu bwana mdogo naye baada ya ayaya hajaweza kurudi tena

Chibwa ft juru - Nishai

Chibwa anauwezo mkubwa sana nashindwa kuelewa alipatwa na nini baada ya hii nishai sijamskia tena kwenye solo project mpaka leo

Mo music - basi nenda

Jamaa alitubariki ngoma moja ya mapenzi iliyopendwa sana ila hakuweza ku maintain akapotea mazima

Juru- Mbulula

Huyu bwana mdogo wa arusha alituletea hit song moja akachimba mazima

Coyo - Itakucost

Huyu ngosha alikimbiza sana na hii ngoma, akatoa zingine zikawa average baada ya hapo kapotea

Gigy money-Nampa papa

Gigy naye alibahatisha hii ngoma moja na mpaka leo hana ngoma ingine kali kama hii

Lody music - Kubali

Huyu bwana mdogo hii ngoma aliitendea haki sana, baada ya hapo kajitahidi kurudi lakini wapi

Kontawa ft Nay wa mitego- Champion

Baada ya champion,sijawahi kuskia ngoma ingine kali kutoka kwa huyu bwana mdogo, ngoma zote anazotoa ni average, sahv kinachomfanya aendele ku rotate ni content zake anazofanya instagram ila huku kwenye music simuoni kama ana safari ndefu

Dayoo - Mwaka wa kuforce

Baada ya mwaka wa kuforce dayoo hajaweza kutoa hit nyingine mpaka leo japo anapambania nafasi

Kama kuna wengine nimewasahau ongezea kwenye comment
Eleza pia wasanii hao WAKO wapi wanajishighulisha na nini
 
Huyu jamaa na ka sauti kake 😀
Ngoma zake zilzofanya pouwa ni

Nimpende nani na kuna ngoma moja kafanya na Juma nature
Hiyo nimpende nani ndio naijua Mimi😅😅... Kuna dogo nae alikua anatokea mwanza c sir madini nae alikua na Ngoma yake yakuitwa kifungo huru.
 
Yes ni kweli jamaa naye baada ya hii ngoma sijamskia tena
Ma dj na watangazaji wa kibongo wanabana sana.

Hawa ma dj na watangazaji wamekatisha ndoto za wasanii wengi sana.

Unakuta msanii anajichanga anaingia studio anarekodi ngoma kali.

Enzi hizo unakuta msanii anaishi pugu kajiungeni huko, au mbagala ndani ndani.

Labda mwingine katoka mkoani kafika dar kafikia kwa shangazi yake, hawezi hata kuomba nauli ana hela nusu ya kulipia studio tu.

Anaamka saa 10 alfajiri anaanza kutembea kwa mguu mpaka studio.

Studio ni mikocheni kwa master, bamaga kwa majani kinywele, au msasani mawingu studios.

Bongo records ilikua ni bamaga nyumbani kwao na majani

Unaambiwa ukifika Bongo records kwa majani, kwanza heshima iwe mbele kama mfuko wa shati.


Muulize afande sele pamoja na ustaa wake, aliwahi kupigwa makofi, kisa aliwasha bangi, pale studio uwani.

Ukifika unakaa nje ya geti,na sio nje ya geti uegemee ukuta wa studio nooo!!! Ni nje ya geti upande wa pili wa barabara

Akifungua geti, anakua ni kama mwalimu mkuu yupo asembo na nyie wasanii ndio wanafunzi mko upande wa pili wa road.

Akisimama pale nje ya geti anawaona wooote ule upande wa pili.

Ukiingia ndani hela yako unalipia kwa secretary, secretary mwenyewe kajala wa harmo, hacheki na wowote.

Msanii akifanikisha kurekodi process inakua ni hiyo hiyo kufuata ngoma yake studio.

Anaweka ngoma yake kwenye cd anapeleka redio, akifika redio kizungumkuti kinaanzia getini, mlinzi anataka umuungie ya vitumbua.

Ukishindwa kumshawishi vizuri, yawezekana cd yako ikaishia pale pale getini, simply anakwambia maelekezo yametolewa wasanii wakabidhi cd getini, na huwezi kumbishia.

Ukikivuka hicho kizingiti cha mlinzi, unaenda kukutana na secretary wa studio.

Huyu secretary siku hiyo itategemea na mood yake ipoje, unaweza ukampa cd, akaipokea halafu anatupia kwenye dust been na huwezi kumuuliza kitu.

Mtu wa mwisho hapo alikua ni dj au mtangazaji, ilikua ukimpa cd unamshikisha na vichenchi, anaweza akachukua hata namba yako ya simu.

Siku msanii upo zako harakati mara simu inapigwa ni dj, anakwambia leo ngoma yako itachezwa redioni kipindi fulani, kipindi chenyewe ni usiku na kweli unakuta unasifiwa hapo na mtangazaji husika kisha ngoma inagongwa lakini kwa sababu ni usiku mnene unakuta ngoma inasikilizwa na walinzi.

Hapo anakwambia uwe unanitumia vocha, ukituma vocha, ngoma ndio inachezwa, ila ukikausha na wao wanakausha
 
Ni kweli mkuu,

Nakumbuka miaka ile, home tulikua tuna record nyimbo kali za wasanii zinazopgwa redioni kwenye kanda,
Kukosekana na internet wakati ule kulifanya radio na television kuwa kimbilio letu kubwa
Bongo fleva ya miaka ile nlikua naipenda sana
Yes, Na kwangu hadi leo Master J ndio Godfather wa hili game japo yeye hapendagi kabisa hizi debates, anaona zinampotezea muda tu haoni umuhimu wa kuitwa legend wala mambo ya heshima.

Bongo flava hapo zamani ilikuwa inaitwa "Muziki wa kufoka foka" kwasababu wasanii waasisi wa huu muziki wengi walikuwa wanarap, muziki ulionekana wa kihuni tu, mwanzo kabisa miaka ya 1980 mwishoni walikuwaga watoto wa kishua wanarap mistari yao kwa kiingereza ila kwa beats zilezile za wasanii wa Marekani, miaka ya 1990 wachache walijaribu kuimba kwa kiswahili kama kina Saleh Jabir na prodycers enzi hizo walikuwepo kina Bony Luv lakini huyu alikuwa na shughuli zake nyigine kama ku dj na pia alikuwa na shughuli zingine kwenye radio ya couds ilipofunguliwa na kusaga kwasababu walikuwa karibu sana, muziki huu bado ulikuwa hauna future, muziki ulikuwa haurusiwi kupigwa redioni.

Ndipo master J akathubutu kuingia kwenye uandaaji wa muziki kwa miguu yote miwili, baba yake alimtimua nyumbani, hakuweza kumwelewa kwasababu alimsomesha chuo Uingereza kwa pesa nyingi degree ya electronics na alikuwa na uwezo wa kumpachika Tanesco kwasababu alikuwa mkurugenzi ila Master alichagua kuandaa muziki ambao ulikuwa unaonekana wa kihuni, hauna future, wala pesa.

Kipindi anaanza ni yeye peke yake aliekuwa ana studio full time ya kuandaa muziki wa kizazi kipya, alikuwa anarekodi kwa kiasi kikubwa kwa kiswahili wasanii kama kina Sugu lakini pia alirekodi chache kwa kiingereza zilizokuwa hit mfano "Are You Down", iliyoimbwa na kundi la Deplowmatz mwaka 1997.

hapo baadae mziki ukaanza kuonekana angalau umepata direction, miaka ya 1999 hadi 2001 kukaongezeka producers, Tajiri mwenye radio flani alimleta na kumuajiri Mzungu Mikka Mwamba afanye kazi kwenye studio kwa mshahara, wakaja wengine kina P Funk, Enricco, n.k. hawa wote walisomea sound engineering.

Master J kazi aliyokuwa anaifanya mwanzoni sio kidogo, alipiga mzigo wa kufa mtu, kuandaa beats siku 3, kumix na kumaster siku 3, yeye mwenyewe, hapo baadae kidogo ndio akapata wasaidizi kina Ludigo kwenye hiphop, kina said kwenye upande wa nyimbo za gospel na bolingo, n.k. lakini bado aliendelea kutengeneza ngoma kibao tu.

Na hapo baadae miaka ya 2000s akaja kugundua kitu kingine kilichompa mkwanja mrefu kwa kazi ndogo tu, MATANGAZO, alijua kucheza na makampuni, tangazo moja tu lisilozidi hata dakika moja lilikuwa linaweza kumuingizia kipato kikubwa kuliko kuandaa album nzima ya muziki.

Mwaka 2008 aliachana rasmi na production, na kazi yake ya mwisho ilikuwa wimbo wa “Niite Basi” wa Joselin.
 
K sal ft ferooz Mwana mkiwa

Hii ngoma ilivuma sana miaka ya 2000, baadaye K sal akatoa ngoma ingine aliofanya na Mandojo & Domokaya inayoitwa starehe na fedha ila haikufanya pouwa baada ya hapo kimya hadi leo

Kali P - Imekaa vibaya

Baada ya hii ngoma sijawahi mskia tena huyu jamaa mpaka leo

Kalapina - Mstari wa mbele

Hili dude la Mwana kikosi cha mizinga ni kali sana, na mpaka leo Kalapina hajawahi tena hit nyingine kama hii, ngoma zote zilizofuata ni average

K basil - Ridhiki

Ni moja ya nyimbo pendwa kwa wakati ule, ila jamaa hakufanikiwa kutengeneza Hit song nyingine mpaka leo

John mjema - Wachumba 30

Jamaa alitoa hit song moja, mpaka anafariki hakuweza kutoa ngoma ingine kali

Ziggy D -Eno mike

Hii ngoma ilivuma sana kipindi imetoka naweza kukiri ni moja ya ngoma nnazopenda hadi leo, ila Ziggy dee hakufanikiwa kutoa ngoma ingine kali kama hii

Fresh P ft Juma Nature Tina

Jamaa alitamba sana mwaka 2006 kipindi hii ngoma inatoka baada ya hapo mpaka leo hajaweza kurudi tena

Richie longomba -Funguo

Hii ngoma ilikua kali sana ule mdundo sijui nani aliupiga ila ni moja ya ngoma iliyovuma sana

Ocg ft Juma nature Aqwelina

Hawa jamaa walikua watatu wakitumia herufi za mwanzo za majina yao ndo wakaunda hilo kundi walifanikiwa kutoa hit song moja iliyotengenezwa studio za Bongo record na producer alikua Soggy doggy

Rich one ft Juma nature Hatuna kitu

Huyu jamaa naona mziki anafanya kama fani tuu, alitoea hii ngoma yake moja ambayo mpaka leo hajaweza kurudi na ngoma ingine

Dolo ft Juma jature Razia

Dolo naye ni kama rich one tuu amebebwa sana na crew yake ya TMK ila uwezo wa kawaida, ndo maana baada ya radhia hakuweza kurudi tena

Mazense crew ft Juma nature - Riziki

Hawa jamaa nao walipata ngekewe kupata chorus ya juma nature ngoma ikawa kali sana ila tangu kipindi hiko hawajaweza kurudi tena

Adili -ft Mandojo & Domo kaya - Peke yangu

Huyu jamaa hii ngoma ilimtambulisha vizuri sana lakini kwa bahati mbaya hajawahi kufanya ngoma ingine kubwa kama hii

Sat B - Fagio la chuma

Hii ngoma ilivuma sana miaka ile ya 2000 baada ya hapo jamaa hakurudi tena

Univeral corner - T.shirt & jeans

Hii ngoma ilifanya watu wakaanza kuvaa T.shirt na jeans ilivuma sana ila jamaa hawakuweza kuja na ngoma ingine

Tng squard - Bongo dotcom

Hii pia ilitikisa sana miaka ile inatoka lakini hawa jamaa ni kama walibahatisha tuu

Man ex ft Duly sykes - Nimechezea bahati

Huyu jamaa alifanya hii ngoma kwa beat ile ile ya wimbo wa Bwana misosi nitoke vipi, ngoma yake ikawa kubwa sana ila hakuweza kurudi tena

Picco - Kikongwe

Huyu jamaa hii ngoma ilipendwa sana miaka ya 2002 baada ya hapo jamaa yuko chalii

Stopper ryames - Mtu tatu ndani ya track moja

Jamaa namkubali sana kwa uwezo wake ila hajaweza kutengeneza heat song nyingine kama hii

H mbizo - mpenzi wangu

Huyu jamaa baada ya kutoa hii ngoma akapotea mazima

Pingu na deso ft Mr blue - Jonita

Hawa jamaa walikua ni member wa Tiptop connection chini ya kaka yake Babu tale, the late Abdu bonge, walifanikiwa kutoa heat song moja wakapotea mazima

Dani msimano - siku nzuri
Huyu jamaa alikua ni rafiki wa karibu sana na Mr ebo & wagosi wa kaya, hii ngoma yake ilipendwa sana, ili akashindwa ku maintain akapotea mazima

Pig black - Nini mnataka

Huyu jamaa alipata bahati ya bit kali sana na ngoma yake ilivuma sana baada ya hapo jamaa akapotea

Mack dizo ft Duly sykes Suger mamy

Hii ngoma ilimtambulisha vizuri sana mack dizo ila hakuweza kuendelea kutoa ngoma nyingine kali

Alcom ft mishi - selina

Huyu ustazi ana roho safi sana watu wanaokaa kinondoni B wanaweza kumuelezea vizuri anaishi jirani na Hardman yule aliyetamba na ngoma ya Tamala,
Alcom baada ya selina hajawahi kufanya hit song nyingine

Chelea man - Msela

Huyu jamaa alishawahi kupita pale tiptop connection, alibahatika kutoa hit moja tuu hii ya msela , baada ya hapo alitoa ngoma ingine inaitwa heshim ft Afande sele ila haikufanya pouwa sana baada ya hapo akapotea mazima

Oten -Nicheki

Hii ngoma ya Oten ilivuma sana miaka ile ya 2000, baada ya hapo alitoa ngoma kadhaa zilifanya pouwa lakini hajawahi kutoa heat song kali kuifunika hii ngoma yake ya kwanza iliyo mtambulisha


JI -kidato kimoja

Ngoma ilitoka 2008 na ilifanya pouwa sana ila mwamba baada ya hapo akapotea mazima

Roho saba - Nakupenda hiphop

Huyu jamaa namkubali sana, nafaham ngoma zake nne
•Nakupenda hiphop
•Waite polisi
•stay
•Focus

Ila zote hizi hazikufikia level ya Nakupenda hiphop, nliskia jamaa ni mwanajeshi na ameacha music

Rado- Usiulize

Hii ngoma ilifanywa studio za Baucha kinondoni, ilikua ni dis truck kwa Fid q, ngoma ilisumbua sana, baada ya hapo rado alitoa ngoma zingine lakini mpaka leo hajaweza kutoa ngoma kali tena na ameshapotea

Sajna - Iveta

Hii ngoma ilifanya pouwa sana, akaja na ngoma ingine akimshirikisha Lina, baada ya hapo kapotea mazima

2 berry ft shirko - Wewe tuu

Hawa jamaa walitia hitsong moja baada ya hapo wakagombana kila mmoja akawa anafanya kazi kama solo artist, Berry black aliweza ku maintain kwa kipindi kifupi akaja kupotea , Berry white hakuweza ku maintain kabisa

Offside trick ft AT - Samaki

Hawa jamaa baada ya hii ngoma hawakufanikiwa kutengeneza hit nyingine

Amini - Bado robo saa

Amini licha ya kua THT baada ya robo saa mpaka leo hajatoa hit nyingine

Vumilia - Utanikumbuka

Huyu dada naye alipita THT, na anaonekana alitokea maisha magumu sana, alifanya ngoma kama mbili ila hii ya Utanikumbuka ndo ilimtambulisha kwenye game baada ya hapo, akatoa ngoma ingine inaitwa tatizo ni umaskini haikufanya poa sana, na kuna ngoma alifanya na Ney wa mitego pia haikufanya vizuri, akapotea mazima

Edru g ft barnaba - Scola

Baada ya scola alifanya ngoma zingine lakini hakuna iliyopenya akapotea mazima

Mataluma -Mama mbaya

Huyu jamaa naye alibahatisha ngoma moja na akapotea

Top c ft Ali kiba -Ulofa

Ngoma ilitengenezwa chini ya studio za Bob junior magomeni, ngoma ilipendwa sana hii, ila top c hakuweza kutengeneza hit nyingine safari yake ikaishia hapo

Spince ft Ali kiba - Ayaya

Huyu bwana mdogo naye baada ya ayaya hajaweza kurudi tena

Chibwa ft juru - Nishai

Chibwa anauwezo mkubwa sana nashindwa kuelewa alipatwa na nini baada ya hii nishai sijamskia tena kwenye solo project mpaka leo

Mo music - basi nenda

Jamaa alitubariki ngoma moja ya mapenzi iliyopendwa sana ila hakuweza ku maintain akapotea mazima

Juru- Mbulula

Huyu bwana mdogo wa arusha alituletea hit song moja akachimba mazima

Coyo - Itakucost

Huyu ngosha alikimbiza sana na hii ngoma, akatoa zingine zikawa average baada ya hapo kapotea

Gigy money-Nampa papa

Gigy naye alibahatisha hii ngoma moja na mpaka leo hana ngoma ingine kali kama hii

Lody music - Kubali

Huyu bwana mdogo hii ngoma aliitendea haki sana, baada ya hapo kajitahidi kurudi lakini wapi

Kontawa ft Nay wa mitego- Champion

Baada ya champion,sijawahi kuskia ngoma ingine kali kutoka kwa huyu bwana mdogo, ngoma zote anazotoa ni average, sahv kinachomfanya aendele ku rotate ni content zake anazofanya instagram ila huku kwenye music simuoni kama ana safari ndefu

Dayoo - Mwaka wa kuforce

Baada ya mwaka wa kuforce dayoo hajaweza kutoa hit nyingine mpaka leo japo anapambania nafasi

Kama kuna wengine nimewasahau ongezea kwenye comment
Alicom badae alitoa moyo ilisikika kimtindo.

Oten baada ya nicheki alikuja kutoa "mimi" alimpiga sana madogo afande sele humo ndani. Baadae alikuja kutoa "tuyasahau" ambayo alimshirikisha afande sele na suma lee. Ulikua wimbo rasmi wa kumaliza bifu lake na afande sele. Kuanzia hapo ndio akapotea kwenye game

Tng walikua na ngoma nyingine inaitwa "ling on it". Sikumbuki vzr ipi iliwahi kutoka kati ya hiyo na bongo.com lakin zote zilibamba.

Sema mkuu umetisha. Inaonekana umeanza kufatilia bongo fleva kitambo.
 
Back
Top Bottom