Original Comedy wamechacha

Original Comedy wamechacha

jsenyinah

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2012
Posts
249
Reaction score
339
Hawa jamaa enzi wakiwa EATV, wamama wengi sana walikuwa wanaunguza mboga! Ni namna tu walivyokuwa wanakonga roho za watu. Ikifika Alhamis, watu wakawa wanaacha mambo mengine na kujongea karibu na runinga zao. Walikuwa moto moto sanaaa.Enzi hizo walikuwa wanajituma,wanakuwa wabunifu kwa kuwa walikuwa bado hawana magari na nyumba mjini.Walikuwa na adabu.

Baada tu ya hawa jamaa kupata vijisent vya kununua magari na kujenga nyumba mjn,wakaanza kudharau sanaa. Wakawa wanajifanya wajuaji. Huku walipo TBC1 (Ze Comedy) ni kama wamepwaya sana hawa jamaa.Usela mwingi.


Badilikeni nyie Original Comedy, mtakufa njaa mjn.Hamna vipaji vingine, cha kuhubiri Masanja analazimisha tu.Hana mvuto.
 
Nawakubali sana wale jamaa wa mizengwe japo hawavumi kiviiile!
TBC1 yenyewe hakuna anayeipenda, mambo yao yamekuwa ovyo ovyo tu ya kichama!
Hao jamaa kikubwa kilichowaharibia zaidi ni yale magamba ya kijani, zaidi ukiwa star ukitaka kujiharibia hata kama huna nyodo na majigambo ingia mkataba na tbc!
 
Wameshindwa kwa sababu moja kubwa "creativity" wameshindwa kubadilika na wakati,sio lazima uongee accents za makabila fulani ili kufurahisha audience, kujifanya wanawake kunaboa sana acting childish location zao za mjini dar tu zinaonyesha sio wabunifu.
 
Back
Top Bottom