ilboru1995
JF-Expert Member
- Oct 4, 2007
- 2,329
- 268
Inasemekana kuwa wanasayansi ktk nchi zilizoendelea wanaamini kuwa tishio kubwa kuliko lote duniani ni ongezeko la wanaadamu, wanaamini kuwa wanaadamu ndo wanaoharibu mazingira kuliko viumbe wengine, wanaamini maendeleo ya mwanaadamu hususan viwanda ni chanzo cha uchafuzi mkubwa wa mazingira ya dunia. kutokana na ukweli kuwa dunia haiongezeki ila wanadamu wanaongezeka sana ilibidi nchi tajiri duniani kuandaa mpango mkakati wa kuwapunguza binadamu wasiokuwa na mpango! Nchini HAITI UN waliweka vimelea hatari vinavyosababisha mlipuko wa magonjwa ya kipindupindu na kuua maelfu ya watu. Inasemekana UKIMWI hapa Afrika Mashariki ulienezwa na Manowari ya USA iliyokuwa imepiga kambi pale Mombasa, tayari maelfu ya waafrica wamepoteza maisha kutokana na gonjwa hili hatari. Muamar Ghadaffi aliwakamata madaktari wakiwachanja watoto virusi vya UKIMWI! Programu ya kuwapa watoto chanjo hufanywa mashuleni kwa nchi changa kama Tanzania...Inasemekana Majaribio ya magonjwa hatari hufanywa ktk nchi ya Congo DRC, magonjwa kama ebola soon yatapelekwa kwa walengwa kwa lengo la kupunguza wingi na ongezeko la watu duniani... Inasemekana program hii pia inajumuisha kufadhili vikundi vya kigaidi vitakavyo saidia kuwapunguza watu kwa kutumia mabomu kama inavyofanyika kule Iraq, Syria, India, Pakistan, Afghanistan, Bolivia, Peru, Colombia, Africa ... Kama haya yanayosemwa ni kweli na kuwa WHO ni wahusika wakuu, je? nini kifanyike?... karibuni wadau tujadili ...