Operesheni KIMBUNGA yaanza rasmi

Operesheni KIMBUNGA yaanza rasmi

stineriga

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2012
Posts
2,172
Reaction score
892
Na Theonestina Juma, KAGERA

OPERESHENI kimbunga ya kuwarejesha wahamiaji haramu makwao katika Mikoa ya Geita, Kagera na Kigoma imeanza rasmi ambapo ndani ya siku mbili tu, wahamiaji hamu 1851 na ng'ombe 10763 wamekamatwa.

Hayo yamebainishwa jana (leo) na Mkuu Operesheni nchini,Simon Sirro ambaye pia ni Mkuu Msaidizi wa operesheni kmbunga katika mkutano na Waandishi wa habari kuhusiana na operesheni ulioanza rasmi Septemba 6, mwaka huu kufuatia agizo la Rais Jakaya Kikwete alilotoa akiwa ziarani Mkoani Kagera mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu.

DSC09011.JPG

Mkuu wa Mkoa Kagera Kanal Massawe akiwa na Mkuu wa operesheni nchini na Mkuu wa operesheno Kimbunga Kamanda Simon Sirro ambaye pia ni kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Kamanda Sirro amewataka wananchi wote kutoa ushirikiano katika zoezi zima ambalo amesema halina mwisho mpaka hapo watakaporidhika.

Alisema katika mkoa wa Kigoma wamekamatwa wahamiaji haramu 855, short gun moja, gobole moja na ng'ombe 200, Mkoa wa Geita wahamiaji haramu 246 wamepatikana, gobole tatu na ng'ombe 240, sare ya jeshi moja na kibuyu cha maji cha JWTZ moja.

Halikadhalika Mkoa wa Kagera Wahamiaji 750 wamekamatwa, short gun moja, gobole sita, ng'ombe 1,323, ambapo ng'ombe 200 walikamatwa ndani ya pori la akiba la Moyovosi Kigoma na wengine 200 wamekamatwa katika pori la akiba la Burigi mkoani Kagera. Alisema ng'ombe 1,123 wamekamatwa wilaya za Karagwe na Kyerwa na 240 kutoka maeneo mbali mbali mkoani Geita.

Alisema miongoni hao wahamiaji haramu 750 waliokamatwa mkoani Kagera, 26 wamekatwa katika Manispaa ya Bukoba. Kamanda Sirro alisema katika zoezi hilo, wahamiaji hao wanawapakia kwenye malori na kuwapeleka hadi mipakani wa Tanzania nan chi husika na kuwakabidhi kwa viongozi wan chi husika.

"Katika harakati za kutekeleza zoezi hili, suala la haki za binadamu tunazingatia sana, kwani wahamiaji haramu tunawaondoa kwa upole na utaratibu unaotakiwa"alisema

Alisema katika utekelezaji wa zoezi hilo, ametoa onyo kali kwa mtu yeyote ambaye watawarushia risasi maofisa wao, hawatakuwa na mchezo nao, tuko tayari kupambana na yeyote atakayejaribu kuwarushia risasi"

alisema."Huu si wakati wa kuchezeana kwa kurushiwa risasi, kwani muda waliopewa kusalimisha silaha ziliisha kama yeye ni raia mwema muda huu hatakiwi kuwa na silaha yoyote kinyume cha sharia, kama mtu anasilaha heri aitelekeze huko huko porini"alisisitiza. Aidha aliwataka wananchi wenye haki wasihofu lolote waendelee na shughuli zao za maendeleo.

Kwa upande wa Mkuu wa mkoa wa Kagera, Kanali Fabian Massawe amewaka vyombo vinavyoendesha operesheni kuwa makini katika zoezi hilo kwa kuzingatia haki za binadamu.

Alisema wanatakiwa kuhakikisha wahamiaji haramu hao wanaondoka na vitu vyao na wananchi wasikubali kuwahifadhia mali zao.

"Kuna taarifa kuwa kuna baadhi ya wahamiaji haramu, wanawapatia wananchi kuwahifadhia mali zao, tunataka waondoke navyo na kama wana wauzia iwe katika maandishi mtu yeyote atakayebainika kuhifadhi vifaa vya wahamiaji haramu watakamatwa na kushtakiwa kwa kuhujumu nchi"alisema.

Aidha Kanali Massawe alisema katika zoezi hilo halitawakumba wale wahamiaji haramu wa kike waliolewa na Watanzania wanatakiwa kwenda idara ya uhamiaji ili kuweza kupewa hati maalum na baadaye kuhalalishiwa uraia wake.

"Katika utekelezaji wa zoezi hili kuna malalamiko kuwa wanawake ambao ni wahamiaji haramu wanarudishwa,
huku baadhi yao wakiwa na watoto watatu hadi sita, hatuko kwa ajili ya kutenganisha ndoa za watu, wale walioondoka bila kujua sheria wanatakiwa kurudi kama walivyoondoka"alisema.

Alisema lengo la serikali si kwa ajili ya kuachanisha familia za watu na wala hawatamfukuza mtu kwa vile amemwoa mhamiaji hamu katika utekelezaji wa agizo la Rais Kikwete.

Alisema kabla ya kuanza kwa zoezi hili jumla ya wahamiaji haramu 11,061 waliondoka mkoani Kagera, silaha 65 zilisalimishwa SMG zikiwa tatu,Short gun 10 na magobore 52.

Alisema pamoja na idadi hiyo kuondoka kwa hiari mkoa ulitazamia kuondoka kwa wahamiaji haramu 52,000 -53,000 hivyo idadi ya wahamiaji haramu bado ni kubwa.

Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa timu ya operesheni kwa kuwataja wahamiaji haramu
waliko ili sharia iweze kuchukua mkondo wake. Juali 26, mwaka huu Rais Kikwete akiwa wilayani Biharamulo alisema operesheni hiyo ambayo itaendeshwa katika mikoa hiyo itakuwa ni ya aina yake ambayo haijahi kutokea katika nchi hii.

RORYA KWETU: Operesheni Kimbunga yaanza rasmi ya kuwarejesha wahamaji haramu makwao, ni agizo la Rais Kikwete
 
helikopta kutumika na zana zote za kipolisi kusaka wahamiaji haramu popote pale walipojificha, porini , misituni n.k .

sapoti operesheni KIMBUNGA.

Yani hawa Wahamiaji haramu inapaswa warudi woteee.
 
Sirro sio wa kamanda wa mkoa wa mwanza,,huyu jamaa alistaafu na muda fulani alikuwa Tanapa,,kamanda wa mkoa wa Mwanza ni Ernest Mangu
 
Safi sana, warudi kwao banaaaaaaaaaaaa "Watuwache tupumuwe"
Tatizo ni pale oparesheni inapoendeshwa kwa kuangalia sura za watu. Kuna hakimu mkazi huko Kagera kapata kichapo kwa kuwa tu ana sura ya kitusi. Kwa utaratibu huu tutajikuta wahamiaji haramu hasa wenye asili ya kihutu wakiachwa bila kuguswa huku watanzania wenye asili ya kitusi wakiswagwa kwenda mahali wasipopafahamu. Zoezi linaendeshwa mechanically.
 
Sirro sio wa kamanda wa mkoa wa mwanza,,huyu jamaa alistaafu na muda fulani alikuwa Tanapa,,kamanda wa mkoa wa Mwanza ni Ernest Mangu
Sijui Siro yuko wapi, lakini aliyekuwa TANAPA anaitwa Tosi, mhitimu wa darasa la saba aliyepanda vyeo kiajabu hadi kuwa mkuu wa oparesheni polisi.
 
zoezi ilo linaenda kinyume n haki za binadamu sababu wahamiaji wanachapwa bakora,watoto wanafatwa adi mashuleni kutolewa na kubebwa juu juu kwa bakora
 
Safi sana zoezi liendelee kwa nguvu zote lakini pia lazima tutazame mianya ya uhamiaji haramu ili kupunguza au kumaliza tatizo hili.
 
Operesheni kimbunga, hii nimeipenda sana :A S wink:
 
Hao mnaowaita wahamiaji haramu walioolewa na wa Tanzania ndo wanawaleta ndugu zao na kuwapa hifadhi. Hao walioondoka lazima watarudi kwani wamewaacha dada zao. Kama kuna sheria inayoruhusu wahamiaji haramu walioolewa kuendelea kuishi nchini ingeangaliwa upya. Wahamiaji haramu ndo wanatumia mwanya huo kujazana nchini. Wakenya wengi wamewaoa watanzania na kuishi nchini hali kadhalika wanyarwanda na warundi, anatangulia dada anaolewa tz basi kama ana ndugu zake 12 wote lazima watakuja Kuishi Tanzania wakifuata mwenendo ule ule wa dada yao. Yaani kama ni akina dada lazima waolewe na watanzania na sheria imewapa kibali waendelee kuishi nchini bila kufuata utaratibu wa uhamiaji na baadaye wanajimilikisha ardhi hasa kwenye misitu, hifadhi za taifa au maeneo wazi.
 
zoezi ilo linaenda kinyume n haki za binadamu sababu wahamiaji wanachapwa bakora,watoto wanafatwa adi mashuleni kutolewa na kubebwa juu juu kwa bakora

Kama maafisa wa Tanzania wanafanya haya ulosema hawawatendei haki hao watoto.
 
Dah! hao watoto ni wenzetu hao!! inatia huruma sana!
 
Natamani ningekuwa Karagwe! Dini yangu inaruhusu kuwa na wake 6, toto kali 6 za kinyarwana zingekuwa zangu!
 
Tatizo ni pale oparesheni inapoendeshwa kwa kuangalia sura za watu. Kuna hakimu mkazi huko Kagera kapata kichapo kwa kuwa tu ana sura ya kitusi. Kwa utaratibu huu tutajikuta wahamiaji haramu hasa wenye asili ya kihutu wakiachwa bila kuguswa huku watanzania wenye asili ya kitusi wakiswagwa kwenda mahali wasipopafahamu. Zoezi linaendeshwa mechanically.

hawaangalii sura tu mkuu!!kuna mambo mengi sn ya kiinteligensia yanachunguzwa,wanaulizwa maswali na team za watu ambao ni professionals,hivyo hakuna atakae onewa!!!!sura na lafudhi ni moja tu ya items za uchambuzi unaotumika kuwatambua!!!
 
Back
Top Bottom