Open University warejesha foundation program

Masiya

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
7,602
Reaction score
7,341
Chuo Kikuu "Huria" cha Tanzania leo kimetangaza kurejeshwa kwa Foundation Program ambayo awali ilisimamishwa na serikali. Kwa hiyo njia nyingine ya kwenda vyuo vikuu imefunguliwa tena ingawapo dhana ya uhuria wa chuo kikuu hiki imepungua. Nasema imepungua kwani sasa vigezo vya udahili ni
1. Form 6 mwenye point 1.5 kwenye masomo mawili
2. Mwenye Diploma ya GPA 2 hadi 2.9
3. Mwenye Cheti cha NTA level 5/Professional Level II Certificate.
Hivyo mwenye certificate baada ya o-levels inabidi apate Diploma au NTA level 5 sio kama zamani ambapo certificate ilitosha.

Program ni mwaka 1 Gharama ni Tshs 630,000. Wahitimu wa program hii wanaruhusiwa kujiunga na chuo chochote nchini.

Kazi kwenu.
 

Attachments

  • OUT Foundation Course 14.05.2018.jpg
    137.5 KB · Views: 381
Wanasema wame iboresha programu yenyewe ikiwa ni pamoja na kupandisha vigezo vya kujiunga. Nafikiri Prospectus yao ya 2017/18 itakuwa na maelezo zaidi.
 
Hii inamaanisha hata waliosoma college baadaya Kumaliza form four?
 
Jiwe alisema huwezi toka F4 halafu ukaenda Chuo Kikuu. Aliwasambaratisha kwanza wale vijana wa UDOM, na hapa ukiangalia vigezo kwa wale wa F6 ni jumla ya miaka 3 baada ya F4, wa Diploma ni miaka 4 na NTA level 5 ni miaka 3. Hivyo matakwa yake yametimizwa. Tusicho jua je akija mwingine itakuwaje? Kwani raisi na waziri wakisha sema tuliobaki ni kutekeleza tu.
 
Hii inamaanisha hata waliosoma college baadaya Kumaliza form four?
Ukimaliza College baada ya F4 ili uweze kujiunga na Foundation Program unatakiwa uwe na NTA Level5/equivalent au Diploma, cheti cha kawaida nafikiri ni level 4 au equivalent hakikidhi sifa zinazotakiwa.
 
Naomba nieleweshe kidogo, walivyotangaza ni kwamba NTA level 5 anaweza kuendelea chuo kikuu au VP hapo ndio sielewi, na hii NTA level 5 inapatikana ukijiendeleza ukimaliza form 4 sio lazma usome form 5&6
 
Inaelekea OUT waliweka na hiki kigezo cha wenye Certificate ya kawaida, lakini kimekataliwa ndio maana hakipo katika vigezo vya leo.
(iii) ONE year work experience with professional training certificate in a course of duration of not less than 9 months from an Institution approved by the OUT SENATE, after attaining Certificate of Secondary Education Examination with at least 4 passes or 3 credits passes.
 
Naomba nieleweshe kidogo, walivyotangaza ni kwamba NTA level 5 anaweza kuendelea chuo kikuu au VP hapo ndio sielewi, na hii NTA level 5 inapatikana ukijiendeleza ukimaliza form 4 sio lazma usome form 5&6
Ukiwa na NTA level 5 unakigezo cha kudahiliwa Foundation Program ya mwaka 1 ukifaulu ndio unaomba Chuo Kikuu. NTAlevel5 nafikiri inachukua miaka 2 baada ya F4 kwenye hizi College zetu.
 
Ukiwa na NTA level 5 unakigezo cha kudahiliwa Foundation Program ya mwaka 1 ukifaulu ndio unaomba Chuo Kikuu. NTAlevel5 nafikiri inachukua miaka 2 baada ya F4 kwenye hizi College zetu.
Hapo nimekuelewa mkuu
 
Waungwan naomba mnisaidie, mm nna certificate ya form four yenye C moja pamoja na diploma GPA 3.4 kwa sifa hizi naweza kukubalika na kuanza iyo foundation ya OUT
 
Waungwan naomba mnisaidie, mm nna certificate ya form four yenye C moja pamoja na diploma GPA 3.4 kwa sifa hizi naweza kukubalika na kuanza iyo foundation ya OUT
Hapo kwenye C Moja Form 4 dadavua ulipata C moja na zingine ni nini.
Coz unapaswa uwe na walau D 4 au credit 3
 
Zengine ni F Mkuu
Nafikiri ni vizuri kuwasiliana na Open University wenyewe hasa kuhusu ufaulu wako wa F4 na pia GPA ya 3.4 kama ilivyo ingekuruhusu kuomba Chuo moja kwa moja. Sijui hawa mahitaji yao ya ufaulu wa F4 yamekaaje.
 
Baada ya matokeo ya F6 kuwa hewani, issue ya Foundation Program ya Open University imejitokeza tena. Uzi huu una taarifa kamili kwa wale wanaohitaji kujua wanawezaje kufaidika na program hiyo.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…