Ooh Poor NSSF!! - What is this?


Kama anapata taarifa za kifisadi (kama zipo maana so far tunapewa taarifa za tuhuma, majarida ya magazeti, taarifa za vikao) za NSSF kwanini asisubiri na za PPF, PSPF, na LAPF ndipo azungumzie mustakabali mzima wa pension fund sector na uchumi wa Tanzania.

Na taarifa za kifisadi zipo hapa JF kuna wadau wa PPF walianzisha thread sijui imepotelea wapi but ukichungulia yaliyokuwa yakizungumziwa humo ndani na hao whistleblowers ni ya kutisha kushinda hata ya Dau (kama kweli kama mnavyodai ni fisadi). Hatudanganyiki!!!!
 
Duh! Tunajionea mengi hapa. Tofauti ya hekima na upumbavu ni kubwa sana! "Mungu alituumbia vichwa visivyoangaza,ili awazacho mtu kibaki kusitirika, mtu anapoongea amehiari mawazo yake yawe wazi, yote, mazuri au mabovu huwa peupe. Lakini kuna tofauti kati ya kuwa wazi na kuwa uchi" - Mshindo JF
 

What is your point?
 
AAAAhhh....mdondoaji ,we unaweza kudondoa nini ndugu kama mambo mepesi haya yanakusumbua?
Wewe ukiumwa kichwa huendi kumwona daktari,wasubiri kwanza na tumbo na miguu na moyo viume ili ukienda hospitali uweze ku-adress "mustakabali" wa mwili mzima au sio? Nimekuvulia kofia mzee :lol::lol::juggle:
 
Hivi wachangiaji wa huu mfuko (wengi ni waajiriwa katika sekta/makampuni binafsi) wana nafasi yoyote katika kuamua ni kwa namna gani michango yao inatumiwa?

Who will dare to give u a damn chance to do so? Never on this Earth.
 

Sikutegemea mtu ambaye anajiunga JF anaweza kuwa this low! Mwanakijiji ametoa hoja ambazo ziko very particular kwa NSSF na hakuna aliyezijibu hoja hizi na badala yake watu wanakuja na mambo ya ajabu kama haya!
Come on people let us raise above this mediocrity of being so short sighted.
 

Ukienda kwa daktari kwanini huchukua notebook akaanza kukuuliza maswali mbali mbali wakati umeenda kwa shida ya kuumwa na kichwa?? Unaweza kugundua ugonjwa kwa kuangalia sehemu moja ya mwili? Kumbe tunatofautiana ufahamu endeleea na mambo mepesi mepesi ndio yaliyotufikisha hapa Tanzania kutafuta short cut.
 
Wewe waongea na MM aongea,mwenzio aweka wazi hekima zake, wewe waweka uchi mawazo yako ya kipuuzi ya udini. Pengine ungekaa kimya ningeendelea kukuheshimu. "Even a fool, when he keeps silent, is considered wise; When he closes his lips, he is considered prudent" - Proverbs 17:28
What is your point?
 
mh watanzania sisi huu udini utatumaliza jamani.yaani thread ikitoka tunachangia kutokana na itikadi nasio hali halisi hata kama jambo zuri madam si wa itikadi yako kisiasa na kidini basi ni craap.michango inegemea ktk bias.tukiendelea hivi hili jamvi litakuwa halina maana yoyote litabakia kuwa jamvi la wengi wenye msimamo na itikadi fulani ambapo mtataka kusikia mazuri tu ya upande wenu hatimaye hamtajenga kitu bali ni kubomoa.
 
Sasa tumeanza kumtegemea Mwanakijiji too much! hatujifunzi tu walivyotutenda wakina, Mtikila, Mrema, Lipumba na huyu Kijana. Hili zigo letu wote mwenzio akienda huku wewe unaenda huko, tukija kutana ngoma inogile!

mambo mengi yanasemwa, na yataendelea kusemwa... lakini si wote watakaoridhika kwamba lililosemwa limewagusa au kuwaingia vilivyo. Wapo watakaolielewa na wapo watakaoliamini... lakini pia wapo watakaolibeba zimazima kuliko hata mtoa hoja. Mara nyingi napenda majadiliano yaliyo kinyume na ninavyotaka mimi ili niuone upande wa pili... vivyo basi, kama mtu anategemea mtu alete hoja anayotaka na haiji vile ndio maana imewezekana kuona upande tofauti na NSSF ambao ni PPF...Sikatai, yawezekana kabisa mtu kukisema kitu kwa sababu ya chuki moyoni, lakini pia yawezekana ni kutumwa na Uzalendo. pamoja na yote hayo, lazima tuwe tayari kukubali tunapokosolewa bila kujali tunachukizwa ama kufurahishwa. Kwani si mara zote rafiki yako atakuonesha mapungufu yako, watu wenye akili hujifunza kutoka kwa watu wasiowapenda, bali huiga kwa wawapendao.Huo ndio mchango wangu hapo.
 

Kwa taarifa yako sikutaka kulisema hili nadhani hoja za MMwanakijiji zimetawaliwa zaidi na udini kuliko mantiki alipinge hilo kama anaweza.
 
Webmaster mimi nashauri huu mjadala ufutwe. Hatuwezi kujadili wachangiaji wa JF badala ya mambo yanayo endelea Tanzania!!. Hatuwezi kuendelea kuachia mijadala kama hii ya personalities.
 

Hoja za kinafik na kifataani? Sijaona cha maana zaidi ya hayo.
 

'Urs is better'. Ivi we mwanakijiji..lol.. Are you ok? You should get yourself checked out dude. Hint: Delusions of Grandeur.
 

NSSF ndo ina wateja wengi. hata mm binafsi ni mteja wa NSSF so nikianza kulalamika kuhusu hiimifuko ya pension nitalenga lawama zangu kwa NSSF zaidi kuliko hata PPF.

tunaweza kusema Tanzania ni nchi ya kidemekrasi zaidi tukiilinganisha na Misri au libya au Uganda .je tunatakiwa kuridhika????. Au tunatakiwa tujilinganishe na the best na sio kujilinganisha na the worst .

NSSF tutaisema na nyie msiosema mkikimbia kujificha kwenye migngo ya subirini akiondoka huyo boss na nyie mtajiunga. Then tutawashangaaaa Same as akindoka JK then tutawasngaa kama mtaanza............. Pensio yako haibadiliki kwa kuwa Dr yuko ofisini ni ile ile hata angekuwa Miachel,

Great thinker anaongea hoja awe ni Kikwete , mwandosya , mramba au Chenge.........

Mimi binafsi nataka nione NSSF inajenga nyumba japo 20 kila mwaka kila mkoa. Sio miradi isiyo na faida kwa wadau wakuu. NSSF inatakiwa kuwa tofauti na NMB au CRDB. May be Dr dau anaweza kuwa BoT gavernor mzuri.
 

Nimekugongea senksi hapo chini kwa sababu ya hiyo red bana. Ni kweli tunatofautiana ufahamu! Mimi sina uwezo wa "kugundua ugonjwa" kwasababu sio daktari, mie huona symptoms fulani na kumwona daktari. Yeye mwenyewe pia hutumia vipimo,sio ramli,na kugundua ugonjwa na kunitafutia tiba. Siwezi kusubiri mpaka na symptoms nyingine zijitokeze ndo niende hospitali. Sijajaliwa ufahamu wa namna hiyo bana!

The Following User Says Thank You to Mdondoaji For This Useful Post:

Mshindo (Today)​
 
Hivi karibuni kumekuwepo shinikizo la NSSF kwenye mradi wa kufua umeme wa Makaa ya Mawe kule Kiwila Ileje. Tangu lini pension fund wamekuwa na expertise ya kufua umeme.

Inatakuwa na mantiki sana kama NSSF wangesema wana strategic investor mwenye ujuzi na uzoefu wa kuendesha miradi kama hii. Kwa uzoefu wangu mashirika yote ya pension duniani huwa hayawekezi kwenye miradi mikubwa kama lead investor. Wajibu wa pension fund huwa ni kuidentify miradi ambayo return investment yake siyo ya kutilia mashaka. It would have been appropriate kwa NSSF kuwekeza kwa kununua hisa kwenye NmB zilizouzwa kwenye soko la hisa au Unit trust or twiga cement.
 
Kwanza Divides kubwa iwe kwa waliwekeza pesa zao kabla ya watu wengine je hawa jamaa wanafanya hivyo
 
Muulize Mwanakijiji William Erio anafanya nini kule PPF au hakuoni kila nikimuuliza swali hili mwanakijiji anakimbia kulijibu kwasababu anajua ana lake NSSF . Au mwanakijiji tatizo ni Dr RAMADHAN? Pengine hili linakusumbua.

Labda nadhani miaka hii yote hujanielewa vizuri. Ya Mjomba wa Mkapa (Erio) ninayajua kwa kiasi ambacho kitakushangaza. Lakini nitakuwa si mpambanaji mzuri kama nitapigana bila mikakati. Sihitaji hata kidogo kumthibitishia mtu suala la "dini" haliko katika fikra zangu maana nikikubali kuangalia la Dr. Dau kwa mwanga wa udini (kama wewe na wengine mnavyoamini) itabidi mnieleze vipi niliwang'ang'ania:

Robert Mboma
Ben Mkapa
Ed Lowassa
Peter Msolla
Peter Noni
John Magufuli
Gov. Ndulu

Na wengine? Au hawa wote nao ni Waislamu na hivyo niliwang'ang'ania kwa sababu ya dini zao? Kwa mfano nikianza (na linakuja) suala la PPF ina maana niliachilie la NSSF au linafanya hoja dhidi ya NSSF/Kiwira ambazo nimezitoa hazina nguvu? Leo ukisikia naanza kuchambua ufisadi wa PPF utaridhika kwamba "mwanakijjiji kweli haangalii udini"? Unajuaje? Nadhani mna kazi nyinyi ambao mnapomuangalia Dau mnamuangalia kama "muislamu kwanza" halafu mko tayari kutokutaka awajibike yeye mwenyewe na wenzake kwa sababu ni sehemu ya Umma wa Waislamu.

Dhana hii ni ya hatari sana kwa uongozi wa taifa letu. Maana itabidi tujiulize kama wale wanaotaka NSSF ipewe Kiwira nao wanafanya hivyo kwa sababu ya udini hasa kama dini zao zinafanana na ya Dr. Dau, sivyo?
 
'Urs is better'. Ivi we mwanakijiji..lol.. Are you ok? You should get yourself checked out dude. Hint: Delusions of Grandeur.

Kujua uko sahihi haiitaji unyenyekevu wa uongo. My position is better that part I know so I will not cover myself under the pretense of false humility. Are you ok?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…