EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,090
Jana wakati natizama taarifa ya habari ya saa mbili usiku kulipita habari moja ya uzinduzi wa kampeni ya kuondoa unyanyasaji wa kijinsia iliyokuwa inazinduliwa na Mh. Celina Kombani. Sasa mmoja wa watu waliokuwa pale akasema maneno yaliyonifanya nitafakari kidogo,
Akasema "Tangu hizi kampeni za usawa na habari za urithi zimeanza kumekuwa na ongezeko kubwa sana la ndoa kuvunjika tofauti na zamani" Hilo likanifanya nitafakari kidogo, ila kali zaidi likawa kwamba "Tangu hii habari ya urithi imepigiwa chapuo na hao wanaharakati vifo vya kina baba walioko kwenye ndoa, hasa wale wenye uwezo kidogo vimeongezeka maradufu" akataja na makabila ambayo yanaongoza kwa hilo (Nayahifadhi)
Hebu tulijadili kidogo hili, hivi lina ka ukweli?
Akasema "Tangu hizi kampeni za usawa na habari za urithi zimeanza kumekuwa na ongezeko kubwa sana la ndoa kuvunjika tofauti na zamani" Hilo likanifanya nitafakari kidogo, ila kali zaidi likawa kwamba "Tangu hii habari ya urithi imepigiwa chapuo na hao wanaharakati vifo vya kina baba walioko kwenye ndoa, hasa wale wenye uwezo kidogo vimeongezeka maradufu" akataja na makabila ambayo yanaongoza kwa hilo (Nayahifadhi)
Hebu tulijadili kidogo hili, hivi lina ka ukweli?