Mkuu Zitto heshima kwako,
Mimi ni kati ya watu wanaoamini kwenye maono ya mtu hata awe adui yangu vipi, nitasema kweli kuwa mtu huyo atafika mbali sana, lakini pamoja na mtazamo chanya nilionao kwako, wewe umekuwa ukibaldilika badilika na kubadilisha kauli mara kwa mara kiasi kwamba ni ngumu sana kukuamini, unakumbuka jana EATV unasema umevuna wanachama wa CHADEMA 200 Moshi Mjini, Bado Arusha nk?
Unakumbuka ulivyosema mnataka majimbo ya Kawe, Ubungo, na Segerea? Bila kujali nguvu ya Upinzani hasa CHADEMA maeneo hayo? nilitafsiri kuwa pengine una hasira.. lakini ni bora ukatulia kwanza,
Wenzako kwenye chama wala hawaelewi adui yao ni nani..wanajua CHADEMA inangoza nchi, sasa dawa ni kupambana nayo, muulize Mwl. Kaijage or what it is atakwambia "anavyoishughulikia CHADEMA"
Bado wewe bila kujua unahitaji support ya watanzania wakati uanajua wamechoshwa na LiCCM nyie mnakuja na mbadala wa upnzani kuisaidia CCM.
Hujawahi popote narudia popote kuionya CCM kuishambulia CHADEMA na Upinzani kwa ujumla huku wakikusifia wewe, bila kujua kuna siku utapigwa virungu na kuwekwa Lupango ikionekana ni mpinzani kweli?
Mimi nakutakia kila la kheri Mkuu, lakini ujue kuwa siasa ni zaidi ya Mikakati na mbinu za darasani anazowafundisha kitila..Siasa ni watu.. na political wind inawabeba UKAWA... check that out with your team.