Ona alichonifanyia huyu dada

Ona alichonifanyia huyu dada

Uwezo unao,unampenda na bado unadate 4yrs, kakuona boya. Kama gari kashapandishwa sana na si ajabu gari yako imetumiwa kama kwickie coach. Pole, tuma mtu ailete gari ,kawape wazazi na kama hawapo uza buy lingine.
 
Mapenzi bana, usiyachukulie siriasi sana. Mi nishaachana na mambo ya kuweka akili kwenye mapenzi maana hayatabiriki
 
Huyo tayari ana plan b hawezi kuwa jeuri hivyo, teh teh teh shikamoo mapenzi
 
Kama uliweza kutembea Kwa miguu ukampa yeye gari, mwachie kabsa ilo gari tena kwa maandishi akuone gentleman sana!
 
Kachukue ngalangala Lako Kisha umuangukie kwa 'ki-rush' au Kruza2, Ina maana hujajua tu kuwa mwanamke huadhibiwa kwa zawadi pekee?
 
Chukua gari lako wee.. gari lenyewe ndio hilo, wanawwke wapo kibao, utapata mwingine. Halafu usimjaze akilini kiasi ukakosa kufanya yako, take it easy.
 
Wajanja wamekuzidi... Gari yako hio hio imetumiwa kukukata kichwa
 
ucipende kuhonga sna utakuja jinyonga bro kama muongaj unatakiwa ucheze cut&fill mining method (unakula ore na waste) ataisoma number
 
Ukute tangu mwaka uanze hujawahi kumpa mama yako zawadi au hata kumtumia ka 50, leo unahonga gari kwa mtu hata mkataba wa maisha hamna...! Pole sana!!!!!!!

Mkuu hii ndio aina ya wanaume waliopo sasa, nadhani hata Mungu anatushangaa wanaume wa kizazi hiki, yaani tumekua watu wa kulia lia, kulalamika lalamika,kunung'unika sana.

Yaani badala ya wanawake kulia lia na kulalamika imekua kinyume chake, wanaume ndio wamekua hivyo. Kamhonga gari bado mwanamke kammwaga, hii ni ajabu sana na bado jamaa anaendelea kung'ang'ana.
 
lukatony

chukua gari yako tulia . jiweke karibu na marafiki wanaoweza kukufariji na uwaambie kilichotokea kwani hao ndio msaada wako kwa sasa dhidi ya mawazo. hakikisha unakula vizuri ili kuepuka matatizo ya kiafya baadae. ndani ya mwezi mmoja utarudi normal kabisa na ataanza kukutoka akilini. Ila tambua kwamba uwezekano wa yeye kutaka kurudi baadae ni mkubwa sana.

cheers
 
Last edited by a moderator:
Dah... Kumbe kuna watu mapenzi yamewatawala kiasi hiki? Yaani nimuhonge gari mi nitembee kwa miguu, anikosee halafu mi ndo nijishushe!
 
Duh... Kumbe kuna watu mapenzi yamewatawala kiasi hiki? Yaani nimuhonge gari mi nitembee kwa mguu, anikosee halafu mi ndo nijishushe!

Hizi kauli mnapataga nguvu kuziongea humu tu na kwenye vijiwe vyenu na pombe na kahawa, ila mkiwa wenyewe mnagugumia hatari, shikamooo mapenzi
 
HAkupendi.....!!
kama unaweza achana nae na gari chukua immediatelly, life is short to spend it like a slave bro.
 
Back
Top Bottom