Ombi langu kwa NEC, POLISI, TISS, JW na wengine

Sijaona watu wajinga kama washabiki wa chama cha DJ mlevi wa konyagi. Ile ruzuku ambayo walikuwa wanaringia tutaikata kwenye sanduku la kura.
 
Vyombo vyote nilivyovitaja hapo juu heshima kwenu.

Mimi Ni Mtanzania halali,naipenda nchi yangu,na ninafurahi kuwa Mtanzania.

Maombi yangu kwenu:-

NEC
Uchaguzi wa mwaka huu una ushindani mkali Sana,hivyo nawaomba mtende Haki,msikubali kutumika n kasababisha nchi ikaingia kwenye machafuko.
Haki huinua Taifa.
Mkitenda Haki mtakumbukwa na Hakuna atakae wasumbua,Umma wa Watanzania watawalinda na Dunia itawalinda.

POLISI
Wapendwa wakuu wa Polisi Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu Ni mgumu,Mimi Mtanzania mpenda Haki na amani nawaomba safari hii Muwaache CCM na vyama vya Upinzani wapambane wenyewe kwa wenyewe,msiingilie mechi hii,atakae shinda awe ameshinda kihalali,na atakae shindwa awe ameshinda kihalali.
Msiwaonee wapinzani,wakitaka kulinda kura zao wepeni sapoti ili Kama wakilinda halafu wakashindwa wasiwe na la kulalamika.
Pia kama wameshinda wapewe Haki Yao .
Na hiyo ndio mtakua mmeheshimu maamuzi ya Watanzania.
Ushindi wa Haki kwa upande wowote utawaweka huru nyinyi Polisi.
Msikubali kitumiwa na wanasiasa ambao kitaaluma sio wataalamu wa Usalama.
Msikubali nchi yetu ingaingia machafukoni kwa sababu ya mtu mmoja tu.
Ikibidi kutoswa atoswe Tanzania isonge mbele.

Kumbukeni mna wake,waume,watoto,wadogo,wakubwa zenu,shangazi ,Bibi na ndugu zenu ambao sio Askari,mairuhusu wakaishi maisha ya shida kwa sababu ya Vurugu za kuibiwa kura.

Polisi watu wanawapenda Sana na kuwaelewa Sana,nyinyi Ni wenzetu tunapigika wote mitaani.

Tumieni busara Kama mliyotumia siku Lissu aliporudi hamkupiga watu na watu hawakufanya fujo,mlipongezwa sana,mlisifiwa Sana tena na haohao wapinzani.

TISS
Wataalamu salaam,
Ndugu yangu wataalamu wa mambo,Nyinyi Ndio Tegemeo letu sisi Watanzania,nyinyi ndio mnaoweza kushauri na hata ikibidi kulazimaisha.

Nawaomba Sana ndugu zetu nyinyi Mairuhusu nchi mliyoitengeneza kwa amani ikaingia katika machafuko,nawaomba Sana washaurini Wazee wa CCM waweke mazingira ya ushindani wa Uchaguzi Mkuu yawe sawa,ili yeyote atakaeshinda kihalali atangazwe na TUME na yeyoye atakaeshinda kihalali akubali matokeo.
Shaurini au lazimisheni Haki itendeke ili nchi yetu iendelee kupata heshima ndani na nje kuwa na Nchi ya Amani kweli.

Wakuu,mlifanya kazi kubwa sana kuzisaidia na kuziteea nchi zilizokua zikionewa na mabeberu kweli wa wakati huo.
Kwa Nini mshindwe kutetea raia wenzenu?
Kumbukeni maamuzi ya wengi Ni maamuzi ya Mungu.
Wananchi wengi watakae mchagua Mkubaliani huyohuyo kwa sababu huyo ndio Watanzania wamemuamini kwa vyovyote alivyokua kutoka chama chochote.
Tanzania Ni yetu some,waacheni Watanzania wafanye maamuzi na maamizi Yao yaheshimiwe nanyi mtaendelea kupendwa Kama ambavyo Mimi navyowapenda ninyi TISS.


VYOMBO vingine
Tanzania imekua mstari wa mbele kutetea watu wote wanaokandamizwa mahali popote Duniani,toka Sahara Magharibi Hadi Afrika Kusini,toka Palestina hadi Zaire.
Chondechonde Kama dunia nzima inatuhitaji sisi tukawatetee
Kwa Nini sisi tuwakandamize baadhi ya Raia wetu?
Nawaomba Sana Tuifanye Tanzania kuwa mahali salama pa kuishi na kukimbilia na sio kukimbia.
Hapa nawalenga Mahakama,Msajili wa vyama,Vyombo vya habari na wapenda amani wote.

JWTZ
Wapendwa wanajeshi wetu,nyinyi ndio moyo wa nchi,nyinyi mkitetetreka Tanzania itabakia magofu tu,nyinyi ndio kimbilio la wanyonge Afrika nzima na sehemu nyingine Duniani.
Msikubali kuvutwa na Vi wanasiasa uchwara mkaingia
Msikubali kimwanasiasa kimoja tu kikaharibu Taswira nzuri yenu,Msijiingize upande wowote,waacheni wananchi waamue watakavyo,kwa maana maamuzi ya wengi Ni maamuzi ya Mungu.
Heshima yenu huku mtaani Ni kubwa kuliko Taasisi yeyote hapa nchini,mnaaminika na wananchi na mnapendwa bila kifani na vyama vyote.Nyinyi Ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania,sio Jeshi la Chama Cha siasa ama Jeshi la mmtu mmoja.Watanzania wanajivunia nyinyi wanawaamini Nyinyi,wanawakubali nyinyi.Tunawaomba Msiwasikilize wanasiasa wasikilizeni wananchi kwenye Maboksi ya kura.

Hima Himaaaa........

Ewe Mtanzania uliopo kwenye Nafasi Chombo kinachohusiana na Uchaguzi Usikubali kupendelea chama chochote,Wala kudhulumu Haki ya mgombea yeyete kwa sababu utakua umeiepusha Tanzania katika Machafuko na kwa kufanya hivyo utapata baraka na Hakuna mtu au kikundi chochote kitakachokusumbua kwa sababu wakati huo kikundi hicho kitakua kimeahindwa kihalali na hakiongozi dola,ama mtu huyo atakua ameshindwa kihalali na haongozi dola.

Tanzania hoyeeeeeee.......
Umeongea kama mchungaji wa Mungu. Na Mungu akubariki. Sote tunaiependa Tanzania
 
Vyombo vya dola acheni ulingo huru katika uchaguzi huu 2020 watu wakagaragaze watu kwenye mabox si pati picha Mara paap mjuba anashinda chaguzi hakika tz itasimama kila kona watu wata piga kerere za furaha tokea dunia iumbwe hazijawahi sikika
Tiss, polis, jwtz, Nec, mahakama huu ni wakati wa kuonesha uzalendo uliotukuka kwa nchi yetu kwa kutenda haki.
 
Akuna uchaguzi mwepesi uliowaikutokea kama huu wa October 2020.mtaani upinzani haupo kabisa,miaka ya nyuma waliovaa nembo za CCM kuzomewa ilikua ni kawaida kabisa.lakini kwa.sasa wazomeaji ndo wanavaa nembo za CCM.
Wapiga debe ndio mnasema hivyo wakati mwenzenu yuko dodoma anachangisha sadaka kwa ajili ya mskiti kanisani.
 
Sisi Kama wanajeshi hatuna shida na nyie Ila shida itakuja tu pale mtakapoanza kumuletea fyongo fyongo Amri jeshi wetu. Hatutakuwa tayari Mwananchi awaye yeyote yule ajaribu kuchezea sharubu za Kamanda wetu.
Wanajeshi hamfiki hata robo ya majority mtapata tabu sana
 
Sisi Kama wanajeshi hatuna shida na nyie Ila shida itakuja tu pale mtakapoanza kumuletea fyongo fyongo Amri jeshi wetu. Hatutakuwa tayari Mwananchi awaye yeyote yule ajaribu kuchezea sharubu za Kamanda wetu.
We ni kuruta tu, private wa malindo uliyefeli form4!
Amiri jesh mdudu gan? Askari anajua aliapa kulinda katiba na sheria za nchi, hakuapa kulinda mwanasiasa.
Si ajabu hata haujaajiriwa, unakula kwa bakora serviceman ww
 
Mmh

Unafiki TAL anamyonyoa
Anamnyonyoaje wakati TAL kuna matamshi anayatoa anajikaanga mwenyewe.unaanzaje kupinga uwepo wa machinga wakati machinga kwa miaka ya nyuma walikuwa ni ngome ya CDM kwenye majiji makubwa?
 
Back
Top Bottom