Shedafa
JF-Expert Member
- May 21, 2008
- 802
- 173
Mheshimiwa,
Mimi kwa niaba ya watanzania wenzako, ninaomba utufanyie msaada wa kuhamisha lango la kuingilia malori yanayopakia/pakua mizigo ktk kiwanda chako cha Bug/Tazara. Uingiaji na utokaji wa malori kiwandani hapo umekuwa kero kwetu watumiaji wengine wa barabara za Nyerere na Mandela, mfano ni leo majira ya saa 5 asubuhi magari katika barabara hizi yalisimama kwa zaidi ya dak 10 yakisubiri lori lililofunga barabara likisubiri kuingia hapo kiwandani.
Madereva wetu wangekuwa wastaarabu hali isingekuwa mbaya kama ilivyo, kwani hawajui kusubiri. Dereva aliyefunga barabara aliona mwenzie amezuiwa kuingia kwa ajili ya taratibu zao hapo getini lakini yeye akaamua kuliingiza lori lake na kuifunga kabisa barabara mpaka aliyezuiwa aliporuhusiwa.
Kwa hiyo chonde chonde mheshimiwa tunaomba, tunajua ukiamua huwezi kushindwa kupata njia mbadala.
Mimi kwa niaba ya watanzania wenzako, ninaomba utufanyie msaada wa kuhamisha lango la kuingilia malori yanayopakia/pakua mizigo ktk kiwanda chako cha Bug/Tazara. Uingiaji na utokaji wa malori kiwandani hapo umekuwa kero kwetu watumiaji wengine wa barabara za Nyerere na Mandela, mfano ni leo majira ya saa 5 asubuhi magari katika barabara hizi yalisimama kwa zaidi ya dak 10 yakisubiri lori lililofunga barabara likisubiri kuingia hapo kiwandani.
Madereva wetu wangekuwa wastaarabu hali isingekuwa mbaya kama ilivyo, kwani hawajui kusubiri. Dereva aliyefunga barabara aliona mwenzie amezuiwa kuingia kwa ajili ya taratibu zao hapo getini lakini yeye akaamua kuliingiza lori lake na kuifunga kabisa barabara mpaka aliyezuiwa aliporuhusiwa.
Kwa hiyo chonde chonde mheshimiwa tunaomba, tunajua ukiamua huwezi kushindwa kupata njia mbadala.