WanaJF,
UZEMBE NI WA NANI MPAKA PCT IMEKOSA MWAKILISHI BUNGE LA KATIBA?
Ndugu zangu, hili suala limeshatolewa ufafanuzi na Ikulu na Watanzania wakaridhika maana kabla ya ufafanuzi Watanzania walikuwa wame-panic kuwa PCT imeonewa na kudhurumiwa haki yao ya kushiriki kuandaa katiba.
Ufafanuzi ulisema kwamba, baraza la maaskofu alikufuata maelekezo ya sheria katika kuwasilisha mapendekezo yao ya wawakilishi.
Jambo ambalo PCT walikosea ni kujipendekeza kama watu binafsi badala ya kuwa kwenye makundi kama ambavyo sheria ilielekeza. Hivyo serikali haikuwa na budi bali kupiga majina ya PCT kapuni na kupelekea wapentekosti kukosa mwakilishi.
Hivyo hapa mtajionea kuwa kosa lilikuwa la PCT na sio serikali.
KUANDIKWA KWA WARAKA IKULU:
Baada ya maelezo ya serikali kutolewa, baraza la maaskofu liliridhia kuwa wao ndio hawakufuata maelekezo ya sheria hivyo kukiri kuwa walikosea pia walitoa taarifa kwa umma kuwa wameelewana na serikali kuhusu sakata lao.
Lakini ghafla Watanzania tumeshangazwa na Kakobe ambae amejitokeza na kumuandika mhe. Rais ujumbe uliojaa vitisho na mambo mengi ya kusadikika.
Kusema ukweli hili ni jambo la ajabu, sijui Kakobe kakurupuka au vipi, maana kuhusu Pentekosti kukosa mwakilishi tayari Ikulu imelimaliza na aliyefanya kosa la kukosekana kwa mwakilishi wao kwenye bunge ni hao PCT wenyewe.
Sasa Kakobe tatizo lake hapa ni nini!? Nini ambacho hajakielewa katika ufafanuzi wa kurugenzi ya mawasiliano Ikulu kuhusu hili suala!?
Nitoe angalizo kwa Kakobe: kama Kakobe alitaka arudishe umaarufu wake uliotoweka kupitia huu waraka, basi amepotoka big time.
Watanzania sio wajinga kama ambavyo Kakobe anadhani. Kama Kakobe alifanikiwa kudanganya baadhi ya Watanzania na kuweza kujitajirisha, basi asidhani kama ataweza kutudanganya Watanzania wote.
UZEMBE NI WA NANI MPAKA PCT IMEKOSA MWAKILISHI BUNGE LA KATIBA?
Ndugu zangu, hili suala limeshatolewa ufafanuzi na Ikulu na Watanzania wakaridhika maana kabla ya ufafanuzi Watanzania walikuwa wame-panic kuwa PCT imeonewa na kudhurumiwa haki yao ya kushiriki kuandaa katiba.
Ufafanuzi ulisema kwamba, baraza la maaskofu alikufuata maelekezo ya sheria katika kuwasilisha mapendekezo yao ya wawakilishi.
Jambo ambalo PCT walikosea ni kujipendekeza kama watu binafsi badala ya kuwa kwenye makundi kama ambavyo sheria ilielekeza. Hivyo serikali haikuwa na budi bali kupiga majina ya PCT kapuni na kupelekea wapentekosti kukosa mwakilishi.
Hivyo hapa mtajionea kuwa kosa lilikuwa la PCT na sio serikali.
KUANDIKWA KWA WARAKA IKULU:
Baada ya maelezo ya serikali kutolewa, baraza la maaskofu liliridhia kuwa wao ndio hawakufuata maelekezo ya sheria hivyo kukiri kuwa walikosea pia walitoa taarifa kwa umma kuwa wameelewana na serikali kuhusu sakata lao.
Lakini ghafla Watanzania tumeshangazwa na Kakobe ambae amejitokeza na kumuandika mhe. Rais ujumbe uliojaa vitisho na mambo mengi ya kusadikika.
Kusema ukweli hili ni jambo la ajabu, sijui Kakobe kakurupuka au vipi, maana kuhusu Pentekosti kukosa mwakilishi tayari Ikulu imelimaliza na aliyefanya kosa la kukosekana kwa mwakilishi wao kwenye bunge ni hao PCT wenyewe.
Sasa Kakobe tatizo lake hapa ni nini!? Nini ambacho hajakielewa katika ufafanuzi wa kurugenzi ya mawasiliano Ikulu kuhusu hili suala!?
Nitoe angalizo kwa Kakobe: kama Kakobe alitaka arudishe umaarufu wake uliotoweka kupitia huu waraka, basi amepotoka big time.
Watanzania sio wajinga kama ambavyo Kakobe anadhani. Kama Kakobe alifanikiwa kudanganya baadhi ya Watanzania na kuweza kujitajirisha, basi asidhani kama ataweza kutudanganya Watanzania wote.