DUBULIHASA
JF-Expert Member
- Nov 26, 2016
- 3,563
- 5,957
Amani iwe kwenu wazalendo wa nchi hii. Natumaini mungu yupo pamoja nasi katika maisha yetu ya kila siku. Mungu anatupenda sote bila kujali tofauti zozote tulizonazo kwa kuwa sisi sote ni watoto wake na tumeumbwa na yeye.
Ningependa kuwa niwapongeze Watanzania wote kwa kuendelea kulijenga taifa letu kila mtu kwa nafasi yake yaani kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiutamaduni na kadhalika. Kwa mfano wachumi wetu wamekuwa wakituelimisha na kutupa mawazo namna gani ya kujenga uchumi wetu pia wanasheria nao wamekua wakitupa tafsiri za kisheria zinazotusaidia katika maisha yetu, wote mbarikiwe sana. Nami leo nimekuja kutoa mchango wangu mdogo kuhusu lugha mbalimbali zinazotolewa na viongozi wetu.
Tumekua tukishuhudia lugha mbalimbali zisizo na staha zikitolewa na viongozi wetu. Hebu jaribu kutafakari lugha kama wapinzani ni wapumbavu na malofa, watakaoshindwa kumudu nauli wapige mbizi, ninaposimama mimi ni Mungu amesimama, Tuko radhi watanzania wale nyasi kwa vyovyote ndege ya Rais lazima inunuliwe, wapigwe tu nk.
Baada ya kusikia lugha mbalimbali zenye uhaba wa staha nikajikuta narejea nadharia iitwayo SPEECH ACT THEORY. Speech Act ni sayansi ya lugha na falsafa ya lugha ambayo imeelezea dhana kwamba kauli kazi yake ni kutenda. Kwa wataalamu wa lugha yaani watu wa tasnia ya "Linguistics" wanajua ukweli kwamba katika mambo haya ya "Speech Act" siku zote ni kwamba kauli ukiitoa inapelekea tendo litendeke. Kwa hiyo siyo kwamba maneno au kauli zinapotolewa na mtu zinabeba taarifa pekee bali zinabeba matendo ndani yake. Kusema ni kutenda kwa kua maneno huumba kwa hiyo chunga kauli yako. Once you speek, you can't take it back. Neno ukishalitamka halirudi tena mdomoni, hivyo basi mdomo unaweza kukiponza kichwa kama sio mwli kabisa.
Kama ilivyopata kuandikwa na mwanafalsafa wa Oxford J. L Austin ( How To Do Things With Words) na baadaye kuendelezwa na mwanafalsa wa kimarekani J. R. Searle ni kwamba kauli inaweza kuwekwa katika hatua tatu za utendaji au vitendo kama ifuatavyo
(1) Kauli yenyewe inayotolewa na yenye maana mfano nikiingia madarakani watu watalimia meno.
(2) Lengo la kauli hiyo...... hapa inabidi ujiulize swali kwamba huyu aliyeitoa kauli husika alikua na maana gani mfano kutisha watu, kufurahisha, kuelimisha, kuburudisha nk
(3) Matokeo ya kauli yake- kwa mtoaji, mlengwa mfano watu kuogopa, kuteseka, kutajirika nk
Nimejaribu kufanya upembuzi wa kauli zifuatazo kwa muongozo wa wanafalsafa niliowazungumzia kama ifuatavyo
Nataka watu waishi kama mashetani, yaani hii inatia ukakasi kabisa. Katika hali ya kawaida ni kwamba katika jamii zetu yaani nyumbani, shuleni, mitaani na pia katika nyumba za ibada tumefundishwa kwamba shetani ni kiumbe mbaya sana kwa hiyo unabidi tumwogope sana na pia tusimwabudu. Tumefunzwa kwamba shetani ndiye aliyeileta dhambi duniani pia ndiye aliyesababisha kuwepo na kifo duniani, magonjwa, mafuriko, matetemeko, ugaidi, njaa, vita, ukame. Kiongozi huyo alipotamka maneno hayo ni kweli alimaanisha na lengo lake la kuigeuza Tanzania kuwa Jehanamu imewezekana. Nchi ya viwanda haipo ndo hao akina Ndangote wanaondoka, hapa kazi tu haijawezekana hakuna kazi wala ajira zozote mpaka sasa. Elimu hakuna ndo hivyo wanavyuo vikuu wanalia coz mikopo ni majanga.
Watu watalimia meno, hii kauli ni ile inayopatikana katika kitabu cha Luka 13:28 inayosema "Hapo ndipo mtalia na KUSAGA MENO YENU, wakati mtakapomwona Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa mungu, lakini ninyi wenyewe mkiwa mmetupwa nje". Jamani watanzania tuwe wakweli, hivi huyu mtu alimaanisha nini hasa? Kweli alimaanisha tutaumia kweli kweli kwa sababu msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Kwa hili alimaanisha na ndio maana sasa tinasagia meno na kulimia pia na kauli yake imetimia, maneno huumba na aliongea kwa vitendo. Kwa mfano wanyonge tumetupwa nje ya mikopo ya elimu ya juu, hakuna kazi kwa vijana wahitimu wa taaluma mbalimbali, kwa wafanyakazi serikalini hakuna ongezeko la mishahara, kupanda madaraja, uhamisho vilevile kwa wanafunzi hakuna elimu bora ya ukipanga bali ya ukilaza ndio imetawala.
Msinidrive, hii kauli ya msinidrive asili yake ni ubabe na udikteta ndani yake. Kauli hii inamaanisha huyo anayeitoa hataki umjaribu kwa sababu anaweza akakufanya kitu mbaya ukajajutia maisha yako yote. Ukileta ujinga anaweza hata kukupasua au akufanye kitu kinachofanana na hicho. Kwa WABONGO wengi tumezoea mtu akisema "usinidrive" tunaelewa kwamba huyu mtu anamaanisha "usiniendeshe", "usinipelekeshe" "usinitumikishe". Je kweli huyu kiongozi hatukumchangua ili atutumikie? Basi MAJANGA. Je hawa wanavyuo kudai haki yao ya kupatiwa mikopo ni kumpelekesha au kumuendesha huyu kiongozi?. Baada ya tafakuri yangu ya hii kauli kwa muktadha wa Kitanzaniatanzania nikaamua kurejea kamusi yangu ya "Oxford Advanced Learner's Dictionary- New 8th Edition" imetoa maana ya neno "drive" kwa muktadha wa lilivyotumika kwa tafsiri zisizo rasmi
>To make somebody very angry, crazy. Kauli hii ikimaanisha kumfanya mtu awe na hasira na achanganyikiwe. Kwa hiyo watoto wanyonge wa Kimaskini Tanzania kudai haki yao ya kupatiwa mikopo inamfanya mheshimiwa awe na hasira na achanganyikiwe. Hili limetimia mpaka sasa na ndio maana hakuna anayemjaribu na wote tunamwogopa ili tusije ziamsha hasira zake na kuchanganyikiwa pia tusijejuta. Kwa mfano mpaka sasa uhakiki imekua danadana hata aliowapa mamlaka hawana majibu mpaka aseme yeye coz yeye ni one man show na pia one man army. Hata ndugu yangu Lissu pamoja na kuzijua sheria naye amenyuti kimya. Brother Lema alimjaribu kidogo tu mpaka sasa ni historia. Wafanyakazi wananyimwa haki na stahiki zao ila viongozi wa vyama vya wafanyakazi wako kimya wanaogopa kupasuliwa kama jipu. Sio kituo cha haki za binadamu, sijui jukwaa la katiba, wala wanaharati na pia yoyote aliyeweza kujibu shambulizi la NAINYOSHA NCHI KWANZA, SITAKI MAMBO YA VIKATIBAKATIBA MIMI KWENYE UTAWALA WANGU
>To make them do something extreme eg drive somebody crazy/mad/insane ikimaanisha kumfanya mtu afanye kitu kwa kupitiliza mfano awe juha au punguani wa kupitiliza. Sidhani kama wanafunzi wa elimu ya juu walifikia huko. Kwa hili huyu mheshimiwa ameamua kuwa mbogo kwa sababu hataki kushughulikia kero za watu wake hivyo sasa anakereka kuona wanadai haki ili hali yeye anataka waishi kama mashetani kwa wakati huohuo walimie meno. Kweli yeye ni msema kweli na maneno yake yameumba kwa kuwalk the talk na talk the walk. Shikamoo J. L. Austin wewe ni noma sana uliposema HOW TO DO THINGS WITH WORDS.
Namaliza kwa kusema ole wenu watanzania, hawa jamaa wanaposema huwa wanamaanisha kweli kweli kwa kuwa wao wakisema ni mungu amesema na pia ni Mungu kasimama wao walipo. Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
.
Ningependa kuwa niwapongeze Watanzania wote kwa kuendelea kulijenga taifa letu kila mtu kwa nafasi yake yaani kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiutamaduni na kadhalika. Kwa mfano wachumi wetu wamekuwa wakituelimisha na kutupa mawazo namna gani ya kujenga uchumi wetu pia wanasheria nao wamekua wakitupa tafsiri za kisheria zinazotusaidia katika maisha yetu, wote mbarikiwe sana. Nami leo nimekuja kutoa mchango wangu mdogo kuhusu lugha mbalimbali zinazotolewa na viongozi wetu.
Tumekua tukishuhudia lugha mbalimbali zisizo na staha zikitolewa na viongozi wetu. Hebu jaribu kutafakari lugha kama wapinzani ni wapumbavu na malofa, watakaoshindwa kumudu nauli wapige mbizi, ninaposimama mimi ni Mungu amesimama, Tuko radhi watanzania wale nyasi kwa vyovyote ndege ya Rais lazima inunuliwe, wapigwe tu nk.
Baada ya kusikia lugha mbalimbali zenye uhaba wa staha nikajikuta narejea nadharia iitwayo SPEECH ACT THEORY. Speech Act ni sayansi ya lugha na falsafa ya lugha ambayo imeelezea dhana kwamba kauli kazi yake ni kutenda. Kwa wataalamu wa lugha yaani watu wa tasnia ya "Linguistics" wanajua ukweli kwamba katika mambo haya ya "Speech Act" siku zote ni kwamba kauli ukiitoa inapelekea tendo litendeke. Kwa hiyo siyo kwamba maneno au kauli zinapotolewa na mtu zinabeba taarifa pekee bali zinabeba matendo ndani yake. Kusema ni kutenda kwa kua maneno huumba kwa hiyo chunga kauli yako. Once you speek, you can't take it back. Neno ukishalitamka halirudi tena mdomoni, hivyo basi mdomo unaweza kukiponza kichwa kama sio mwli kabisa.
Kama ilivyopata kuandikwa na mwanafalsafa wa Oxford J. L Austin ( How To Do Things With Words) na baadaye kuendelezwa na mwanafalsa wa kimarekani J. R. Searle ni kwamba kauli inaweza kuwekwa katika hatua tatu za utendaji au vitendo kama ifuatavyo
(1) Kauli yenyewe inayotolewa na yenye maana mfano nikiingia madarakani watu watalimia meno.
(2) Lengo la kauli hiyo...... hapa inabidi ujiulize swali kwamba huyu aliyeitoa kauli husika alikua na maana gani mfano kutisha watu, kufurahisha, kuelimisha, kuburudisha nk
(3) Matokeo ya kauli yake- kwa mtoaji, mlengwa mfano watu kuogopa, kuteseka, kutajirika nk
Nimejaribu kufanya upembuzi wa kauli zifuatazo kwa muongozo wa wanafalsafa niliowazungumzia kama ifuatavyo
Nataka watu waishi kama mashetani, yaani hii inatia ukakasi kabisa. Katika hali ya kawaida ni kwamba katika jamii zetu yaani nyumbani, shuleni, mitaani na pia katika nyumba za ibada tumefundishwa kwamba shetani ni kiumbe mbaya sana kwa hiyo unabidi tumwogope sana na pia tusimwabudu. Tumefunzwa kwamba shetani ndiye aliyeileta dhambi duniani pia ndiye aliyesababisha kuwepo na kifo duniani, magonjwa, mafuriko, matetemeko, ugaidi, njaa, vita, ukame. Kiongozi huyo alipotamka maneno hayo ni kweli alimaanisha na lengo lake la kuigeuza Tanzania kuwa Jehanamu imewezekana. Nchi ya viwanda haipo ndo hao akina Ndangote wanaondoka, hapa kazi tu haijawezekana hakuna kazi wala ajira zozote mpaka sasa. Elimu hakuna ndo hivyo wanavyuo vikuu wanalia coz mikopo ni majanga.
Watu watalimia meno, hii kauli ni ile inayopatikana katika kitabu cha Luka 13:28 inayosema "Hapo ndipo mtalia na KUSAGA MENO YENU, wakati mtakapomwona Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa mungu, lakini ninyi wenyewe mkiwa mmetupwa nje". Jamani watanzania tuwe wakweli, hivi huyu mtu alimaanisha nini hasa? Kweli alimaanisha tutaumia kweli kweli kwa sababu msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Kwa hili alimaanisha na ndio maana sasa tinasagia meno na kulimia pia na kauli yake imetimia, maneno huumba na aliongea kwa vitendo. Kwa mfano wanyonge tumetupwa nje ya mikopo ya elimu ya juu, hakuna kazi kwa vijana wahitimu wa taaluma mbalimbali, kwa wafanyakazi serikalini hakuna ongezeko la mishahara, kupanda madaraja, uhamisho vilevile kwa wanafunzi hakuna elimu bora ya ukipanga bali ya ukilaza ndio imetawala.
Msinidrive, hii kauli ya msinidrive asili yake ni ubabe na udikteta ndani yake. Kauli hii inamaanisha huyo anayeitoa hataki umjaribu kwa sababu anaweza akakufanya kitu mbaya ukajajutia maisha yako yote. Ukileta ujinga anaweza hata kukupasua au akufanye kitu kinachofanana na hicho. Kwa WABONGO wengi tumezoea mtu akisema "usinidrive" tunaelewa kwamba huyu mtu anamaanisha "usiniendeshe", "usinipelekeshe" "usinitumikishe". Je kweli huyu kiongozi hatukumchangua ili atutumikie? Basi MAJANGA. Je hawa wanavyuo kudai haki yao ya kupatiwa mikopo ni kumpelekesha au kumuendesha huyu kiongozi?. Baada ya tafakuri yangu ya hii kauli kwa muktadha wa Kitanzaniatanzania nikaamua kurejea kamusi yangu ya "Oxford Advanced Learner's Dictionary- New 8th Edition" imetoa maana ya neno "drive" kwa muktadha wa lilivyotumika kwa tafsiri zisizo rasmi
>To make somebody very angry, crazy. Kauli hii ikimaanisha kumfanya mtu awe na hasira na achanganyikiwe. Kwa hiyo watoto wanyonge wa Kimaskini Tanzania kudai haki yao ya kupatiwa mikopo inamfanya mheshimiwa awe na hasira na achanganyikiwe. Hili limetimia mpaka sasa na ndio maana hakuna anayemjaribu na wote tunamwogopa ili tusije ziamsha hasira zake na kuchanganyikiwa pia tusijejuta. Kwa mfano mpaka sasa uhakiki imekua danadana hata aliowapa mamlaka hawana majibu mpaka aseme yeye coz yeye ni one man show na pia one man army. Hata ndugu yangu Lissu pamoja na kuzijua sheria naye amenyuti kimya. Brother Lema alimjaribu kidogo tu mpaka sasa ni historia. Wafanyakazi wananyimwa haki na stahiki zao ila viongozi wa vyama vya wafanyakazi wako kimya wanaogopa kupasuliwa kama jipu. Sio kituo cha haki za binadamu, sijui jukwaa la katiba, wala wanaharati na pia yoyote aliyeweza kujibu shambulizi la NAINYOSHA NCHI KWANZA, SITAKI MAMBO YA VIKATIBAKATIBA MIMI KWENYE UTAWALA WANGU
>To make them do something extreme eg drive somebody crazy/mad/insane ikimaanisha kumfanya mtu afanye kitu kwa kupitiliza mfano awe juha au punguani wa kupitiliza. Sidhani kama wanafunzi wa elimu ya juu walifikia huko. Kwa hili huyu mheshimiwa ameamua kuwa mbogo kwa sababu hataki kushughulikia kero za watu wake hivyo sasa anakereka kuona wanadai haki ili hali yeye anataka waishi kama mashetani kwa wakati huohuo walimie meno. Kweli yeye ni msema kweli na maneno yake yameumba kwa kuwalk the talk na talk the walk. Shikamoo J. L. Austin wewe ni noma sana uliposema HOW TO DO THINGS WITH WORDS.
Namaliza kwa kusema ole wenu watanzania, hawa jamaa wanaposema huwa wanamaanisha kweli kweli kwa kuwa wao wakisema ni mungu amesema na pia ni Mungu kasimama wao walipo. Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
.