Ole Sendeka amtwanga konde M/kiti UVCCM!

Tatizo la Sendeka ni shule. Wot do u expects from form 4 failure with Div 4.

kinachomsadia ni huo mzuka wake wa kimasai ambao sometimes unapanda sipo...
 
Hapo busara ilikuwa zero kabisa. Karne hii sio ya kupigana.Kama kuna tatizo ni kutumia vikao husika ili kutatua matatizo yaliokuwepo baina ya hawa viongozi. Ngoja tusubiri kama kweli Ole aliyepigwa naye atalifikisha suala lake kwenye vyombo vya sheria
 
Mzee Sendeka kateleza hapa.

Na mafisadi watamkamata kirahisi kwa kumvisha kesi ya jinai. Akiwa convicted na jinai, baadaye wanamuwekea pingamizi wakati wa kugombea ubunge.

Kawekewa ulimbo kanasa mwenyewe, it seems jamaa wanaijua short temper yake ilivyo pamoja na hulka yake ya kutiana mkononi....

Tusubiri tuone.
 
Yees nilikuwa nagojea hili dokezo kama la Nyambala.
Ole Sendeka anapigwa vita na si ajabu the whole thing ni stage managed.
HINT 1:Ole hawaivi na Edo
HINT 2:Edo na "aliyepigwa ngumi" ni maswahiba
Conclusion..mwana JF jazaj mwenyewe!


Hii safi sana.

Kama hauna ubavu, ya nini kuchokoza wenzako?

Ona sasa. Yamemkuta ya Israel vs Hamas!!

teh teh teh teh teh!!
 
Mzee Sendeka kateleza hapa.

Na mafisadi watamkamata kirahisi kwa kumvisha kesi ya jinai. Akiwa convicted na jinai, baadaye wanamuwekea pingamizi wakati wa kugombea ubunge.

Kawekewa ulimbo kanasa mwenyewe, it seems jamaa wanaijua short temper yake ilivyo pamoja na hulka yake ya kutiana mkononi....

Tusubiri tuone.


Well, hii kesi ni nzuri sana. Lakini pia, kama Ole Sendeka alishambuliwa kwanza, inabidi ajihami na kuhakikisha amemmaliza nguvu adui kabla ya kwenda polisi, vinginevyo angeweza "kuuawa".

Sasa kama atakuwa amepeleka kesi polisi, huko mahakamani mashahidi ndiyo watahitajika kutoa maelezo ya kilichotokea.


BTW: Hivi ukiwa mbunge hutakiwi kujihami iwapo utashambuliwa kwa nia ya kuumizwa?
 
Hata Ole Sendeka? Sasa watabaki na nini?

Hii dhana ya watu kumiliki majimbo ni moja ya kansa mbaya sana. Kama taifa tungali tunajifunza siasa za ushindani.Ni utaraibu ambao tunachukua mda mrefu sana kuuzoea.

Kama huwa ana hasira hizo nashangaa mpaka leo hajatwanga mtu bungeni, akiweza kuvumilia upuuzi wa maelezo na majibu ya mawaziri ni kipi kingemshinda?

Ni mmoja wa wabunge waliofanya vyema sana mwaka jana, kwa haiba yake alipaswa kuwa juu ya haya aliofanya. Inasikitisha sana.


Wabunge wote ni mafisadi ....... hakuna hata mmoja aliyepo pale kumtetea mwananchi. Tusijidanganye. Wote wanaokimbilia huko wanafuata pesa tu. Ni wafanyakazi wangapi wa umma wakistaafu wanapata mafao yanayofikia TShs. 30,000,000/= baada ya kulitumikia Taifa kwa zaidi ya miaka 30? Ni mbunge yupi katika historia yao aliwahi kusimama bungeni na kutoa hoja ya kuliangalia hili.

Wabunge wanalipwa kiasi gani baada ya miaka 5? Achilia mbali mishahara na marupurupu ya kila mwezi na kila vikao ... UFISADI MTUPU. Halafu eti tushangae kuona wanayageuza majimbo yao kama ya urithi!!!

Hata hivyo, kateleza kidogo tu, na hiyo haiwezi kumfanya asiwe miongoni mwa "wabunge bora" kwa mwaka 2008 kwa vigezo vilivyopo JF. Au siyo?
 
Yees nilikuwa nagojea hili dokezo kama la Nyambala.
Ole Sendeka anapigwa vita na si ajabu the whole thing ni stage managed.
HINT 1:Ole hawaivi na Edo
HINT 2:Edo na "aliyepigwa ngumi" ni maswahiba
Conclusion..mwana JF jazaj mwenyewe!

Mkuu LG, heshima mbele sana,

- Huu wako ndio tunaita uchambuzi makini kwa siasa zetu za bongo, maana huwa ni only in Tanzania, kwani ukisoma the whole sagga between the lines unaishia tu na huu uchambuzi wako, saafi sana na keep it up!

Kwa sisi wana-JF ni kuamua tunataka kwenda wapi na hii habari, lakini huu uchambuzi wa LG, umetulia sana, ingawa na yeye Sendeka simuelewi sana siku hizi sijui ni frustrations za mafisadi au what?.
 
Mkuu LG, heshima mbele sana,

- Huu wako ndio tunaita uchambuzi makini kwa siasa zetu za bongo, maana huwa ni only in Tanzania, kwani ukisoma the whole sagga between the lines unaishia tu na huu uchambuzi wako, saafi sana na keep it up!

Kwa sisi wana-JF ni kuamua tunataka kwenda wapi na hii habari, lakini huu uchambuzi wa LG, umetulia sana, ingawa na yeye Sendeka simuelewi sana siku hizi sijui ni frustrations za mafisadi au what?.

Mkuu FMES, nashukuru sana.
Jamaa kama Ole waliotoa msimamo thabiti katika valangati la bungeni mnamo February 2008, lililopelekea wazito kadhaa kupoteza nyadhifa wanaandamwa sana na wabaya wao.Lakini tunashukuru jamii inaweza kuona chimbuko la migogoro hii ambayo kimsingi ni watetezi wa umma versus mafisadi.
 
ni muhimu kuangalia mazingira yaliyomfanya mh. mbunge kurusha sumbwi kabla ya kumhukumu.

kama kweli huyo mwenyekiti wa uv-ccm ndio alianza kurusha konde kama anavyodai mh. mbunge basi nadhani "instincts" inakutuma unakwepa kisha unarudisha pigo kisha ndio unaomba samahani. katika hali kama hiyo ningemshangaa mh. mbunge kama angejibu kwa mshale au silaha moto. aidha ningemshangaa kama angeenda nyumbani na baadaye kurudi na kuanza mashambulizi.

hiyo ni reaction ya papo kwa hapo hivyo sioni kosa.

ni mtazamo wangu tuu
 
Tatizo la Sendeka ni shule. Wot do u expects from form 4 failure with Div 4.

kinachomsadia ni huo mzuka wake wa kimasai ambao sometimes unapanda sipo...

Ndugu Masatu,

Unaushaidi wa Elimu ya huyu Mheshimiwa?

Mpaka sasa jamii inaelewa kwamba Ole Sendeka amesoma na kuitimu Kidato Cha Sita kama ifuatavyo( Kulingana na tovuti ya Bunge):


Oldmoshi High School A-Level Education 1985 1987 HIGH SCHOOL
Monduli Secondary School O-Level Education 1981 1984 SECONDARY
Naberera Primary School Primary Education 1974 1980 PRIMARY

Elimu si kigezo cha kuwa kiongozi makini na mwenye hekima mfano ni Rais Mugabe na Degree zake saba lakini badala ya kumpa busara ndio zimemfanya awe mweu hadi kutokowa na imani na kivuli chake.

Ebu tumwangalie John Major, waziri mkuu wa zamani wa Uingereza. Aliweza kuongoza wasomi mahili na waingereza kwa ujumla wa hekima na busara pamoja na kwamba alimaliza kidato cha nne 'unachokiponda'.

Najua ya kwamba elimu ni muhimu katika dunia ya leo lakini kwenda na kuitimu darasani haimaanishi kwamba umefauhulu pia katika matumizi ya hiyo elimu yako. Unaweza kuwa umehitimu chuo kikuu lakini ukawa huna busara na hekima za kiongozi bora.

Naomba kutokukubalina na wewe katika hicho kipimo ulichotumia kumweka Sendeka kwenye mizani.

Shadow.


John Major - Wikipedia, the free encyclopedia

BUNGE::
 
Yaani kweli kuna mtu anaweza kuamini kuwa Ole Sendeka alikuwa anajihami? I don't think so. Basi tu Tanzania yetu ndiyo hivyo tena. Mwenye nguvu ana nguvu kweli kweli. Namshauri huyo dogo a "play it safe" maana si kazi kubwa kwa Sendeka kumsakikisia majambazi wa Mererani wakamtoa roho. Tamaa ya madaraka ni kitu kibaya sana. Any way iko siku ukweli utajulikana. Hakuna cha mafisadi kumwinda Ole Sendeka wala nini. Kinachomuwinda ni tamaa zake mwenyewe, ubabe na woga unaosababishwa na kutokusoma. I do not expect much from such a mediocre except, ofcourse his unbeatable oratory power.
 
Huyu Bwana Ole Sendeka tatizo lake akipandisha mori hashikiki, nakumbuka Old Moshi akiwa Head Prefect akibishiwa tu mori juu, ana hasira za haraka haraka sana...ukim-challenge tu tayari povu linamtoka, ila at the end of the day form 6 ilimtoa povu...
 
Mkutano wa Lowassa wazua balaa Monduli

2009-01-10 12:13:37
Na Mwandishi Wetu


Mkutano wa viongozi wa jadi wa kabila la Kimasai ulioitishwa na kiongozi wake aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, umezua balaa, baada ya mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Mkoa wa Arusha, James Milya, kurushiana makonde mazito hadharani.

Tukio hilo lilitokea jana baada ya mkutano huo wa viongozi wa jadi wa Kimasai kuahirishwa kwa muda kwa ajili ya chakula cha mchana.

Mkutano huo uliokuwa wa siku mbili ulimalizika jana, lakini kwa mujibu wa Ole Sendeka, Lowassa hakuwepo wakati tukio la purukushani hiyo lilipotokea.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Ole Sendeka alisema aliamua kujitetea baada ya Milya kumrushia konde ambalo alilikwepa.

Alisema kutokana na hali hiyo, aliamua kujitetea kwa kumrushia konde moja ambalo lilimpata hadi kuanguka chini.

Akizungumzia zaidi juu ya mkutano huo, Ole Sendeka alisema kwa ujumla haukuwa wa kisiasa na haukupangwa kwa lengo la kumhujumu.

Alisema wakati akichangia mada, katika mkutano huo uliokuwa na ajenda mbili, ya kuzungumzia elimu ya mtoto wa kike kwa jamii ya wafugaji na nyingine ya matatizo ya ardhi, baadaye Milya alichangia hoja hiyo akiwashutumu wanasiasa na hasa katika jimbo la Simanjiro kwamba ni mafisadi na wanafiki.

``Huyu bwana mdogo alinishambulia akidai kuwa sisi wanasiasa na hasa wa Simanjiro ni wanafiki na kwa nini hatuchukuliwi hatua.

Alitamka wazi ingawa hakutaja jina langu, lakini alisema `kama mchangiaji huyo aliyemaliza kuzungumza sasa hivi` akimaanisha jina lake (Sendeka),`` alisema.

Alisema baada ya kuahirishwa kwa muda kwa ajili ya kupata chakula, alimuuliza Milya kwa nini alimshambulia kiasi hicho naye akamjibu kwamba sasa ameanza vita.

Alisema bila kutegemea alirushiwa ngumi, ambayo hata hivyo, alifanikiwa kuikwepa.

``Katika kujitetea niliamua kumrushia ngumi moja ambayo ilimpata na akaanguka chini, nilichofanya ni kujitetea tu katika mazingira kama yale...`` alisema.

Lakini kwa upande wake Milya alisema hakumrushia ngumi, isipokuwa Ole Sendeka ndiye aliyempiga hadi akaanguka chini.

Alisema baada ya kuanguka Ole Sendeka alitaka kuendelea kumpiga, lakini wajumbe wa mkutano huo walimnusuru.

Hata hivyo alisema aliripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha Monduli na kufungua jalada namba Monduli/RB/35/09.


SOURCE: Nipashe
 
Sendeka ataka CCM imwadhibu ‘mbaya wake’
John Mhala, Arusha
Daily News; Sunday,January 11, 2009 @21:15

Mbunge wa Simanjiro mkoani Manyara, Christopher Ole Sendeka amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, kumwonya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ya mkoa huo, James Ole Millya.

Sendeka alisema hayo jana wakati wa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mtafaruku wa kutwangana ngumi uliotokea wilayani Monduli muda mfupi baada ya mapumziko ya semina ya wazee wa jadi wa Kimasai waliokuwa wakijadili mada za ardhi na kumwendeleza mtoto wa kike wa kifugaji kielimu.

Mbunge huyo alidai kitendo cha mwenyekiti huyo kuandamana kwa magari, pikipiki, baiskeli na miguu hadi Simanjiro kuwashukuru wajumbe waliomchagua na kutoa shukrani kanisani, hakiingii akili kwa mtu yeyote yule.

Alisema Millya ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha na inashangaza na kusikitisha kuona anakwenda Simanjiro kwa ‘mbwembwe’ kubwa na msafara mzito kwa lengo la kuwashukuru wajumbe na kutoa sadaka kanisani.

“Huyu ni Mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Arusha, alipaswa kufanya maandamano yake mkoani Arusha… hata yangekuwa mabasi na malori, lakini kwenda na maandamano jimboni Simanjiro ni ishara tosha kuwa Mwenyekiti huyo ana lake jambo ambalo chama Mkoa wa Arusha kinapaswa kumwonya, vinginevyo anaweza kuleta balaa kwa wapiga kura,’’ alidai Ole Sendeka.

Alisema hakuna mwenye hati miliki ya ubunge katika jimbo lolote nchini, lakini kwa hili linalofanywa na Millya ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ndani ya chama na inaelekea anajiandaa kuwania ubunge katika jimbo hilo.

Akizungumzia ugomvi wao na Millya uliofikia hatua ya kutwangana makonde, Ole Sendeka alisema ugomvi huo aliuanza yeye kwa maneno na vitendo hatua iliyofikia kujibu mashambulizi ya hali ya juu ikiwa ni njia pekee ya kujitetea.

“Mimi niko tayari kusuluhishwa na mtu yeyote awe wa kidini ama kiongozi wa chama, lakini kwanza lazima kijana huyo aelezwe kuwa anachokifanya anakijua na wanaomtumia kwa hilo anawajua kwa undani zaidi,’’ alisema Sendeka.

Naye Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mohamed Mbonde alipoulizwa juu ya Mwenyekiti huyo kwenda kwa maandamano wilayani Simanjiro, alisema hana taarifa hizo na kama suala hilo lipo, ni la binafsi, halihusiani na chama wala jumuiya yenyewe.
 
Ole Sendeka kuburuzwa kizimbani keshokutwa
Mussa Juma Simanjiro

MBUNGE wa Simanjiro kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Christopher Ole Sendeka, keshokutwa anatarajiwa kuburuzwa mahakamani.

Mbunge machachari, anatuhumiwa kumpiga na kutishia kumua Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wa Mkoa wa Arusha, James Ole Millya.

Akizungumza na Mwananchi jana jijini Arusha, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Basilio Matei, alisema vijana wake wanaendelea na upelelezi kuhusu tuhuma hizo kabla ya kumfikisha mahakamani Ole Sendeka.

"Maofisa wangu wanaendelea na upelelezi wa kesi hiyo na ninatarajia kwamba watakamilisha kazi yao, ili Januari 14 tumpeleke (Ole Sendeka) mahakamani,"alisema Matei.

Kamanda huyo alisema "Ole Sendeka anatuhumiwa kumpiga na kutishia kumuua mlalamikaji kwa kutumia bastola, ambayo imepatika baada ya mtuhumiwa kuidondosha wakati wa tukio".

Wakati huo huo, Ole Millya alipokelewa kwa shangwe katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, wakati wa ibaada ya shukrani ya kuombewa baada ya kushinda nafasi hiyo.

Ibada hiyo ilifanyika katika Kanisa la Usharika wa Olkesment na iliongozwa na Mchungaji Emanuel Kweka na kufuatiwa na sherehe kubwa ambayo watu wengi waliihusisha na uzinduzi wa kampeni ya Ubunge wa Simanjiro.

Sherehe hiyo iliyofanyika nyumbani kwa mwenyekiti huyo, ilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo baadhi ya wanachama wa CCM na waumini wa kanisa hilo.

Wafuasi wa Ole Millya waliimba nyimbo mbalimbali za kumpongeza na kumtaja kama Mbunge Mtarajiwa.

Hata hivyo baadhi ya wafuasi wa Ole Sendeka walisusia ibaada hiyo ya shukrani kwa madai kuwa hizo ni kampeni za ubunge.

Vurugu za viongozi hao, zilitokea juzi katika semina ya viongozi wa mila iliyokuwa inafanyika katika Chuo cha Ualimu Monduli, na Ole Sendeka alikuwa miongoni mwa waalikwa.

Semina hiyo ambayo ilikuwa imeandaliwa na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na kuwashirikisha viongozi wa jadi wa Kimasai. Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chilligati

Habari za uhakika toka kwa viongozi wa CCM, zimeeleza kuwa vurugu hizo huenda zikajadiliwa katika vikao vya maadili vya chama hicho hivi karibuni.

Wakati huo huo mwandishi Hemed Kivuyo, anaripoti kutoka Simanjiro kuwa Ole Sendeka ameiomba CCM mkoani Arusha imuonye Ole Millya.

Sendeka alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mgogoro uliotokea wilayani Monduli muda mfupi baada ya mapumziko ya semina ya wazee wa jadi wa kimasai (Olaigwanani), waliokuwa wakijadili mada za ardhi na nafasi ya mtoto wa kike wa jamii ya wafugaji katika elimu.

Alisema kitendo cha Ole Millya kuandamana kwa magari, pikipiki, baiskeli na miguu kwenda Simanjiro kuwashukuru wajumbe aliomchagua na kutoa shukurani kanisani si cha kuungwa mkono.

Alisema pia inashangaza na kusikitisha kuona mwenyekiti wa UVCCM mkoani Arusha anakwenda Simanjiro kwa 'mbwembwe' kubwa na msafara mzito kwa lengo la kuwashukuru wajumbe na kutoa sadaka kanisani.

"Huyu ni Mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Arusha alipaswa kufanya maandamano yake mkoani Arusha hata yangekuwa kwa mabasi na malori, lakini jimboni Simanjiro kwa maandamano ni ishara ya kutosha kuwa ana lake jambo na chama Mkoa wa Arusha, kinapaswa kumwonya vinginevyo anaweza kuleta balaa kwa wapiga kura," alisema.

Ole Sendeka alisema ingawa hakuna mwenye hati miliki ya ubunge katika jimbo lolote hapa nchini, lakini kwa yanayofanywa na Ole Millya ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ndani ya chama na inaelekea anajiandaa kuwania ubunge katika jimbo hilo.

Akizungumzia ogomvi wao na Ole Millya uliofikia hatua ya kutwangana makonde, Mbunge huyo wa Simanjiro alidai kuwa aliuanza Millya kwa maneno na vitendo na kwamba yeye alichokifanya ni kujibu mashambulizi ya hali ya juu ikiwa ni njia pekee ya kujitetea.

Alisema semina ilikuwa ikizungumzia uporwaji wa ardhi na kumwendeleza kielimu mtoto wa kike wa kimasai, lakini yeye alifika hatua ya kumshambulia na kumkashifu wazi wazi hatua iliyomfanya hata mwenyekiti wa kikao hicho Vicenti Parseko Ole Kone Mkuu wa Mkoa wa Singida, kumkatiza kwa kumweleza juu ya kutoka nje ya mada zilizopo, lakini akikaidi hilo.

Alisema ulipofika wakati wa mapumziko alimwendea na kumuuliza lakini alijibiwa kashfa na kurushiwa "konde", jambo lililomsukuma kujibu mapigo.

"Mimi niko tayari kusuluhishwa na mtu yeyote awe wa kidini ama kiongozi wa chama, lakini kwanza lazima kijana huyo aelezwe kuwa anachokifanya nakijua na wanaomtumia kwa hilo nawajua kwa undani zaidi," alisema Sendeka.

Katibu wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Mohamed Mbonde, kuhusu madai kwamba Ole Millya ameanda Simanjiro kwa maandamano alisema hana taarifa hizo na kwamba hilo halihusiani na chama.
Source: Mwananchi Read News
 
Nasisitiza tatizo la Sendeka ni shule tu. Hakuna anae m-set anaji set mwenyewe na ukihiyo wake.

Mbunge mzima unashindwa ku behave hadharani ovyo kabisa
 
Huyu mbunge anachekesha sana. Kwani kwenda Simanjiri kwa maandamano yeye kuna mkera nini? Millya si ameenda kwao kutoa shukurani kanisani? Binafsi sipendi kuona Ole Sendeka anaswekwa jela. Lakini inavyo elekea, akikosekana msuluhishi, hii kesi inaweza kumsumbua sana inspite of all hi "symphathizers" kuwa eti anawindwa na mafisadi. Hilo halipo. Maneno yake mawili matatu bungeni against mafisadi (tena ya kuuma na kupuliza RE Mkapa) yanatosha tu kwa mediocre wenzake kumuona ni mpambanaji. To a serious person, Ole Sendeka hana lolote. Ni kuongea tu, kazi ambayo anaiweza sana kiasi kwamba hata polisi wanaoifanyia upelelezi kesi yake wanaweza kushindwa kugundua tatizo liko wapi na kuanza kumwadhibu Millya. The guy can talk!
 
Back
Top Bottom