Cannabis
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 8,938
- 25,281
Inasemekana bodi ya klabu ya Manchester United imeridhia maamuzi ya kumfukuza kazi Ole Gunnar Solskjær. Maamuzi hayo yanakuja kutokana na muenendo usioridhisha katika msimu wa mwaka 2021/22. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya klabu hiyo kupokea kichapo cha magoli 4 kwa 1 dhidi ya Watford. Inasemekana ndani ya muda wowote klabu hiyo itatoa tamko rasmi na kuwataja Michael Carrick na Darren Fletcher kama makocha wa muda mpaka klabu itakapotangaza kocha mpya.
====
Imethibitishwa, Manchester United yamfukuza Ole Gunnar Solskjær.
RASMI: MAN. UTD YAMFUKUZA SOLSKJAER
Baada ya Mkutano wa dharura wa Bodi ya timu hiyo kukaa jana kutokana na mlolongo wa matokeo mabovu, klabu imeachana na Ole Gunnar Solskjaer
Solskjaer alichaguliwa kuinoa timu hiyo Desemba 2018 baada ya Jose Mourinho kufutwa kazi