Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,291
Kwa wale Old Boys wa Old Moshi Secondary School (Moshi Secondary School),
Bila shaka tunaikumbuka shule yetu. Shule hii pasi na shaka inastahili kutambuliwa kwamba ni Shule Kongwe. Kwa tuliosoma hapo shule hii imegusa maisha yetu. Asante sana walimu wote na wafanyakazi wengine wote wa shule hii.
Kwa harakaharaka, shule hii inatuhitaji sisi wahitimu wa zamani (alumni) tuchangie maendeleo ya hali na mali ya shule hii. Tuulize vipaumbele, na tuone wapi tunaweza kujumuika.
Kwa wale wenye fursa ya kuieleza serikali, muiombe iiweke shule hii katika mipango yake ya kuboresha shule kongwe, na kutekeleza maboresho hayo ikiwa imo.
Sote kwa pamoja tutafute namna endelevu ya kuiinua shule yetu hii maridhawa.
Mwaonaje?