G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Watu wameipiga moto ofisi ya mtendaji wa kata ya Soweto mjini Moshi na kuteketeza vyote vilivyokuwepo ndani.
========
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira, amesema watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo, kwa tuhuma za kuchoma moto ofisi ya Kata ya Soweto iliyopo Moshi.
Awali tukio hilo liliripotiwa kufanywa na watu wasiojulikana, ambapo wamechoma moto ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Soweto usiku wa kuamkia jana Novemba 10, 2019, ambapo pia wamechoma nyaraka zilizokuwa ndani ya ofisi hizo.
Mkuu wa Mkoa Anna Mghwira, amesema kuwa moto huo ulianza majira ya saa 7 usiku, na baada ya moto huo kuwaka majirani waliokuwa karibu na ofisi hiyo walianza kuuzima na baadaye kutoa taarifa polisi.
Aidha Anna Mgwhira amewataka wananchi kuwa watulivu wakati vyombo vya ulinzi na usalama vikiendelea na uchunguzi.
Pia, soma:
========
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira, amesema watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo, kwa tuhuma za kuchoma moto ofisi ya Kata ya Soweto iliyopo Moshi.
Awali tukio hilo liliripotiwa kufanywa na watu wasiojulikana, ambapo wamechoma moto ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Soweto usiku wa kuamkia jana Novemba 10, 2019, ambapo pia wamechoma nyaraka zilizokuwa ndani ya ofisi hizo.
Mkuu wa Mkoa Anna Mghwira, amesema kuwa moto huo ulianza majira ya saa 7 usiku, na baada ya moto huo kuwaka majirani waliokuwa karibu na ofisi hiyo walianza kuuzima na baadaye kutoa taarifa polisi.
Aidha Anna Mgwhira amewataka wananchi kuwa watulivu wakati vyombo vya ulinzi na usalama vikiendelea na uchunguzi.
Pia, soma:
Mvomero: Ofisi ya kijiji cha Mlali yachomwa moto, vitu vyote ndani vyateketea
Wilayani Mvomero mkoani Morogoro ofisi ya kijiji cha Mlali imechomwa moto usiku wa kuamkia leo, nyaraka zote muhimu zateketea. Watu wasiojulikana, wameichoma moto Ofisi ya Kijiji Cha Mlali kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro nchini Tanzania usiku wa kuamkia leo Jumatatu Novemba 11...
www.jamiiforums.com