Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 945
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, Mkoani Geita, Mhe. Nicodemas Henry Maganga imekabidhi Kompyuta yenye thamani ya Shilingi 1,500,000 katika Shule ya Sekondari Iponya.
Kwa niaba ya Mbunge, Kompyuta zimekabidhiwa na Makatibu wa Mbunge ambaye ni Ndugu Method Nehemia na Ndugu Juma Mohamed walioambatana na Katibu wa Mtandao wa Waraghbishi Wilaya ya Mbogwe, Ndugu Leonard D. Mbigule.
Kompyuta zimekabidhiwa kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Iponya, Mwal. Stephano Kusana ambaye amemshukuru sana Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, Mhe. Nicodemas Henry Maganga kwa maono ya kuleta Kompyuta ambapo itasaidia kurahisisha na kuongeza utendaji kazi unahitaji vitendea kazi vya kisasa katika elimu.
"Tunatamani kila Idara iwe na Kompyuta, Tunamshukuru sana Mbunge wetu, Nicodemas Henry Maganga. Tumepitia changamoto hasa wakati wa kuandaa matokeo ya wanafunzi, kumbukumbu ya vitu vya kiofisi ya Mkuu wa Shule na Ofisi ya Taaluma" - Mwalimu Shule ya Sekondari Iponya
"Kimsingi tuna mahitaji ya Kompyuta hapa Iponya, zikipatikana Kompyuta zingine mkatuongezea Ofisi kubwa tano; Ofisi ya Mkuu wa Shule, Ofisi ya Taaluma, Ofisi ya Makamu, Ofisi ya Uhasibu zitasaidia sana. Tunamshukuru sana Mbunge, Mungu ambariki" - Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Iponya, Stephano Kusana.
Kwa niaba ya Mbunge, Kompyuta zimekabidhiwa na Makatibu wa Mbunge ambaye ni Ndugu Method Nehemia na Ndugu Juma Mohamed walioambatana na Katibu wa Mtandao wa Waraghbishi Wilaya ya Mbogwe, Ndugu Leonard D. Mbigule.
Kompyuta zimekabidhiwa kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Iponya, Mwal. Stephano Kusana ambaye amemshukuru sana Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, Mhe. Nicodemas Henry Maganga kwa maono ya kuleta Kompyuta ambapo itasaidia kurahisisha na kuongeza utendaji kazi unahitaji vitendea kazi vya kisasa katika elimu.
"Tunatamani kila Idara iwe na Kompyuta, Tunamshukuru sana Mbunge wetu, Nicodemas Henry Maganga. Tumepitia changamoto hasa wakati wa kuandaa matokeo ya wanafunzi, kumbukumbu ya vitu vya kiofisi ya Mkuu wa Shule na Ofisi ya Taaluma" - Mwalimu Shule ya Sekondari Iponya
"Kimsingi tuna mahitaji ya Kompyuta hapa Iponya, zikipatikana Kompyuta zingine mkatuongezea Ofisi kubwa tano; Ofisi ya Mkuu wa Shule, Ofisi ya Taaluma, Ofisi ya Makamu, Ofisi ya Uhasibu zitasaidia sana. Tunamshukuru sana Mbunge, Mungu ambariki" - Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Iponya, Stephano Kusana.