Kiboko yao Mwalimu, nasikia Henry Kissinger wakati huo Foreign Sec alitia mguu Bongo na kama kawaida ya manjonjo ya Marekani alikuja na gari yake ya kumtembeza akiwa Bongo. Hii gari inadaiwa ilitakiwa itolewe haraka kabla hajafika. Mwalimu akatia ngumu anakuja na nyumba yake pia? Akajibiwa ni gari tu na vifaa vingine. Kwa jeuri ya Mwalimu akauliza tena kwani aliambiwa huku hatuna magari? Basi akasema atapanda magari haya haya tunayopanda sisi au arudi kwao. Basi gari haikutolewa bandarini na njemba ikapanda gari ya Ikulu. Chezeya Mwalimu weye!! RIP Baba wa Taifa.