Oa au olewa na Mzanzibar ili mtoto wenu awe na hadhi + uwanja mpana wa kufanikiwa (Zanzibar citizenship privilege)

Pia, huwa najiuliza, hao Wazanzibar ambao hawautaki muungano huwa wanatoka wapi? Kwa sababu ukiutazama muungano kwa haraka haraka, wanaonufaika zaidi ni Wazanzibar kuliko Watanganyika.



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Kwasababu wanaamini wana fursa nyingi za kimaendeleo ambazo zinakosekana kutokana na huu Muungano,.

Na moja ya tatizo jengine kubwa la wazanzibari kwa Muungano ni hili la SMT kulazimisha CCM itawale Zanzibar hali yakua imeshakataliwa kitambo sana, 90% ya wa zanzibari hawaitaki hata kuiona, ila inaendelea kuongoza kupitia mgongo wa SMT. Hilo jambo lina wa frustrate sana kwa kweli.
 
Yaani mtoto wangu aanze kula urojo na aluwa badala ya ugali wa dona hapana aisee atajiajirk tu
 
tatizo la mbongo akikataliwa tu anahisi amebaguliwa kwa rangi yake, anashindwa kufahamu factors nyengine nyingi zinazopelekea

Hiyo kitu ipo kwenye damu,,,washajiwekea ni watu wa kubaguliwa. Mfano, mtu mweupe akimuita black wewe "kima" njoo hapa italeta maana mbaya, but akitokea mweusi akamwambia mweusi mwenzie wewe "kima" njoo hapa, umeona ee 😂 hapo nani ataonekana mbaya? Ni white people
 
Kwann ndugu ? Maana mi nazungumza kulingana na experience ...... au Kama kuna kimwana toka kisiwan ni connect nae na. Mie NI wowe mZnz

sio kitu rahisi mwanamke kukapa nyuma kama unavyofikiria, hata madada poa hueka bei ya juu zaidi kwa vile kuna thamani zaidi kutokana na mazingira ya kiulimwengu yanavyokwenda, halafu wewe unasema mwanamke akunyime mbele akupe nyuma? siku zote nyuma hua ndio silaha ya mwisho ya mwanamke, acha story za vijiweni hizo.
 
sio kitu rahisi mwanamke kukapa nyuma kama unavyofikiria, hata madada poa hueka bei ya juu zaidi kwa vile kuna thamani zaidi kutokana na mazingira ya kiulimwengu yanavyokwenda, halafu wewe unasema mwanamke akunyime mbele akupe nyuma? siku zote nyuma hua ndio silaha ya mwisho ya mwanamke, acha story za vijiweni hizo.
Vyovyote unavyo bisha lkn reality on the ground ndio nilicho kichangia, wasichana wengi wa Znz kule kisiwan ni vigumu mnoooo kuolewa na kijana toka bara,

Na wana sababu zao bayo kimsingi ni ubaguzi tu, Hali ipo tofauti huku bara Dada zetu Wana pachikwa Sana mimba na vijana toka kisiwan Al maarufu wa pemba
 
View attachment 2034209

Soma kwa makini, hakika utakuwa umemrahisishia maisha mtoto wako, wa kuuchukua uamuzi ni wewe mzazi wake mtaajiwa.

Wengi wanaweza kudhani hii maada nimeianzisha kwasababu raisi wa sasa ni mzanzibari, la hasha!! Uraia wa Zanzibar una hadhi ya juu sana kuliko huu uraia wa Tanzania tangu zamani.

Kwanini uoe au kuolewa na Mzanzibari?

Idadi ya wazanzibari ni ndogo takribani milioni 1 na nusu, lakini muungano unawapa nguvu (power), influence, ajira, n.k kubwa sana kuzidi kundi au kabila lolote unalolijua na ndio maana nakushauri upigane kufa kupona ili mtoto wako aingie hili kundi.

Moja ya njia ya kupata huu uraia mtamu ni mtoto kuwa na mzazi moja mwenye uraia wa Zanzibar, kwa hio ukioa au kuolewa na mzanzibari, mtoto weny atakuwa raia wa kizanzibari.

FAIDA ATAZOPATA MTOTO WAKO AKIWA RAIA WA ZANZIBAR

A. Kuwa katika kundi lenye nguvu kubwa kuzidi kabila lolote

View attachment 2035151


Ujumbe wangu hapa ni kwamba, nafasi ya mtoto wako kupata nafasi za uongozi aidha kwa huku bara au Zanzibar ni mkubwa endapo atakuwa ni raia wa Zanzibar maana wapo wachache takribani milioini 1 tu na wana fursa ya kupata vyeo vingi sana tofauti na huku bara kwenye watu milioni 60 wanaopambania vyeo vichache.

Ili kuwe na muungano ni lazima kuwe na mchanganyiko wa pande mbili katika uongozi, mamlaka, maamuzi na hata hizo ajira. Na ndio maana hata kwenye nafasi za uraisi au makamu wa raisi inabidi kuwe na pande mbili (Zanzibar ndio jamii pekee inayotoa rais au makamu wa rais kila mara lakini haijawai kutokea kabila flani kutoka bara kujirudia kupata hivyo vyeo kama ilivyo kwa Zanzibar wanavyojirudia miaka nenda rudi kupata Urais na umakamu ) hata kwenye vyeo vingine vikubwa lazima mzanizbari awepo, kwenye mawaziri lazima Zanzibar iwepo, uko jeshini jwtz lazima wawepo majenerali na maluteni wazanzibari, polisi inabidi kuwe na ma rpc kutoka Zanzibar, n.k. hivi ni vyeo vizito haswaa vyenye powe na influence kubwa sana. Mchaga, msukuma, mhaya, mnyakyusa, mpare, n.k wanabadilishwa mda wowote na anawekwa mwengine lakini hadhi ya nafasi ya Mzanzibari inabaki pale pale tu. Hali hii inawafanya wawe jamii yenye nguvu kubwa kuzidi kabila lolote ulijualo hapa bara, hii pia inawasaidia mno kwenye kushikana mkono, mkuu wa idara flani akiwa mzanzibari anaweza kupandisha wenzake vyeo, kuwapa wenzake kipaumbele kwenye ajira, n.k. Ukiachana na nguvu waliyo nayo huku bara, bado wana serikali yao ambayo raisi, makamu wa raisi, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugezi wa taasisi, majaji wa mahakama, wabunge, n.k ni lazima wawe wazanzibari.


B. Urahisi wa kupata ajira za bara

View attachment 2034920


hapa nazungumzia ajira za muungano kuanzia wizara mbali mbali, jwtz, usalama wa taifa, ikulu, tra, benki kuu, bandari, polisi, tbs, n.k. mtoto wako ukimkazania apate hizi diploma au degree ambazo zimejaa kama utititiri kwa watu wa bara, nakuhakikishia itakuwa ni tiketi kubwa sana ya mtoto wako kula mema ya nchi kwenye ajira za muungano, katika huu muungano kuna makubaliano kwamba katika kila nafasi 100 inabidi wawepo wazanzibari 21 sawa na asilimia 21, nakukumbusha kwamba katika watanzania 100 kuna wazanzibari wawili tu, kwao hizo nafasi ni nyingi sana na kuna muda huwa hawazijazi.

huko kwenye interview kigezo kinachoangaliwa zaidi ukiwa na mtoto mzanzibari kitakuwa ni uraia wake maana kwanza wanakuwaga wachache ila kwa upande wa mtoto wa bara ushindani ni mkubwa mno usipime!! Makumi ya maelfu ya wanafunzi humaliza vyuo kila mwaka na wengi hubaki mtaani, ajira zikitangazwa ni vurugu, yani hadi upate kazi ni shughuli pevu si mchezo, utachunguzwa hadhi ya chuo ulichosomea, ufaulu wako chuoni (gpa), umejitolea kwa miaka mingapi kwenye mashirika ili upate zoefu, uzito wa cv yako, n.k. Hata huko vyuoni, mzanzibari sio wa kumdharau eti kisa ana ufaulu mdogo, hapo mkimaliza chuo, wabara waliokuwa wanafaulu vizuri wanaweza kusota sana kupata ajira lakini mzanzibari huyo huyo aliekuwa na ufaulu mdogo anapata ajira fasta tu, tena cheo kizuri tu. sasa uchaguzi ni wako kumuingiza mtoto kundi jepesi ama hili lenye mikiki mikiki.

C. kupata ajira za zanzibar ambazo raia wa bara hana sifa

View attachment 2034933


Serikali ya zanzibar kuna bunge lao, wizara zao, ikulu, n.k ambako wanaajri wazanzibari tu. pia kuna ma mia ya taasisi na mashirika yao ambayo hutoa ajira kwa wazanzibari pekee, mfano tanesco yao inaitwa zeco, tra yao inaitwa zrb, tff yao inaitwa zff. Nssf yao inaitwa zssf, tbs yao inaitwa zbs, n.k.

Ukiwa na mtoto ataekuwa na uraia wa Zanzibar basi inawezekana kabisa mmoja akaajiriwa ajira za muungano Tra mkoani Mbeya na mwengine akaajiriwa taasisi ya Zanzibar kama Zrb, zff, zeco, n.k. Ukiwa na mtoto wa bara hataweza kuajiriwa hizo taasisi za Zanzibar nilizozitaja huko labda itokee hawana wataalam husika. Wala nisikuumize sana kichwa, kiufupi ni kwamba mtoto wako akiwa mzanzibari ataua ndege wawili kwa jiwe moja tu maana ajira za huku wazanzibar wana mgao wao mzuri tu wa asilimia 21 na huko kwao wana ajira nyingi ambazo zipo kwajili yao.


D. Kuendeleza kizazi cha kuwa na Watoto / wajukuu wataofaidi mema ya muungano – kwa kuwa mtoto wako atakuwa ni mzanzibari, basi hata Watoto wae na wajukuu watakula mema ya huu uraia miaka nenda rudi,

Kwa hayo mambo niliyoyawka hapo nakushauri, Hata wakikucheka unajipendekeza hakuna shida, hapo ni kwamba unamtanulia goli mtoto wako aje kupata nafuu ya maisha
UZI HUU UMESHINDIA TUZO YA .... "UZI WA KIJINGA NA WA KIPUUZI" YA MWAKA 2021.

tuzo hii hutolewa kila mwaka.

HONGERA SANA KIJANA
....ukikua akili yako itabadilika.
 
Eti Raia wa Zanzibar, hakuna kitu kama Raia wa Zanzibar, sote ni Raia wa Tanzania
Mkuu acha ubishi usichotaka kuelewa ni kipi?? Au unajifanya huelewi wewe?? Unaambiwa ukiwa mzanzibar una nafas kubwa ya kupata ajira maana kweny serkal ya Tanzania una nafas ya kupata na pia kweny serkali yao ya zanzibar au hujui kama mtanzania wa bara huruhusiwi kumiliki ardhi huko zanzibar??? Japo ww ni mtanzania mbara???


Kuifupi wazanzibar nawasifu na nawakubali wanajielewa sana ona wana katiba yao inayo walinda na kusimamia mambo yao ya zanzibar na kuna vitu vingi tu ukiwa wa bara huruhusiwi kumiliki kwao ila sisi sasa mzanzibar ana miliki ardhi anavotaka wakati sisi kwao hatuna huo uwezo wala urashi ama mamlaka hapa ndipo nawasifu viongozi wa wanasiasa wa zanzibar wana fanya vitu kwa faida ya watu wao sio sisi viongozi wetu na wanasiasa wetu wana fanya vitu kwa masirahi yao na familia zao na ukoo wao ila sio kwa wa Tanzania wote mpaka sasa kungekuwa na limit ya baadhi ya mambo kuwa zuia kama ambavo wao wametuzuia kumiliki ardhi na kupata kazi kwao mpka uwe mzanzibar

Huu muungano bana una chekesha sana inaonekana kama sisi bara ndo tuliwaomba zanzibar tuungane ndoo maana vitu vingine tu nawapa buree ama kuwaaamehe na kuwaonea huruma furani huku wao wakinufaika na kufaidika sana na huu muungano wetu, umeme, fedha za maendeleo, mambo ya kimataifa nk..

Na sisi tunataka tuwe na Tanganyika yetu na ungekua na serkali yake kamili na katiba yake pia na tungeweka vipengere kama vya zanzibar ili tuwe sawa ila kwa sasa haipingiki kabisaa wazanzibar wametupiga bao ukunali ukatae ukiwa mzanzibar una nafasi kubwa kupata ajira kuliko kuwa mtanzania bara.. Ndio maana katiba ya mpya wa mzee Warioba ilitaka muungano wa shirikisho ndo ilikuwa dawa ya haya yote.
 
Haina ubishi kwa zanzibar, mwarabu huwa ana hadhi kama ya mfalme hivi, yani mtu akioa au kuolewa na mwarabu ni kama muujiza hivi, kiukweli kuna tatizo kubwa sana la kutukuza waarabu.

Mbaya zaidi, hao waarabu wengi (sizungumzii waarabu koko) hata wao kwa wao tu wanabaguana koo za kuoa au kuolewa, hata waarabu wa hapo Zanzibar ili uoe binti yao labda uwe muarabu (sio muarabu koko) au kama ni chini ya hapo basi uwe tajiri sana ama uwe na madaraka makubwa sana serikalini, hivi hivi ni ngumu sana.

Hao wamama wengi wa Oman wenye zaidi ya miaka 40 wanakuwa wamekosa soko ila kwa vile mwanamke wa kiarabu hata akichuja huko kwao bado ana soko kubwa kwa wazanzibar, basi inabidi ajishushe tu kuolewa hivyo hivyo tu na Mzanzibar.
Mkuu sio lazima kuoa tu unaweza kuolewa pia mkuu hakuna anaekukataza olewa tu na wewe.
 
Mtoa mada ni zero brain miaka 20 ijayo unajua kuwa ajira zitakuwa zipo vp hata bibi toto atakuwa kazikwa muda mrefu
Hiyo yako moja!! pili;; mleta mada ni mvivu kupindukia badala ya kufikiri kujiajili alipe kodi kwa kutetemekewa km Bakhresaa yeye anawaza vijicent-vya kuajiliwa kiubwete ale kwa kupiga magoti, ivi hili jamaa kweli hivi?

unaweza kuoa km ukimpenda tu!! siyo eti ajira mweee!!...ajira ni kichwa chako kwa nini wewe usitoe ajira kwa wazanzbari??? shule za kata hizi ni majanga kwa kweli!! yaani wanawaza kuajiliwa tuuuu!!! siyo kuajili!!!

en!!eeheee!! ajira nyingine ufisadi kwa nini watu hawapendi ufisadi?? piga hela ndefu kifisadi sasa mie na kuwa fisadi wa Dunia yaani siku hizi bana ufisadi cheo!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom