Foxhound
JF-Expert Member
- Dec 15, 2013
- 28,063
- 74,468
Habari za kupotea?Ha ha ha
Habari za kupotea?Ha ha ha
si kwa mwanamke atiiHivi mnapesa za kuchezea? Nywele nyingi huongeza matumizi ya sabuni buaana eeh!!!
Mimi nina rules kadhaa nimejiwekea kwa nywele zangu natural na nimeona maendeleo kwa kweli...mwanzo ilikuwa zikirefuka tu nanyoa ili ziwe fupi iwe rahisi kuchana na kustyle...lakini nimejifunza cha kufanya ili nywele ziwe laini, zichanike vizuri na kunyooka
1. Fanya conditioning (tunaitaga steaming)
Nywele zinafubaa kwa kukosa matunzo jamani. Fanya deep conditioning kila wiki mara 1 na kila unapotaka kusuka fanya deep conditioning kabla. Deep conditioner zinauzwa madukani au unaweza kufanya ya asili kwa kutumia mix ya ndizi, parachichi, asali, yai na mafuta ya nazi.
Conditioner unakaa nayo dk 30 hadi 40 then unaosha.
2. Mafuta hayazipi nywele unyevu bali yanasaidia kuhifadhi unyevu. Kitu kinachofanya nywele zinakuwa ngumu na kupata tabu kuchanika na kunyooka ni kukosa unyevu.
Kosa tunalofanya wengi ni kudhani mafuta yatazipa nywele zetu unyevu. Unyevu unapatikana kwenye maji au kuna bidhaa zinauzwa zenye kutoa unyevu kwa nywele (Moisturizers au leave in conditioners)
Hivyo kama mzururaji juani kama mimi hakikisha kila asubuhi au jioni unanyunyizia nywele yako maji au unapaka moisturizer yako au leave in halafu unapaka mafuta ya chaguo lako kwa juu ili kuhifadhi unyevu. Achana na habari za nywele ukiweka maji zinanuka, ni myth tu labda ziwe chafu. Kama si mzururaji unaweza kufanya hivi kila baada ya siku 2 au 3...
3. Chana nywele kwa kuzigawa kwenye mafungu. Jamani mimi nilikuwa kinara wa kusema "nywele zangu hazichanikiii". Lakini tatizo lilikuwa ni kulazimisha kuzichana tu randomly mara chana imeingia hapa imetokea kule.
Gawa nywele zako hata sehemu zisizopungua 4 kisha kwa kila fungu paka leave in yako na mafuta yako, chana. Ukimaliza suka kisection chako au kibane kisivurugike hamia kwingine.
Maisha mepeeesiiiii
4. Usilale na nywele natural bila kuzisuka mabutu. Hutokufa, utaamka nazo lakini huo mfungano utakaokutana nao asubuhi utazichukia.
Zisuke mabutu nywele zako kabla hujalala hasa kwa wenye ndefu, atleast wenye fupi wanaweza kulala nazo hvohvo. Kisha jifunge kitambaa au vaa kofia.
5. Google jinsi ya kuzistyle nywele zako wewe mwenyewe. Jamani mimi naamini katika theory ya mkono mbaya. Kuna watu wana mikono mibaya kwa nywele, akikushikashika nywele zinadhoofu.
Minimize ishu za saluni, style nywele zako mwenyewe.
Na kuna styles nyingi nzuri sana kwa nywele za asili, Hebu cheki hizi hapa chini
View attachment 640374
View attachment 640375
View attachment 640918
NB:
Nimeona kuna mtu hapo juu anasema ukipaka leave in au products za Aunt Jackies nywele zako zinakuwa kama umeweka dawa; Sijui ana nywele aina gani ila kwa wenye kipilipili kile concord chenyewe naomba nipingane nae, ni nzuri, zinarahisisha uchanaji na nywele zinakuwa laini ila sio kama umeweka dawa; asije fanya watu mkawa na matarajio ya juu sana halafu mkaja kumuita muongo.
Natumia Leave In Conditioner yao inaitwa Quench, Kuna Leave-in detangler ya watoto inaitwa Knot having it(hii nilinunua tu kwa kupenda rangi ila kwakweli haina ulazima), natumia na detangler inaitwa Knot on My Watch na Defining Curl Custard yao ya Curl La La.
Hizi products ni NZURI SANA. Yani nywele unachana vizuri, ukitaka kufanya style zile za kusokota halafu unafumua zinabaki na mawimbi, ukitaka kupaka tu halafu unaacha nywele zinaonekana mawimbi yake ya asili, ni wewe tu na bei zake ni affordable sana 15000 tu.
Kwa mnaopenda kunyoosha nywele bila kutumia blow dryer angalieni video hiyo..
Wasalaam.
nanyoosha baaba ya muda zinaachia bnaKwa nn ucnyooshe?? Afu uwe unafanya steaming...... Mm nina kipilipili ila dawa cweki nakomaa
Sent from my TECNO W4 using JamiiForums mobile app
mmmh ucjaribu kuwekaa dawa,, utabaki kipara,, zangu nikiweka dawa zina katika zote nabaki na kipara,, weka steaming,, hina ya majani changanya na yai la kienyejii kwa mwezi mara mbili , paka kwenye mizizi ya nywele,, utanipa matokeonina nywele natural ila kipilipili cha hatare.nataka zinyooke .ukiweka dawa zitaota tena?
weka sample ya wigi na bei dearnauza mawig na maweaving original karibun
Auntie Jackies ni bei poa ila nzuri sanaaaa... Tena ukiwa na seti nzima utapenda. Mii nina dry hair lakini with aunt Jackies zimekuwa laini hadi nazionea raha. Try that maaMy dear ukiweka dawa lazima new growth itokee, kwa hiyo itakulazimu uweke tena dawa
Ila kama hutaki nywele za dawa siku hizi kuna products nzuri za natural hair, try za cantu ila za auntie jackie naona zipo cheaper kidogo
Uwe unafanyia na steaming Mara kwa Mara..... Mm zangu mpka sasa zimekua ndefu na bdo naturalnanyoosha baaba ya muda zinaachia bna
Mimi kipilipili changu ni dread toshaa, naziosha na kuzipaka mafuta basi nasepa zangu....watu wanauliza dread nimetengenezea wapi kumbe ni asili tu, kipilipili cha kisomaliMaana ninakipilipili sio cha nchi hii ukichana mbele nyuma zimejirudi ukimaliza nyuma mbele zimevurugika nilijaribu kueka dawa zinakatika nikisuka rasta za aina yeyote baada ya mtindo labda ninyoe nianze upya maana zinazunguka kukatika mateso ya nini nimejiekea dread hapa aaaaaa nakula bata tuu
Anapatikana mkoa gani na anauza bei ganiMpigie 0769302206