Nyerere's legacy failed 100% (economically)

Nyerere's legacy failed 100% (economically)

Nyerere hakufel sema kuna watu ndo walimfelisha.


Magufuli hatofeli ila kuna watu ndo wanataka kumfelisha.
Kama mtu ameutaka urais then anashindwa kuwaControl watu ambao amewateua basi hakutakiwa kuomba hiyo nafasi. Yeye ndiye kiranja mkuu wa nchi, chochote kile kibaya kikifanywa na wateule wake ni sawasawa amaefanya yeye. Tusiwape defencr ya kitoto kama hiyo.
 
Kama mtu ameutaka urais then anashindwa kuwaControl watu ambao amewateua basi hakutakiwa kuomba hiyo nafasi. Yeye ndiye kiranja mkuu wa nchi, chochote kile kibaya kikifanywa na wateule wake ni sawasawa amaefanya yeye. Tusiwape defencr ya kitoto kama hiyo.
RAIA Wa nchi hawatokuja hata sikumoja wamkwamishe Rais. Isipokua nguvu kubwa toka nje ndo inayokwamisha.

Fatilia mashariti alopewa nyerere ndo ujue ninachokisema.
 
Heheheeee. Upuuzi wa kuamini fikra za mwenyekiti ndio umetufikisha hapa tulipo. VENEZUELA wanashikilia zidumu fikra za mwalimu, wanalowea kwenye mfumuko wa bei kama zimbabwe

Maendeleo hayaji bila kuwa na maadui
 
Umesema ukweli mtupu nyerere alitulositisha kama nchi mi sioni kitu cha kujivunia cha ajabu alichofanya

Kwa sababu umekariri mambo niambie hizo nchi za Afrika zilizochukua a different path na zikafanikiwa
 
huyu nyerere kakaa madarakani zaidi ya miaka ishirini,na bado kiuchumi kafeli.

kaenda kuadopt ma ideology ambayo kwa context yetu hayakuadoptika.

unaanzisha vijiji vya ujamaa ili ufuge watu kama mbuzi,mwisho wa siku kauwa kilimo,huku mwenzake kenyatta akipiga watu wake shule,

una preach self reliance,na bado unategemea misaada ya wazungu,what a shame.

naona na Zakayo mtoza ushuru anataka apeleke mitumba ulaya🙂

Kwa akili kama hizi WaAfrika tutaendelea kutawaliwa till the end of time
 
Hivi ilikuwaje Siasa za Ujamaa ziliwekwa katika nchi bila Kupata maoni ya Watanzania?. Je hayo hayakuwa mawazo ya Nyerere zaidi kuliko kuwa ni ya wananchi?
Kwa sababu kila nikisoma vitabu vya Azimio la Arusha sijaona mahali popote umma ukishirikishwa kupata input yake ya aina ya uchumi inaoutaka, kama ni uchumi wa kijamaa, kibepari au chochote kile!.

Unaweza kusema labda chaguzi kuu zilizofuata ziliipa TANU uhalali wa kufuata siasa za Ujamaa, lakini Wananchi walikuwa na chama kimoja tu na mgombea mmoja kila uchaguzi kwa hiyo hawakuwa na mbadala sahihi!, utake usitake lazima mtawala angetokea TANU!!! .yaani TANU was an alternative of itself!!

Ungekaa ukafikiria utofauti wa watu wa 1960 na 2017 nadhani usingeuliza swali kama hili
 
Aliyeshindwa sio NYERERE bali wale waliokuwa chini yake na ambao hawakuwa tayari kusupport kwa ajili ya maslahi yao.....Walitaka viongozi wawe miungu watu wkt NYERERE alitaka usawa wa kiuchumi, kidini, etc.....
.....................NYERERE HAKUSHINDWA.......................
 
Tukiorodhesha nchi zilinonufaika na ujamaa basi orofha ni China, Urusi na nyingine chache zizofika 10. Lakini tukiorodhesha nchi zilizonufaika na mifumo ya kipebari orodha ni ndefu sana. Huoni kua ni poor choice kuchagua njia ambayo ni wachache tu walifanikiwa kwa kuipitia??

Nyerere hakuwa mbinafsi na alikuwa mtu mwenye akili sana asingeweza kufanya vitu kwa sababu tuwengine wanafanya . Taja nchi ya Afrika iliyo mfumo wa kibepari na imefanikiwa sio bla bla
 
Ni nchi chache sana duniani ambazo hazikupitia mfumo wa ujamaa, ndo ulikuwa ni mfumo uliotumika kwa ajiri ya udhalishaji kabla ya capitalism, ndio maana nasema kuna economic stage hata Europe walizipitia kabla ya kuingia capitalism, sisi kwa sasa kuingia capitalism bila kuwa udhalishaji au viwanda tunabakia kama watazamaji tu, na kuwa MANAMBA katika nchi zetu.
History of socialism - Wikipedia[/QUO


Real?
 
Nyerere hakuwa mbinafsi na alikuwa mtu mwenye akili sana asingeweza kufanya vitu kwa sababu tuwengine wanafanya . Taja nchi ya Afrika iliyo mfumo wa kibepari na imefanikiwa sio bla bla
800px-Socialist_states_by_duration.png

Hiyo ni ramani ya nchi zilizowai kujitangaza kuwa za ki socialist katika historia zao. Japo nyingi ziliachana na hiyi sera baada ya kukosa mafanikio
 
6. Kushindwa kuzuia rushwa serikalini na katika mashirika. Mtu anapewa umeneja wa kiwanda au taasisi anaiba anafilisi kisha anahamishwa toka sehemu moja kwenda nyingine. Ilipaswa afikishwe mahakamani na afilisiwe. Hicho ndicho kimeigwa mpaka leo


Hata kikwete alishindwa kuzuia rushwa na ndicho kipindi rushwa ilitamalaki hadi kufikia Dr Dau kujifanyia atakavyo na kufikia kufilisi nssf. Mabilioni aliyoiba Nssf ni ya kufuru
 
1,2,3,4na 5. Ni kweli iso pingika.... UTOPIA. tulilishwa upepo siasa za ujamaa, ni dhambi kubwa pekee kabisa ilo sababisha yote yaliyofuata. Ila kuna mema na mazuri ambayo huwa yanafanya dhambi ya ujamaa ifutike. Amani na utengamano UMOJA wetu kama watanzania. This makes him my personal hero.
 
Nyerere legacy failed 100%.

1. Kuchagua sera za ujamaa lilikua kosa lake kwanza.

2. Kuchukua viwanda, Shule, taasisi na kuzitaifisha lilikua kosa kubwa.

3. Kuanzishwa vijiji vya ujamaa kwa kuwakusanya watu kwa mkono wa chuma was a great mistake. Watu walipoteza mali, wengine kushindwa kucope na mazingira mapya ya kulazimishwa.

4. Kuzuia mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kukosolewa na zikabaki zidimu fikra za mwenyekiti. Here we are.

5. Kutumia rasilimali za nchi kukomboa mataifa mengine bila mkataba wa kurefund izohela baada ya Uhuru. Check Mozambique Na South wanavotufanyia wamesahau tuliyowafanyia so bora tungekuwa kama Marekan hatumii fedha zake katika vita bila return .

6. Kushindwa kuzuia rushwa serikalini na katika mashirika. Mtu anapewa umeneja wa kiwanda au taasisi anaiba anafilisi kisha anahamishwa toka sehemu moja kwenda nyingine. Ilipaswa afikishwe mahakamani na afilisiwe. Hicho ndicho kimeigwa mpaka leo.

7. Alichangia kuendelea kwa katiba inayotuumiza hii leo. Hakuamini nguvu ya upinzani, aliamini katika chama chake pekee. Ilifika anasema rais bora atatoka CCM pekee why?

Tunapaswa kumpima mtu economically kujua alifaulu ama alifeli.

Uchumi wa Tanzania upo chini sana kwasababu ya sera zetu tulizoamua kuingia bila referendum kujua kama watu wanaafiki ama la.

Siamini kama kuna haja hiyo ya kucelebrate life ya Mwl. Katika context ya economy.
Kiuchumi dhambi ya ujamaa ilikuwa kubwa sana na mpaka sasa maumivu yake bado tunayaishi.
 
Nyerere legacy failed 100%.

1. Kuchagua sera za ujamaa lilikua kosa lake kwanza.

2. Kuchukua viwanda, Shule, taasisi na kuzitaifisha lilikua kosa kubwa.

3. Kuanzishwa vijiji vya ujamaa kwa kuwakusanya watu kwa mkono wa chuma was a great mistake. Watu walipoteza mali, wengine kushindwa kucope na mazingira mapya ya kulazimishwa.

4. Kuzuia mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kukosolewa na zikabaki zidimu fikra za mwenyekiti. Here we are.

5. Kutumia rasilimali za nchi kukomboa mataifa mengine bila mkataba wa kurefund izohela baada ya Uhuru. Check Mozambique Na South wanavotufanyia wamesahau tuliyowafanyia so bora tungekuwa kama Marekan hatumii fedha zake katika vita bila return .

6. Kushindwa kuzuia rushwa serikalini na katika mashirika. Mtu anapewa umeneja wa kiwanda au taasisi anaiba anafilisi kisha anahamishwa toka sehemu moja kwenda nyingine. Ilipaswa afikishwe mahakamani na afilisiwe. Hicho ndicho kimeigwa mpaka leo.

7. Alichangia kuendelea kwa katiba inayotuumiza hii leo. Hakuamini nguvu ya upinzani, aliamini katika chama chake pekee. Ilifika anasema rais bora atatoka CCM pekee why?

Tunapaswa kumpima mtu economically kujua alifaulu ama alifeli.

Uchumi wa Tanzania upo chini sana kwasababu ya sera zetu tulizoamua kuingia bila referendum kujua kama watu wanaafiki ama la.

Siamini kama kuna haja hiyo ya kucelebrate life ya Mwl. Katika context ya economy.
doesn't make sense
 
Tumekuwa kwenye socialist 23 yrs, lakini tumekuwa kwenye capitalism for 30+ yrs ,mbona hatujafaulu? tumejaribu hata kuuza viwanda vilivyojengwa katika awamu ya kwanza ili twende na kasi ya capitalism lakni bado tunasota, leo hii tumeambuliwa kuibiwa tu, wht does it mean? capitalism ni open up markets for well developed countries waje wafanye biashara zao katika nchi yako, wewe unabaki kuwa mtazamaji, maana hata kodi unayokusanya ni hafifi kutoka kwao ,wanajua bado hamko na elimu ya kutosha na sharia za kuwabana, ndo hayo yanatokea Acacia ,Barick, dangote kule anae anapiga, wachina nao wanakuja na kampuni zao wakiwa na wafanyakazi wake, wanaajiri 5% ya watanzania katika makampuni yao kama assistants hata kama wanaelimu nzuri, ni aina nyingine ya unyonyaji, serikali zetu zimebaki kama watazamaji tu, kwa ufupi bila kumung'unya kwa sasa Bara la Africa UTEGEMEZI umeongezeka zaidi.
 
7. Alichangia kuendelea kwa katiba inayotuumiza hii leo. Hakuamini nguvu ya upinzani, aliamini katika chama chake pekee. Ilifika anasema rais bora atatoka CCM pekee why?

Sio alichangia kuendelea kwa katiba iliyotuumiza, aliandika katiba YEYE na KAWAWA na MSEKWA!

Halafu, alivyokuwa na smug balls anatoka madarakani kaitumia katiba miaka 24 halafu anatuambia NYINYI MNA KATIBA MBAYA SANA YA KIDIKTETA.

Nani kaandika hiyo Katiba, IDDI AMINI? Cosmic levels of hipocrisy.
 
Nenda kawaulize huko Rwanda mnapopasifia kama mtu anaamua kuishi anapotaka.

Vijiji vya ujamaa vilikuwa na lengo la kuwakusanya watu sehemu moja ili kuwezesha serikali kuwahudumia vizuri na kwa gharama nafuu. Kingibe ni security ya Nchi. Kuna wakati mnadhani mnafahamu kila kitu kumbe ni hamna kitu.

Kama kila mtu ataamua kuishi atakapo maana yake atataka shule na hospital nk. Mna hela za kuwahudumia. Hii ilifail kwa sababu ya uvivu wa babu zenu kama si baba zenu na si Nyerere.

Mliamua kumzunguka mkisaidiwa na wazungu wenu but he was right na tunhekuwa mbali sana.
Tatizo ni utekelezaji. Kumbukeni nyerere alimchagua sokoine kuwa waziri mkuu ambaye aliisimamia kiukweliukweli hio ideology ya ujamaa. Cha ajabu alifariki katika mazingira yenye utata mwingi. na ufuatiliaji wa kifo chake sidhani kama ulikua yakinifu. Ndio maana naungana na mtoa uzi kua nyerere alifeli
 
Mimi sioni tatizo lake katika mifumo aliyoaianzisha ,kwa sababu kuu ni moja kuwa lengo lake kuu halikuwa kujilimbikizia Mali ,Bali lilikuwa ni kuitoa nchi kutoka hatua moja kwenda nyingine,kufeli kwa sera kunatokana na sababu mbalimbali,ikiwemo watendaji,wapokeaji n.k
Kwa hiyo kwangu Mimi sijaona tatizo kwake labda vijimapungufu vya kibinadamu tu.
 
Hufahamu kuwa Department of Treasury ndiyo inamiliki the Fed. Pia sijakuuliza kuhusu air force one, nimekuuliza nani mmiliki wa majeshi haya. Na haya majeshi yanamiliki nini au nani ni muuzaji wa f-16s, jeshi au Boeing?
nANI MMILIKI WA AMTRAK, USPS ..

Achana na hayo, nani mmiliki wa ARAMCO?, GAZPROM, STATOIL
Serikali ya marekani huwa inatoa kandarasi kwa makampuni binafsi kutengeneza vifaa na mifumo ya ulinzi. Kwenye mikataba serikali inakuwa na hakimiliki ya teknolojia kwasababu za kiusalama. Pale marekani inapoamua kuiuzia nchi nyingine vifaa au mifumo ya kijeshi serikali ndio inatoa ridhaa kwa sababu ya kuwa na hakimiliki. Mara nyingi nchi moja inapoiuzia silaha nchi nyingie ni lazima silaha hizo zitakuwa zimepitwa na wakati au kuna slight modification. Mfano mzuri ni ndege f22 amabazo Australia, Israel, UK wameuziwa na marekani. Kila nchi imefanya modification kwenye avionics na mifumo mingine ya mawasiliano. Ukweli ni kwamba makampuni binafsi yanatengeneza vifaa vya kijeshi kwenye nchi za magharibi, nchi za mashariki kampuni nyingi zinamilikiwa na serikali.
 
Back
Top Bottom