Nyerere's legacy failed 100% (economically)

Nyerere's legacy failed 100% (economically)

Benki kuu ya marekani (federal reserve bank) inamilikiwa kwa hisa na watu mbalimbali,
Airforce one ni jina tu la kijeshi linayopewa ndege anayokuwemo raisi wa marekani kwahiyo hata akipanda panga boi yetu jeshi la marekani litaiita "airforce one" . Ndege inayotumiwa kama airforce one mara kwa mara kwa sasa ni Boeing VC-25, inafanana kwa kiasi na Boeing 747. kampuni ya boeing ilianzishwa na William Boeing mwaka 1919.
NASA, US ARMY, NAVY na vingine ilivyo orodhesha ni taasisi na majeshi kama TISS na JWTZ, hazifanyi biashara wala haziendeshwi kibiashara
Najitahidi sana kutumia lugha nzuri (samahani kama nitakukwaza).
Hufahamu unachozungumza na pia hujaelewa hata maswali niliyokuuliza.
Tuishie hapa kwa sababu hatutaelewana, itabidi tuanze upya na tutatoka nje ya mada.
 
Andika pia upande aliofau.
Huko ndiko kunatupa sababu za kumkumbuka
 
Najitahidi sana kutumia lugha nzuri (samahani kama nitakukwaza).
Hufahamu unachozungumza na pia hujaelewa hata maswali niliyokuuliza.
Tuishie hapa kwa sababu hatutaelewana, itabidi tuanze upya na tutatoka nje ya mada.
Kipi unachodhani sikifahamu??
 
Assadsyria3 utakuwa umekula bangi au umechanganyikiwa!!! Umekuwa mwehu!!! Shame on you!!! Umeongelea mabaya tu ya mwalimu !!! Tena katika siku yake muhimu zaidi katika nchi yetu!!! Hivi leo unajiita Mtanzania !!!!

Do you know who was behind that movement? You deserve to be denied your TZ citizenship and deported from Tanzania!!!
Mod tusaidieni huyu mhaini aondoke TZ.
 
Kipi unachodhani sikifahamu??
Hufahamu kuwa Department of Treasury ndiyo inamiliki the Fed. Pia sijakuuliza kuhusu air force one, nimekuuliza nani mmiliki wa majeshi haya. Na haya majeshi yanamiliki nini au nani ni muuzaji wa f-16s, jeshi au Boeing?
nANI MMILIKI WA AMTRAK, USPS ..

Achana na hayo, nani mmiliki wa ARAMCO?, GAZPROM, STATOIL
 
kwa wale wanaopinga philosophy ya mwl ni watoto wadogo ambao hawajitambui. kwani China na urusi ambao ni nchi tajiri duniani wao hawakuendesha uchumi wao kwa kutumia taasisi as serikali na wakafika walipo sasa?

watendaji ndio wanaoiangusha taasisi au nchi.

Nyerere alitimiza wajibu wake na sisi tutimize wetu. Tuache kulaumu laumu kama vile yeye ndio alikuwa akiyauwa mashirika ya uzalishaji mali wakati aliyaanzisha yeye na akatuachia tuyaendeshe tukashindwa.
Tukiorodhesha nchi zilinonufaika na ujamaa basi orofha ni China, Urusi na nyingine chache zizofika 10. Lakini tukiorodhesha nchi zilizonufaika na mifumo ya kipebari orodha ni ndefu sana. Huoni kua ni poor choice kuchagua njia ambayo ni wachache tu walifanikiwa kwa kuipitia??
 
Boss assadsyria3 Nakuomba umwache Marehemu azidi kupumzika kwa Amani. Kashatangulia mbele za Haki, nasi tutafuata. Wewe mwenyewe ume fail mara ngapi toka umezaliwa mpaka dakika hii. Marehemu alikuwa Binadamu pia. Mbona haujatuambia mazuri yake.

My take: Dont fear something you cant control, Fear something you can control.


Nyerere legacy failed 100%.

1. Kuchagua sera za ujamaa lilikua kosa lake kwanza.

2. Kuchukua viwanda, Shule, taasisi na kuzitaifisha lilikua kosa kubwa.

3. Kuanzishwa vijiji vya ujamaa kwa kuwakusanya watu kwa mkono wa chuma was a great mistake. Watu walipoteza mali, wengine kushindwa kucope na mazingira mapya ya kulazimishwa.

4. Kuzuia mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kukosolewa na zikabaki zidimu fikra za mwenyekiti. Here we are.

5. Kutumia rasilimali za nchi kukomboa mataifa mengine bila mkataba wa kurefund izohela baada ya Uhuru. Check Mozambique Na South wanavotufanyia wamesahau tuliyowafanyia so bora tungekuwa kama Marekan hatumii fedha zake katika vita bila return .

6. Kushindwa kuzuia rushwa serikalini na katika mashirika. Mtu anapewa umeneja wa kiwanda au taasisi anaiba anafilisi kisha anahamishwa toka sehemu moja kwenda nyingine. Ilipaswa afikishwe mahakamani na afilisiwe. Hicho ndicho kimeigwa mpaka leo.

7. Alichangia kuendelea kwa katiba inayotuumiza hii leo. Hakuamini nguvu ya upinzani, aliamini katika chama chake pekee. Ilifika anasema rais bora atatoka CCM pekee why?

Tunapaswa kumpima mtu economically kujua alifaulu ama alifeli.

Uchumi wa Tanzania upo chini sana kwasababu ya sera zetu tulizoamua kuingia bila referendum kujua kama watu wanaafiki ama la.

Siamini kama kuna haja hiyo ya kucelebrate life ya Mwl. Katika context ya economy.
 
Hufahamu kuwa Department of Treasury ndiyo inamiliki the Fed. Pia sijakuuliza kuhusu air force one, nimekuuliza nani mmiliki wa majeshi haya. Na haya majeshi yanamiliki nini au nani ni muuzaji wa f-16s, jeshi au Boeing?
nANI MMILIKI WA AMTRAK, USPS ..

Achana na hayo, nani mmiliki wa ARAMCO?, GAZPROM, STATOIL
  • Wacha nikujibu kwa utaratibu.Department of treasury haimiliki wala haipo kwenye utawala wa benki kuu ya marekani (federal reserve bank) bali wao wana print noti zinazotomiwa na benki kuu. Serikali (raisi na congress) wana wateua magavana wa benki hiyo lakini hawaingilii utendaji wake. Hayo hapa ni majibu toka website ya federal reserve bank
  • Who owns the Federal Reserve?The Federal Reserve System is not "owned" by anyone. Although parts of the Federal Reserve System share some characteristics with private-sector entities, the Federal Reserve was established to serve the public interest.
  • Benki kuu kwenye nchi nyingine duniani zinamilikiwa na serikali na serikali ndio mwamuzi wa mwish
  • Kuhusu majeshi ya marekani na vifaa vyake ni kweli vinamilikiwa na serkali kwa 100% kama nchi nyingine duniani, tofauti ni kua vifaa na mitambo ya kijeshi havitengenezwi na jeshi au kampuni za serikali bali wanatoa tenda kwa mikataba maalum na makampuni binafsi kama Boeing, Lockheed Martin n.k
  • Ndege uliyoitolea mfano f-16 zimetengenezwa na makampuni mawili kwa ushirikiano, "Lockheed Martin" na "General Dynamics". Jeshi la marekani lina nunua kutoka kwa hizo kampuni.
N
 
Baba wa Taifa alikuwa mzuri sana mdomoni, mpaka Leo hotuba zake in kiboko. Kiongozi yeyote asiyesikia mawazo ya wengine huwa anashindwa, na ndivyo ilivyotokea.
 
Tukiorodhesha nchi zilinonufaika na ujamaa basi orofha ni China, Urusi na nyingine chache zizofika 10. Lakini tukiorodhesha nchi zilizonufaika na mifumo ya kipebari orodha ni ndefu sana. Huoni kua ni poor choice kuchagua njia ambayo ni wachache tu walifanikiwa kwa kuipitia??

Ni nchi chache sana duniani ambazo hazikupitia mfumo wa ujamaa, ndo ulikuwa ni mfumo uliotumika kwa ajiri ya udhalishaji kabla ya capitalism, ndio maana nasema kuna economic stage hata Europe walizipitia kabla ya kuingia capitalism, sisi kwa sasa kuingia capitalism bila kuwa udhalishaji au viwanda tunabakia kama watazamaji tu, na kuwa MANAMBA katika nchi zetu.
History of socialism - Wikipedia
 
Tukiorodhesha nchi zilinonufaika na ujamaa basi orofha ni China, Urusi na nyingine chache zizofika 10. Lakini tukiorodhesha nchi zilizonufaika na mifumo ya kipebari orodha ni ndefu sana. Huoni kua ni poor choice kuchagua njia ambayo ni wachache tu walifanikiwa kwa kuipitia??

Ni nchi chache sana duniani ambazo hazikupitia mfumo wa ujamaa, ndo ulikuwa ni mfumo uliotumika kwa ajiri ya udhalishaji kabla ya capitalism, ndio maana nasema kuna economic stage hata Europe walizipitia kabla ya kuingia capitalism, sisi kwa sasa kuingia capitalism bila kuwa udhalishaji au viwanda tunabakia kama watazamaji tu, na kuwa MANAMBA au Tegemezi katika nchi zetu.

Hizi mifumo za ujamaa au capitalism zina faida na hasara zake, inategemea na kiongozi na wananchi wanausimamia vipi mfumo husika, hivyo ukisema socialism ni mbaya sio kweli, maana Africa kuna nchi nyingi tu ziko kwenye mfumo wa capitalism toka zinapata uhuru lakini bado ni masikini, 80% ya nchi za kiafrica ni masikini na wote walikuwa capitalism majority.
History of socialism - Wikipedia
 
Ni nchi chache sana duniani ambazo hazikupitia mfumo wa ujamaa, ndo ulikuwa ni mfumo uliotumika kwa ajiri ya udhalishaji kabla ya capitalism, ndio maana nasema kuna economic stage hata Europe walizipitia kabla ya kuingia capitalism, sisi kwa sasa kuingia capitalism bila kuwa udhalishaji au viwanda tunabakia kama watazamaji tu, na kuwa MANAMBA au Tegemezi katika nchi zetu. Hizi mifumo za ujamaa au capitalism zina faida na hasara zake, inategemea na kiongozi na wananchi wanausimamia vipi mfumo husika, hivyo ukisema socialism ni mbaya sio kweli, maana Africa kuna nchi nyingi tu ziko kwenye mfumo wa capitalism toka zinapata uhuru lakini bado ni masikini, 80% ya nchi za kiafrica ni masikini na wote walikuwa capitalism majority.
History of socialism - Wikipedia
Ni kweli lakini sidhani kama ni sahihi kwa sisi kujaribu kufuata kila hatua waliyopitia wenzetu wa ulaya kwasababu mazingira yako tofauti sana na wao walivyo kua wakati wa ujamaa wao. Kuna nchi nyingi tu ambazo punde tu baada ya uhuru hawakufuata sera kijamaa na leo hii wamepiga hatua kubwa sana kimaendeleo pamoja na maliasili chache walizonazo.
 
  • Wacha nikujibu kwa utaratibu.Department of treasury haimiliki wala haipo kwenye utawala wa benki kuu ya marekani (federal reserve bank) bali wao wana print noti zinazotomiwa na benki kuu. Serikali (raisi na congress) wana wateua magavana wa benki hiyo lakini hawaingilii utendaji wake. Hayo hapa ni majibu toka website ya federal reserve bank
  • Who owns the Federal Reserve?The Federal Reserve System is not "owned" by anyone. Although parts of the Federal Reserve System share some characteristics with private-sector entities, the Federal Reserve was established to serve the public interest.
  • Mkuu hata Tanzania, gavana anateuliwa na rais na haingiliwi utendaji wake. Tofauti ni kuwa kila benki mwanachama wa Fed, anatoa asilimia 3 ya mtaji wake. Hiyo asilimia tatu, hawezi kuitoa wala kukopa na kuitumia kama collateral. Hiyo hela baada ya shughuli zote na kuzalisha faida huenda Treasury. Yaani treasury hula faida yote na kuziachia benki asilimia 6 tu ya faida, sometimes less. Sasa niambie nani ni mmilik hapo?Federal Reserve Bank Ownership - FactCheck.org
    Kuhusu majeshi ya marekani na vifaa vyake ni kweli vinamilikiwa na serkali kwa 100% kama nchi nyingine duniani, tofauti ni kua vifaa na mitambo ya kijeshi havitengenezwi na jeshi au kampuni za serikali bali wanatoa tenda kwa mikataba maalum na makampuni binafsi kama Boeing, Lockheed Martin n.k
  • Ndege uliyoitolea mfano f-16 zimetengenezwa na makampuni mawili kwa ushirikiano, "Lockheed Martin" na "General Dynamics". Jeshi la marekani lina nunua kutoka kwa hizo kampuni.
  • Hayo mashirika hutumika kama karakana na kupewa kandarasi na majeshi ya marekani. Lakini technology ni ya majeshi hayo na umiliki upo exclusively kwa majeshi ya marekani. Wakitaka kuuza, lazima serikali imwage wino, na fedha huenda serikalini.
  • Hiyo ni sawa na wewe uwe na kampuni ya kutengeneza saa au simu, uka design kila kitu, halafu ukatenda kutengeneza Guangzhou, bado ni mali yako na faida ni yako wewe as long as umewalipa mafundi na karakana yao.
  • Try to understand, serikali za hizi nchi kubwa zinafanya biashara kubwa sana kuliko unavyoaminishwa.
 
Huwezi ukaona wakati ule wasomi ni wachache? Ujamaa ulikua mzuri sema utekelezaji. Na hakufeli asilimia mia, kwani Hakuna perfect asilimia mia wala imperfect asilimia mia. Amini hakua mbaya asilimia mia, alikua na mazuri yake. Basi badilisha kauli kuhusu Mwalimu kufeli legacy yake asilimia mia
 
  • Hayo mashirika hutumika kama karakana na kupewa kandarasi na majeshi ya marekani. Lakini technology ni ya majeshi hayo na umiliki upo exclusively kwa majeshi ya marekani. Wakitaka kuuza, lazima serikali imwage wino, na fedha huenda serikalini.
  • Hiyo ni sawa na wewe uwe na kampuni ya kutengeneza saa au simu, uka design kila kitu, halafu ukatenda kutengeneza Guangzhou, bado ni mali yako na faida ni yako wewe as long as umewalipa mafundi na karakana yao.
  • Try to understand, serikali za hizi nchi kubwa zinafanya biashara kubwa sana kuliko unavyoaminishwa.
Hapo umeandika vizuri na ndio tofauti inakuja.

Marekani pamoja na kwamba jeshi ndio linalo design hizo mashine na kua mmiliki, lakini wanatoa tenda kwa makumpuni ili watengenezewe, haya makampuni yanaajiri maelfu ya watu na yanaendeshwa kwa faida kubwa kwa sababu yanaendeshwa kibiashara.

Tofauti inakuja Tanzania wakati wa Nyerere viwanda vya uzalishaji vilikua vinamilikiwa na kuendeshwa na serikali. Serikali ilikua haitoi kandarasi ili bidhaa zitengenezwe bali ilikua inatengeneza yenyewe.

Kwahiyo serikali ilikua inafanya biashara kuazia uzalishaji hadi uuzaji, hapo ndipo tatizo linakuja, ni vigumu sana serikali kusimamia biashara kama vile inavyosimamiwa na makampuni ya watu binafsi.
 
Hapo umeandika vizuri na ndio tofauti inakuja.
Marekani pamoja na kwamba jeshi ndio linalo design hizo mashine na kua mmiliki, lakini wanatoa tenda kwa makumpuni ili watengenezewe, haya makampuni yanaajiri maelfu ya watu na yanaendeshwa kwa faida kubwa kwa sababu yanaendeshwa kibiashara.
Tofauti inakuja Tanzania wakati wa Nyerere viwanda vya uzalishaji vilikua vinamilikiwa na kuendeshwa na serikali. Serikali ilikua haitoi kandarasi ili bidhaa zitengenezwe bali ilikua inatengeneza yenyewe. Kwahiyo serikali ilikua inafanya biashara kuazia uzalishaji hadi uuzaji, hapo ndipo tatizo linakuja, ni vigumu sana serikali kusimamia biashara kama vile inavyosimamiwa na makampuni ya watu binafsi.
Unaongeleaje shirika kama la Greencore?
(Hint: Google it)
 
Uzuri wa JF ndio huu. Mara fulani watu huweka mapenzi pembeni na kuanza kuchambua hoja.
 
Nyerere legacy failed 100%.

1. Kuchagua sera za ujamaa lilikua kosa lake kwanza.

2. Kuchukua viwanda, Shule, taasisi na kuzitaifisha lilikua kosa kubwa.

3. Kuanzishwa vijiji vya ujamaa kwa kuwakusanya watu kwa mkono wa chuma was a great mistake. Watu walipoteza mali, wengine kushindwa kucope na mazingira mapya ya kulazimishwa.

4. Kuzuia mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kukosolewa na zikabaki zidimu fikra za mwenyekiti. Here we are.

5. Kutumia rasilimali za nchi kukomboa mataifa mengine bila mkataba wa kurefund izohela baada ya Uhuru. Check Mozambique Na South wanavotufanyia wamesahau tuliyowafanyia so bora tungekuwa kama Marekan hatumii fedha zake katika vita bila return .

6. Kushindwa kuzuia rushwa serikalini na katika mashirika. Mtu anapewa umeneja wa kiwanda au taasisi anaiba anafilisi kisha anahamishwa toka sehemu moja kwenda nyingine. Ilipaswa afikishwe mahakamani na afilisiwe. Hicho ndicho kimeigwa mpaka leo.

7. Alichangia kuendelea kwa katiba inayotuumiza hii leo. Hakuamini nguvu ya upinzani, aliamini katika chama chake pekee. Ilifika anasema rais bora atatoka CCM pekee why?

Tunapaswa kumpima mtu economically kujua alifaulu ama alifeli.

Uchumi wa Tanzania upo chini sana kwasababu ya sera zetu tulizoamua kuingia bila referendum kujua kama watu wanaafiki ama la.

Siamini kama kuna haja hiyo ya kucelebrate life ya Mwl. Katika context ya economy.
Then you are forgetting that your beloved RUKSA buried all the good things created by Nyerere. Do you remember the economic paralysis (1985 - 1995)?

Remember that 70% of the infrastructure we use now was created by Nyerere
 
kwa wale wanaopinga philosophy ya mwl ni watoto wadogo ambao hawajitambui. kwani China na urusi ambao ni nchi tajiri duniani wao hawakuendesha uchumi wao kwa kutumia taasisi as serikali na wakafika walipo sasa?

watendaji ndio wanaoiangusha taasisi au nchi.

Nyerere alitimiza wajibu wake na sisi tutimize wetu. Tuache kulaumu laumu kama vile yeye ndio alikuwa akiyauwa mashirika ya uzalishaji mali wakati aliyaanzisha yeye na akatuachia tuyaendeshe tukashindwa.

Yeye alipewa madaraka yote ya kuteu watu na kutengua, mahakama,polisi wote chini yake. Sasa alikuwa anateua watu wabaya au watu ambao hawana uwezo na wakati hata kama amekosea anarusiwa kubadilisha lakini yeye alichagua kuwaamisha kituo kimoja na kwenda kingine.

Mtu kama huyu huwezi ukamsamehe kama uchumi wa nchi ukiharibika. Lawama zote ni zake, yeye kama kiongozi alifeli wa asilimia kubwa kwenye mambo mengi, kuanzia demokrasia, uchumi, utawala bora na mengineo.
 
Back
Top Bottom