Nyerere's best hotuba.

Nani kapiga dochi?

Ha hahaa you guys mmenikumbusha mbali mno
dochi lilikuwa linaharibu mpira ule wa makaratasi ya nailoni...
ukipiga dochi unasababisha lawama tele....na kama ni gozi
watu wanacheka hadi basi utasikia duh...bonge la dochi..lol
 
Nyerere alikuwa mwanafalsafa na mwanasiasa wakati huohuo. kwangu mimi naona ni kasoro kidogo kwani siasa mara zote huelemea upande mmoja na falsafa husimama kati. hapa unaona akisema kiongozi mzuri atatoka CCM. Kwa upande mmoja alikuwa sahihi kwani CCM wakati huo ilikuwa na nguvu sana na kwamba ni lazima kiongozi mzuri angetoka CCM ama kwa kukiasi nakuingia upinzani au akiwa ndani ya ccm. upande wa pili inaonyesha alikusudia kukipigia debe CCM na hii ilikipa nguvu sana. Wanaopenda kutumia upande mbaya kuhusu nyerere wanaweza lakini ukweli ni kuwa atabaki kuwaNyerere ni important material si kwa tanzania pekee bali kwa dunia nzima.
 
Ha hahaa you guys mmenikumbusha mbali mno
dochi lilikuwa linaharibu mpira ule wa makaratasi ya nailoni...
ukipiga dochi unasababisha lawama tele....na kama ni gozi
watu wanacheka hadi basi utasikia duh...bonge la dochi..lol

Boss ushawahi kufuma mipira wewe?

Unajaza minailoni kibao halafu katikati ukiweka sponji lazima mpira wako udunde kama gozi.
 

"Hapo Nyerere hakukosea"?

Kwa hiyo Mkapa alikuwa kiongozi safi?

Na Kikwete naye ni kiongozi safi?
 
Boss ushawahi kufuma mipira wewe?

Unajaza minailoni kibao halafu katikati ukiweka sponji lazima mpira wako udunde kama gozi.


Mie nilikuwa specialist hapo
na kuna mbinu ya kutengeza mpira unaodunda kabisa
unaijua?
 
Mie nilikuwa specialist hapo
na kuna mbinu ya kutengeza mpira unaodunda kabisa
unaijua?

Naijua...

Unachukua tyubu ya tairi ya baskeli halafu unalikata kwa kipande ambacho si kirefu sana.

Unafunga na kamba upande mmoja. Unajaza upepo hadi inakuwa ya mviringo viringo.

Unafunga kamba na upande wa pili ili upepo usitoke.

Ukishamaliza ndo unaanza sasa. Halafu kuna zile kamba (acha zile za katani)....tulikuwa tunaziita nyuzi....unazjijua?

Basi hizo ndo unafumia sasa. Halafu watu tulikuwa tunafuma kwa patterns kali sana lol
 

aisee
leo nimeamini uswazi umewahi kuishi
hivi vitu adimu mno
sio kila mtu anavijua
mkimaliza mnafunga mtaa au mnaenda uwanjani kabisa kwa mechi lol
 
Dawa ya mtu mwenye malalamiko yasiyo msingi ni ndogo tu. Mpe hizo data anazotaka halafu tuone atazifanyia nini.

Inawezekana serikali imepima ikaona ni sumu tayari ila naona wewe unataka hadi waonje kabisa ndio wajue kama ina madhara.
 
Inawezekana serikali imepima ikaona ni sumu tayari ila naona wewe unataka hadi waonje kabisa ndio wajue kama ina madhara.

Serikali kuogopa sumu ya uamsho ni sawasawa na wewe kuogopa Afro lako mwenyewe litakuzidi uzito na kukudondosha.

Kama kweli serikali inaogopa uamsho basi ni goigoi kuliko tunavyoifikiria.
 
Hapa najiuliza hivi ndani ya akili ya Mwalimu kulikuwa na nini ameleza kwanza kuhusu Rushwa ndani ya serekali yake baadae akaeleza kuwa kama mahitaji ya wananchi hayatopatikana ndani ya CCM watatafuta nje ya CCM, mwisho akaeleza kuwa kiongozi mzuri wa Nchi hatotoka nje ya CCM .kwa mtazamo wangu mwalimu amewachia viongozi wa CCM fomula nzuri ya kujifanyia watakavyo na ndio maana utasikia siku zote wantumia wimbo huo wa mwalimu tena kwa sauti yake kuwa Kiongozi mzuri hatotoka nje ya CCM tunajionea baraka zake .
 

Unadhani kwa nini aliwanyanganya wakatoliki na madhehebu mengine shule akazifanya ziwe za serikali. Kama angeziacha ziwe chini ya makanisa huenda wewe usingekuwa unajua hata kusoma. Wivu hausadii unless unakufanya ujibidiishe, lakini hizo porojo zenu za kwenye vijiwe vya kahawa hazitawafanya muendelee kama wenzenu.
 
Mbona hamkusema kama mnataka na makabila yahesabiwe?

Unataka tuseme? Kuna ugumu gani kusema? Kila kitu kina mwanzo wake. Ujambazi n.k. unaanza na udokozi. Udokozi usipodhibitiwa unaingia wizi ambao pia usipodhibitiwa huleta ujambazi-wizi wa mchana mchana, kama kiinamacho vile.
 
Unataka tuseme? Kuna ugumu gani kusema? Kila kitu kina mwanzo wake. Ujambazi n.k. unaanza na udokozi. Udokozi usipodhibitiwa unaingia wizi ambao pia usipodhibitiwa huleta ujambazi-wizi wa mchana mchana, kama kiinamacho vile.

Si unajua ndugu kuwa mti hauendi ila kwa nyenzo...
Msiposema wanapotezea..ona sasa haitajulikana kamwe Bongo land kuna makabila mangapi yanayo exist!!
 

hii safi sana,mwangu lazima nimfundishe..afu aje kuwa mwana jf..great thinkers
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…