NYERERE DAY: Mwalimu Jr. uko wapi?

Rais jk amekuwa mstari wa mbele kupigana na ufisadi na ndio leo hii linazungumzwa wazi wazi na amepiga hatuwa kubwa kurekebisha hilo na limekuwa likionekana hata kwa mataifa wahisani na wao kukubali kazi yake Rais kuwa ni yakupigiwa mfano katika ulimwengu ingesaidia kama John Malecela angeweza kulieleza hilo kwa wananchi wakati alipokuwa akitowa maoni yake haya Hongera Rais JK kwa msimamo wako imara zidi ya Mafisadi


mkuu spea

kuzungumza waziwazi bila kufanyia kazi hakuna maana hata kidogo na ndio maana wasiojua wanabwatuka na hongera kwa jk!!!!!leo hii kama wanaongelewa na bado wanaendelea kuiba sioni umuhimu wake!!!!natumaini utamshauri aache blaablaaah
Mkuu MAMA MIA nakupa mfano mmoja kuna wakati fulani nilikuwa naongea na muengereza mmoja katika mazungumzo yetu tukagusia maswali ya Afrikana akanambia kuwa nyinyi wafrika mnakuwa na haraka sana na mnavamia mambo na akasemakuwa mabadiliko yoyote yanachukuwa wakati sasa unapokuja kwa Jk amekuwa makini kwa hali iliyojitokeza hivi sasa kwani ikiwa atapuruchuka na kufanya maamuzi tu kuna uwezekano yakatokea matokeo tusiyo yatarajia Rais ni mtu wakupongezwa na atafanikiwa hilo halina shaka na wengi hapa watakuja shanga ni vipi ameweza kuliongoza taifa hili na kulipa ubora wa maisha katika mataifa ya afrika kilakitu kinachukuwa muda na hilo litaoneka pale atakapo maliza kipindi chake cha pili 20015
 
Naunga mkono hoja ya kumpongeza JK kwa kuwa jasiri akamtosa Lowasa kwenye issue ya Richmond. Lakini kwenye issue ya EPA kamwe hawezi kumtosa Rostam kwa sababu zile bilioni 30 za Kagoda ndizo zilizotumika katika kampeni iliyomwingiza madarakani.
Kitakachofanyika mwezi ujao ni kukatafuta kambuzi ama kakondoo ka kafara katakachofikiswa mahakamani na itatolewa taarifa kuwa baadhi ya makampuni yaliyotajwa kwenye EPA zilifanya biashara halali ili kumlinda RA na kuonyesha JK was
serious. Leo tunapomkumbuka Nyerere pia tunakumbuka mambo ya kipuuzi yanayoendelea sasa ambayo wakati wake yasimgepota nafasi. Zidumu fikra za Baba wa Taifa na JK afuate.
 
Wakati huu tunapomkumbuka Mwalimu ni vyema tukarejea zile ambazo hakika zilikuwa fikra zake sahihi. Nukuu zifuatazo kutoka katika kitabu chake cha Binadamu na Maendeleo zinasawiri fikra sahihi za Mwalimu ambazo hatuna budi kuzienzi. Zidumu fikra sahihi za Mwalimu!

...Lakini watu hawaendelezwi; ila watu hujiendeleza wao wenyewe..

...na maendeleo tunayoyataka ni maendeleo ya watu; yaletwe na watu; yaendeleze watu; yawafae watu...

...Narudia tena basi. Uchaguzi si asante, wala si zawadi kwa kazi iliyopita. Usimpe mtu kura kwa sababu ya kazi iliyopita, ikiwa sasa huna imani naye kwa kazi ijayo...

...Ni kiburi cha ovyo mtu kuropoka yale anayoyaona kuwa ya kweli bila ya kujali matatizo yatakayowapata wananchi. Mtu anayepiga makelele 'Moto! Moto!' katika darasa lililojaa watoto anaweza akasababisha vifo vingi zaidi kwa msukumano na wasiwasi kuliko yule ambaye aliuona moto akanyamaza; kwa vyo vyote lazima atasababisha vifo vingi zaidi kuliko yule ambaye atawatoa watoto darasani kwa utaratibu...
 
"And there is in Tanzania a fantastic amount of talk about getting money from outside. Our Government, and different groups of our leaders, never stop thinking about methods of getting finance from abroad. And if we get some money or even if we just get a promise of it, our newspapers, our radio, and our leaders, all advertise the fact in order that every person shall know that salvation is coming, or is on the way. If we receive a gift we announce it, if we receive a loan we announce it, if we get a new factory we announce it – and always loudly. In the same way, when we get a promise of a gift, a loan, or a new industry, we make an announcement of the promise. Even when we have merely started discussions with a foreign government or institution for a gift, a loan, or a new industry, we make an announcement – even though we do not know the outcome of the discussions. Why do we do all this? Because we want people to know that we have started discussions which will bring prosperity" - Mwalimu, 1967
 
Neno Zidumu fikra za Mwalimu JK Nyerere lilitanguliwa na neno
Kidumu ....... Angefufuka leo, angekubali kidumu chama cha Demokrasia na Maendeleo.
 

IMEKUWA kama bahati vile kukuta kwenye mtandao huuhuu mahojiano kati ya Mwalimu na Muulizaji maswali hodari huko Akhera kwa jina la Sirafili.

Bila ya kupoteza wakati 'interview' yenyewe tamu na inayofungua macho na masikio kwelikweli (Audio itawekwa baadaye na Mwnakijiji-kama DHL haijafilisika na wakimfikishia mzigo haraka) ilikuwa kama ifuatavyo:


SIRAFIL: Unaonaje maisha yako hapa Mwelimu Sr.?

MWALIMU: Hakika sina cha kulalamika maana nilifuata takriban amri zote kumi nilizotakiwa kama Nasara kuzifuata. Ila niliyumbishwa na ile njia ya Msalaba tu. Hata hivyo kwa kuwa nilikuwa nikisema mara kwa mara mimi binafsi yangu kuwa Mungu kwetu sote Waislamu na Wakiristo ni mmoja hayo nimeyaacha nyuma. Ila naomba wasiniharibie huko duniani kwa kunitakia utukufu jambo ambalo pamoja na cheo nilichopewa astaghafirulillahi hata siku moja sikuomba.

SIRAFIL: Umesikitika kuiacha dunia?

MWALIMU: Hata kidogo!
Nasikitika tu kuwa walioko huko hawajui kilichoko huku na hasa watakaokuwa viongozi kama mimi ambao hawatawatendea watu wao haki!

SIRAFIL: Bado unadhani Ujamaa ni kitu kinachowezekana huko duniani?

MWALIMU
: Jibu ni ndio na hapana. Ndio kwa sababu lazima wasio nacho wabebwe na wenye nacho. Hapana kwa maana kwamba usawa sio sera ya huku kwa hiyo haiwezi kuwa ya huko duniani pia. Si unaona hapa tunazidiana sana Sirafil. Unaona wale walioko kwenye maghorofa ambayo mfano wake duniani hakuna. Na wale kule ambao sithubutu hata kuangalia. Wale waliokuwa wanyonge na walioonewa au kuteswa au kuuawa kwa kudai haki zao huko duniani ndio matajiri wa huku. Na wale matajiri na viongozi wakubwa wakubwa huku hawafikii hata daraja la ufakiri hapa akhera. Inatisha!

SIRAFIL: Unasemaje kuhusu Azimio la Arusha?

MWALIMU
: Yapo mengi ya kutupwa, lakini kuna mengi pia ya kuyafanyia kazi. Azimio la Zanzibar halikuwa na nia nyengine isipokuwa kuhalalisha viongozi kuwinda na mbwamwitu na kukimbia na sungura. Hilo haliwezekani katu! Kiongozi awe kiongozi. Fulstopu. Akijiingiza kwenye mengine atavuruga mambo tu. Namshukuru sana Mo Ibrahim wa Sudan kwa kuona hili na ninamtakia mafanikio makubwa baada ya kupanda mbegu inayoruhusu wasio waroho, wasio walafi, wasio na uchu wa madaraka kuwa viongozi bora na bado wakatajirika kwa sifa hiyo ya uongozi bora na sio kwa kupora haki na mali za wananchi wao.

SIRAFIL: Ulimuonaje mwanao wa kufikia, yaani, kaka BM katika uongozi wake?

MWALIMU: Kaniangusha sana. Yote niliyomfundisha alisahau. Kaniigiza vibaya, kenda upogo.
Niltaka aprojusi kwanza majeolojisti wetu wenyewe na kisha ashirikiane na Wachina kuchimba dhahabu yetu lakini inaelekea kina Barrick bado wapo duniani na ujanja wao uleule wa kula asilimia 99 na kumuachia mwenye mali asili asilimia moja tu! Au aliridhika na kilo ya dhahabu aliyozawadiwa?

Nilifanya kosa la kutokifanya KISWAHILI lugha ya kufundishia toka nasari hadi Chuo Kikuu sanjari na kuleta walimu toka nje kufundisha lugha za kigeni na hivyo kuwa na Watanzania walioelimika kwa lugha mama yao na wakati huo wanaozivinjari lugha za nje kama mchezo tu. Huku ninaulizwa maswali mengi sanana hakika nina deni ambalo nimeshindwa kulilipa ukizingatia lugha hiyo ilivyonisaidia kuwaunganisha wananchi wangu na kuleta amani na mshikamano nchini. Kama huyu bwana angetupa turufu na kukienzi Kiswahili hivi leo mapungufu yake yote yangekuwa kwenye kaburi la sahau duniani na akhera. Lakini atakufa na kihoro cha kushindwa kufanya mengi ambayo alikuwa na nafasi ya kuyafanya kirahisi tu.

SIRAFIL: Yapo maendeleo makubwa katika mawasiliano nchini mwako hivi leo. Hakuna anayeitegemea tena TTCL. Kuna Televisheni 33 hivi sasa, redio karibu 70 nchi nzima na magazeti 14 ya kila siku na wavuti na blogi kabakaba nchini mwako, unasemaje?

MWALIMU: Je, zinatumika kama vyombo na vifaa vya kuelta maendeleo au vyombo vya kuongeza umasikini, maradhi na ujinga (ikiwa ni pamoja na wizi wa mitihani)?

TEKNOHAMA ni kitu muhimu sana (namsifu yule Mhariri wa magazeti huru ya kwanza kwa kutogoa jina hili) inachukua mahala pa yale niliyosema kama masharti ya maendeleo, yaani, watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Ambayo kama ningeliandika upya kitabu changu ningelisema ili tuendelee leo tunahitjai huduma zinazotumia TEKNOHAMA; biashara inayotumia TEKNOHAMA; watu wenye ubunifu na wajasiramali , wasio na ubinafsi wala ulafi, ambao wanaojali usafi, taratibu nzuri na wanaojenga mahusiano mazuri katika jamii; ardhi inayolimwa kisasa na kitaalamu; ardhi inayochimbwa madini yanayosaidia kuondoa umasikini wa Mtanzania; ardhi yenye wanyama wanaochangia biashara kubwa ya UTALII isiyo haribu maadili, utamaduni na utu wetu; siasa zinazoruhusu watu kutajirika lakini wakati huohuo masikini kutoachiwa kufa njaa au kukosa paa au kukosa huduma za afya au kukosa elimu au kukosa mahitaji yote ya msingi; na uongozi unaotambua kwamba una kazi moja tu nayo ni kuongoza na sio kujilimbikizia mali na kwamba familia na watoto wao ni Watanzania wote na sio wale waliowaoa au walioolewa nao au waliowazaa.

SIRAFIL: Unasemaje kuhusu migodi ya DHAHABU waliyopewa watani zako kwa bei sawa na bure!

MWALIMU: Wizi wa mchana! Angalia na laana niliyoiacha, je, huoni mfumo mzima wa Ubepari uko mashakani. Ubepari sio siasa itakayohimili vishindo duniani. Kwa sababu unalea sana ubinafsi na ulafi. Mimi sikukataa watu wasitajirike nilikataa ubinafsi na ulafi. Na huku nimejifunza tatizo kubwa huko duniani ni hili na wala sio jingine.

Ninatamani wangelijua kwamba kwa kuongeza royalty kidgo tu pasingekuwa na haja ya bodi za mikopo kwa wanafunzi wala bima za afya ambako wajanja wanaiba zaidi kuliko wanaohitaji huduma hizo wanavyofaidi.

Bado Tanzania ina madini na rasilimali mali asili za kutosha watoto wake wote kusoma bure; kutibiwa bure; na kupatiwa nyenzo za kuanza maisha kwa gharama sawa na bure.

Mnafuata ushauri wa IMF? World Bank? Hivi mbona hawakuwashauri wakina Gordon Brown na George Bush? Na wenzao wa Euro O-zone?

SIRAFIL: Chama chako kiliwaahidi Waislamu kuabudu kwa mujibu wa dini yao. Na ilani ya chama si uliiona kabla hujaja huku? Si iliahidi kuwarudisha Kadhi wao uliyewapokonya bila sababu za msingi? Vipi bado wanapiga danadana na wewe ulishawaambia kwamba kadhi ni haki yao uliyowadhulumu ?

MWALIMU: Ninashangaa hata mimi. Ahadi ni deni! Niliusimamisha Ukadhi ili tujenge umoja kama nilivyosimamisha kuwepo vyama vingi wakati ule au ushirika uliotishia nguvu za serikali. Sababu ya kuvunja umoja sasa hamna. Watakaovunja umoja ni mafisadi, viongozi wasiokuwa na uwezo wa kuongoza, madikteta uchwara, na wale wanaopayuka payuka ovyo bila kuwa 'sensitive' kwa tofauti zetu za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Aidha kwa chama kukosa sera na viongozi bora, wakweli na safi kama ilivyo huko Afrika Kusini, Zimbabwe na Kenya leo.

Kadhi ni haki ya Waislamu. Na fikira za kipumbavu za baadhi ya watu fulani fulani -kuwa hawa jamaa watapiga watu mawe (kwani yule Mchungaji aliyekampenia DP kule Tarime alipigwa mawe na Waislamu?) , watawachinja watu, watafanya ubaya huu na ule-huu ni unafiki mtupu.

Tatizo ni viongozi wa dini ambazo zina viongozi wanaojilimbikizia mali kutoka kwa waumini wao kuona wivu kwamba na viongozi wa Waislamu nao wanaweza kuneemeka na kuondokana na umasikini na hivyo kuifanya kazi yao pengine vizuri kulikowao wanavyofanya za kwao sasa. Kashfa za ngono, wizi na uporaji makanisani vinawafanya viongozi hao wa dini nyingine pia kutumia 'ukadhi' ili kuficha vitendo viovu vinavyoendelea katika makanisa kadhaa humu nchini bila waumini kujua hili wala lile!

Hivi hawa maaskofu wanaotaka kumfundisha Rais jinsi ya kufanya kazi zake kweli wao watakubali Rais aanze kuwafundisha jinsi ya kufanya kazi zao.

Hawa maaskofu vijana vipi hawa. Wanafanya inductive au deductive reasoning kweli? Mbona naona kama wanaishia kwenye 'fallacies' na kukontradikti hata 'basic tenets' za dini achilia mbali kugombanisha watu na katiba ya nchi ambayo waziwazi inaruhusu watu kupraktisi dini yao kwa mujibu wa sheria na kanuni zao na sio vinginevyo, ikiwemo, Waislamu kuwa na haki ya kufuata sheria zilizoko kwenye kitabu chao kitakatifu!

Kwanini Askofu akosee kwa kusema Mahakama ya Kazi inataka kuanzishwa na sio kurejeshwa? Haoni tofauti ya hili?

Je, maendeleo ya Waislamu sio maendeleo ya Watanzania. Hayo mambo muhimu wanayozungumzia wao ni yapi wakati imeandikwa: ' Pata ufalme wa Mungu kwanza, na mengine yatafuatia!' Au hapo mabwana hawa walisinzia?

Katika dhambi Mwenyezi Mungu anazozichukia zaidi ni dhambi ya UNAFIKI. Viongozi wa dini kwa kweli kama wanataka umoja na amani ya Tanzania iendelee kuwepo ni lazima wawe mbali kabisa na laana hii ya UNAFIKI-yaani kusema uongo ukijua fika unasema uongo; au kuwa na tadi na inda na kumhini anayestahili kupata kitu fulani, kitu ambacho wewe ukipewa pia hutakataa! Na ukijua fika hicho kitamfaa, na hakina balaa kwa wengine!

Aidha, huu ni wakati muafaka wa kunufaika na fedha za IOC kwani nchi za magharibi zimechacha ile mbaya na Vatican au Wajerumani hawawezi kusaidia wananchi wote wa Afrika.


SIRAFIL: Kada wako mmoja kawa swahiba sana wa Marekani na kiongozi wao wa sasa Bwana Kichaka. Unaonaje hili?

MWALIMU: Kapotea! Kapotea sana. Nilimwachia wasia BM-akae mbali na watu hawa kama ukoma. Ni wanafiki wakubwa. Wakikuahidi hutakaa ukipate. Utakufa hujakiona ulichoahidiwa. Hivi hana habari kuwa ni China ndio inayoununua makampuni ya Kimarekani na 'treasury bonds' karibu asilimia 50 za Federal Bank yao. Lakini hili ndio tatizo la vijana virongozi wetu wa Kiafrika. Wanatarajia watu wao wawe wajasiriamali na wagunduzi wa mambo na njia mpya za kutajirika na kutajirisha nchi lakini wao wenyewe hawana chembe ya 'entrepreneurhsip' wala ' intrapreneurship'! Kisha mtu anafanya makosa ya kuzungukwa na watu ambao ni hovyo kuliko hata yeye mwenyewe. Wao sikuzote ni watu wa KUTUMIA lakini hawavuti hatua nyuma hata siku moja kuwaza na kuwazua jinsi ya kuongeza uzalishaji mali na pato la taifa.Bila shaka kazungukwa na watu ambao hawana ushauri wowote wa maana wa kumpa. Angalia hii hotuba yake ya leo Oktoba 14, 2008. Hotuba yote ni kulalamika tu hana la kuwatia watu matumaini. Ni kama vile Watanzania na ninasikia, anasimamia piaAfrika siku hizi hawana wanachoweza kufanya wao wenyewe. Mimi wakati wangu Bwana nisingewaachia BOT peke yao wafanye upembuzi yakinifu na kuja na mikakati juu ya majibu sahihi kwa hili. Ningeleta jopo la watu toka kila kona ya nchi na dunia nzima ili nitoke na kitabu juu ya: ' Mikakati ya Kuhimili Tufani la Fedha na Uchumi katika Dunia ya Utandawazi' ! Na yote haya ningekuwa nimeyasikia wakati wa mazungumzo na waalikwa mbalimbali. Kijana ajaribu hili. Mimi ninadhani vijana wamekuwa sasa. Wasiwategemee sana wazungu. Wana mengi ya kujifunza toka kwa Wajapani, Wachina, Wahindi,Waarabu, Ulaya Mashariki, Wabrazili, Warussi na Wakorea ambao wameshaonja makali ya 'Credit crunsh sometime back' !

SIRAFIL: Umesikia sakata la EPA ?

MWALIMU: Kuna kazi unaweza ukawaachia watu wengine wafanye mwanzo hadi mwisho. Lakini kuna zingine lazima uzifanye mwenyewe au uziidhinishe peke yako. Kisha lazima mtu kutenganisha kati ya undugu na urafiki kwa upande mmoja na kazi kwa upande mwingine. Urafiki huharibu sana kazi! Heri mweke rafiki pembeni umlipe mshahara kila mwezi lakini mambo yako yawe safi. Hili naona kwa hakika mwenzetu linamshinda mshinda vile! Kwa mengine anajitahidi kwa kweli. Lakini ili uwe safi lazima uzungukwe na watu safi-kuanzia nyumbani, katani, jimboni, chamani, Ikulu hadi barazani.

Tatizo kama ni Chama mimi sikuibia serikali kukipa chama. Labda kwa kuwa wakati ule tulikuwa hatuna vyama vingi.
Ukishawafundishia watu tabia ya kudokoa dokoa vya wengine ujue lazima watakudokolea na wewe mwenyewe. Sasa hivi kuna vijana wenye BCom, BBA, MBA -kwanini chama kisijizatiti na kuanzisha upya miradi yake ili iache kupokea asilimia 10 toka kwa wanaoiibia serikali?

Badala ya kumiliki moja kwa moja waanzishe mifuko ya pamoja ya kuwawezesha makada wenye uwezo wa kibiashara aidha mmoja mmoja au katika vikundi katika ubia wa asilimia 60:40 hivi ili chama kiweze kuvuna kinapowekeza na sio kuiba toka hazina!

SIRAFIL: Mradi wako wa NYUMBU hukumuachia mtu urithi?

MWALIMU: Amiri Jeshi Mkuu! Labda kasahau hili. Awaulize rafiki zake Wamarekani jinsi jeshi lilivyogundua na kuanzisha mambo mengi ambayo ni biashara kubwa sana duniani leo. Mrahaba au mrabaha? uongezwe ili jeshi liwe na kitengo cha 'Research and Development ' ili sasa vitu vyote vya msingi vinavyohitajika kutengeneza barabara, reli, mabomba,pampu za maji, majenereta makubwa kwa madogo, mitambo ya hiki na kile ikiwemo ya redio zinazochipua kama uyoga nchini, madaraja na kadhalika viwe vinatengenezwa nchini.
Nilitaka sana kulizungumza hili kabla ya kuja huku lakini ndio tena Ziraili akaniharakisha mno!

SIRAFIL: Unasemaje kuhusu Madaraka Mikoani?

MWALIMU: Ah, nilidhani mwanangu! Kwa hayo, msimamo wangu ni pale pale. Hata Rais akiwa na dege lake mwenyewe na anaweza akaruka toka Mbeya hadi Tanga kwa dakika tano. Bado. Wapeni watu uhuru wa kuamua juu ya masuala yao ya maendeleo ya kiuchumi na jamii.

Mtu wa aja leo, aondoka kesho atakusaidianiii bwanaee! Angalia Tanga, kama mkoa ulivyodumaa, lakini fursa kadhaa zipo za mkoa kuonesha maajabu! Mwataka jenga bandari Bagamoyo, mbona ya Tanga hamjaipanua? Waishia kuiba magari toka Zanzibar kwa majahazi na kuwatajirisha askari walioamia kando ya bahari za Tanga sikuzhizi enhe!!! Au ndio mitihani mnayowapa watu wangu sasa?

Vinginevyo tofauti inavyozidi kati ya mkoa na mkoa itazua mitafaruku itakayowasambaratisha kama Urusi. Na mwishowe kwani wameishia wapi. Hawaoni hawa jamaa kweli?

SIRAFIL: Mwanahalisi, hizi ni habari za karibuni limefungiwa miezi mitatu. Unasemaje?

MWALIMU: Hivi ule ujinga wa serikali kuwa mshtaki, wazee wa baraza, mwendesha mashtaka na jaji bado upo nchini kwetu?

Na wizara ambayo kazi yake ni kufungia tu magazeti ipo? Na waziri wake anajihesabu ni waziri? Au wananchi wameshindwa kuwafundisha viongozi wao ni wizara zipi zinazohitajika. Na fedha yao ya kodi itumike vipi? Shauri yao kama hawajui kuna nchi zina tawaliwa na mijambazi, zinaitwa Kleptocracy. Isije fikia na nchi yetu inatawaliwa na mawaziri na wabunge wanaolipwa mishahara lakini hawana wanachokifanya au hawana kazi unayoweza kuwauliza leo wamfanyani eti? Hatari sana watu wangu wakielekea huko.

Katika miaka hii ni muhimu nchi iwe na MAADILI kwa watu wote. Na kiongozi awe yule anayeishi kwa kufuata na pengine kupiku maadili yote hayo. Kiongozi asiwe juu ya sheria. Tutajuaje kama sio tapeli, kama ndugu zake hawatudhulumu, kama mke au wake zake hawana biashara zisizoelweka, kama watoto wake hawapendelewi na yeye mwenyewe au na watu wanaomzunguka? Kwamba hakuna uovu na dhambi za kutisha zinazofichwa? Na jamaa kasoma hiyo ' FOIA' baada ya kukabidhiwa au kwa uvivu wa viongozi wangu kama nilivyowajua ndio kaenda kubwaga mahala ambako hata hapakumbuki. Angelisoma, hivi angelikuwa na pupa ya namna hii. Au anataka kujipendekeza zaidi ya hapo kweli ....? Si ndio uwezo wake wa juu kabisa? Na hata kauli zake zaonesha hili. Ni vyema viongozi Tanzania wakajua kuwa kuna Watanzania wenye akili, utajiri na takwa mara mia zaidi yao lakini wanaishi kwa kumhofu muumba wao na hawajioneshi katu hadi wanapolazimishwa saaaana! Ukimuona Waziri, Mkuu wa Mkoa, Katibu Mkuu, Mkuu wa wilaya au Mbunge anajisikia na kujiona mkubwa. Keshafika.Hamna kitu hapo. Bomu hilo. Lingoje tu kuteguliwa na kutupwa jalalani uchaguzi ujao! Kiongozi kama nilivyojifunza mimi ni unyenyekevu na kuwatumikia watu. Mtu mwenye ujibari na kutaka kutumikiwa huyo ni mfalme au sultani. Na sijui kama tunawahitaji kwa kweli katika miaka hii? Na hawa ndio pia wenye ile dhambi ya kutaka kujilimbikizia na kujilimbikizia mpaka kama yuel bwana aliyeona pilau kwa mara ya kwanza, anakula na kuzidisha mno na kisha tumbo kupasuka....

Si mmeona walafi wakupindikua na yaliyowakuta au?

Mliona nilivyowalea kina Mag, Roz, Mada na wale wa kufikia sio? Mimi huku silaumiwi kwa kuwapa wanangu haki kuliko haki niliyowapa watoto wote wa Tanzania. Yaani watoto wa Tanzania walifaidi kuliko wangu binafsi walivyofaidi. Uongo?

Hili Sirafil ni tatizo la kumpa mtu Uwaziri kwa sababu za fadhila badala ya uwezo wake. Anaishia kukuabudu badala ya kuwatumikia wananchi. Ni msiba mkubwa sana katika nchi yoyote ile duniani. Nimejenga misingi mizuri. Ningelipenda viongozi wote baada yangu wasikubali kuogopwa au kuabudiwa au kutetemekewa. Maana waoga, wanaoabudu na wanaotetemeka wakikuona au kukusikia tu-aghalabu ni wababaishaji wa kutupwa!

Huyu bwana hajui kwamba kuna Baraza la Habari -ina maana kalidharau? Sikuacha Tanzania Editors Forum (TEF) -kwanini wasiachiwe kumuonya Mhariri mwenzao? Na wao sio kukurupuka tu bali baada ya kuangalia ukweli na haki iko wapi? Mwanzo wa kumuogopa mkuu wa nchi ndio mwanzo wa kukaribisha udikteta wa kishenzi kama ule wa Zimbabwe eti! Watanzania nimewalea uzuri sana wanajua kwanini nilikuwa na kaudikteta wakati ule; lakini siamini kama watamvulia yeyote yule anayetaka kuwa dikteta kwa dakika hata moja- awe katibu kata, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, waziri au hata rais wa muungano au wa Visiwani!


SIRAFIL: (Baada ya kusikiliza simu ya mkononi). Alikuwa Jibrili. Ananiambia CHADEMA imeshinda ubunge na udiwani Tarime.

MWALIMU: Sishangai. Hiki si kile chama cha Waziri wangu wa zamani wa Fedha, Edwin? Na kimechukuliwa na mtoto wa rafiki yangu mpenzi, yule Mzee kwenye bustani njema ya ghorofa ile pale.....Ndio chama pekee kinachoweza kuongoza Tanzania ukitoa CCM-A na CCM -B.

Chama changu hakina tena mtu kama Nnauye, Kingunge-walinisaidia sana kuandika andika sera hawa. Sasa ukiweka mtoto wa mjini kuwa Katibu Mkuu wa chama unatarajia nini.
Ninashangaa kwamba chama kimeshindwa kuwapata vijana wazuri kushika nafasi nyeti za chama na badala yake wanalazimika kukimbilia kwenye upinzani au kwenye biashara zisizo na kichwa wala miguu huku tunaachia makapi k uongoza chama. Na chama sasa kimejenga tabia ya kuwakatisha tamaa na kuwafukuza watu wazuri na badala yake ndio hivyo wana pumba tu, kufikia tunaitwa CHAMA CHA MAFISADI na hakuna anayeweza kutoa jibu la kuua na kumaliza kabisa tuhuma kama hii!

Ningelikuwepo duniani ningeliwaandikia CHADEMA kitabu juu ya : 'MIKAKATI ya kupambana na CHAMA TAWALA na kujenga demokrasia ya kweli !'

........na wakati huo huo ningelimuomba yule mwandishi wa BLOGI ya DEMOKRASIA ambayo sijui hata kam CCM wameisoma kuandika kitabu cha kukishauri chama changu jinsi ya: ' CHAMA: MIKAKATI YA KUZALIWA UPYA: Katiba Mpya na Demokrasia Kamili kwa uhai wa CCM!'

Washauri wao wanawadanganya eti kuendelea na Katiba viraka ndio CCM itaendelea kuwepo. La hasha. Katiba ya sasa na tabia zote mbaya za kuutafuta na kuuwekea mikwara upinzani ndio unaochimba haraka kaburi la chama changu. Laiti wangelijua?

Hivi vyama vingine vya njaa kali haviwafai kabisa Watanzania. Hawa ni matapeli kama matapeli wa aina nyingine tu. Ukiwa na padri anayeacha kazi yake ya uchungaji na anakwenda kueneza siasa inayopingana na amri kumi za Muumba unategemea nini? Anakejeliwa hadi na TV ya taifa na haoni wala hasikii? Hakuna laana mbaya kwa mchungaji kama ile ya kuwa mnafiki na nusu hayawani!Unapokuwa na chama cha kina nanihino unategemea kuna baraka za Muumba hapo kweli?

SIRAFIL: TBC imerudi. Unaonaje hili?

MWALIMU: Kweli. Kwanini haikuwa AFRICAN BROADCASTING CORPORATION. Afrika inahitaji Kiswahili sasa kuliko wakati wowote mwingine huko nyumba. Mkinirihusu nitawaambia hili. Ya nyumbani sawa iwe TBC lakini ile ya nje, yaani, redio, TV na internet ziwe ni ABC!

SIRAFIL: Una habari madaraja ya Rufiji na Msumbiji yameshajengwa?

MWALIMU: Daa! Kwa hiyo sina deni tena duniani? Allahamdulillahi. Basi kawaambie Wachagga haraka waende Lindi na Mtwara... ... wakifika hapo tutajenga kusini bila wasiwasi! Aikaeli unasemaje?

SIRAFIL: Unamshauri nini Rais wa sasa kuhusu Kabila na Kongo?

MWALIMU: Unajua ukiacha shamba la mwenzako linavamiwa tu na magugu na wewe unakaa kimya huku jirani zako wengine wakimhinikiza muacha magugu ang'oee magugu japo hawana sauti na uwezo kama wewe unajipalia mkaa hata kabla jua halijatoka.

Askari waliopelekwa na UN huko Kongo ni wakora na watu wanaotafuta maisha na maslahi binafsi tu kwa kujitajirisha na utajiri wa masikini wa Kongo.

Hivi hauoni kuna upofu hapa. Eti Mugabe atume jeshi Tanzania isitume na ni Tanzania inayotishiwa na magugu ya Mashariki ya Kongo?

Vikosi vya magharibi vinatosha kabisa kuleta amani ya kudumu Kongo Mashariki na hivyo kuhakikisha amani Tanzania kwa miaka mingi ijayo. Vinginevyo, vita Tanzania vitaanzia magharibi ya nchi hiyo na vitaletwa na wageni na wala sio wazawa!

SIRAFIL: Hesabu zinaonesha sio tu Watanzania wanalipwa mishahara isiyokidhi mahitaji yao ya msingi bali pia malipo yao yancheleweshwa, yanakatwa ndivyo sivyo na mashirika ya hifadhi na bima yanawadhulumu ziada katika mapato yao yanayowekezwa kwenye mambo mbalimbali. Unasemaje kuhusu hili?

MWALIMU: Ni kweli. Hii ni miaka ya utandawazi na kama tunataka kuumuka haraka na sio kujiweka kwenye mafungu ya umasikini sikuzote lazima tukubali kuwa na wafanyakazi kutoka popote pale duniani wanaolipwa vizuri lakini sio vizuri kuliko wazawa au wenyeji wenyewe. Waende nchi za Uarabuni zilizoendelea wakajifunze hili!


[ Nina hakika nikiipitisha hii kwa Mwalimu Jr. basi itasambaa dunia nzima. Na ingawa haya yamo kama kejeli lakini vionozi wan chi hii wakiyachambua ndani nje watainusuru nchi hii wakati huu wa mashaka na giza Tanzania!-Ideas.Unlimited}
 
"And there is in Tanzania a fantastic amount of talk about getting money from outside. Our Government, and different groups of our leaders, never stop thinking about methods of getting finance from abroad. And if we get some money or even if we just get a promise of it, our newspapers, our radio, and our leaders, all advertise the fact in order that every person shall know that salvation is coming, or is on the way. If we receive a gift we announce it, if we receive a loan we announce it, if we get a new factory we announce it – and always loudly. In the same way, when we get a promise of a gift, a loan, or a new industry, we make an announcement of the promise. Even when we have merely started discussions with a foreign government or institution for a gift, a loan, or a new industry, we make an announcement – even though we do not know the outcome of the discussions. Why do we do all this? Because we want people to know that we have started discussions which will bring prosperity” - Mwalimu, 1967

Dogo:

Hayo yote aliyaona lakini mwenyewe alikuwa specialist wa kuomba. Msemo wa waChina KUJUA NA KUTOFANYIA UNACHOJUA NI KUTOJUA KAMILI.
 
Kama kuna utakatifu ambao Nyerere angeliukubali sio huu wa kutangazwa na Kanisa ambalo kwa hivi sasa linaendeshwa kwa uongo, fitina, ujanja, ubabaishaji na wizi.

Kumbukeni enzi Maaskofu kama Sangu, Moshi, Nyaronga,Babu yangu Stefano, Baba Askofu wa Mbulu na vitu walivyovifanya katika nchi hii tena wakati mgumu wa chama kimoja. Nenda Iringa ukaone RUICO inavyoendeshwa; nenda St. Augustine, Mwanza, nenda Kilimanjaro, nenda Arusha, nenda Peramiho utasikitishwa jinsi uongozi mzuri ulivyopotea ghafla katika kanisa.

Kwa hiyo utakatfu wa kwanza uwe ule wa safu ya viongozi wa kanisa kujisafisha. Hawawezi kuendelea kutegemea kuwepo kwa waumini wasiohoji hiki au kile. Wao watashtukia tu sisi vijana tumehama na makanisani wanaenda wazee na watoto kama ilivyo Ulaya. Viongozi wa kanisa kuweni wakweli, acheni ubinafsi, acheni uroho na acheni kuchonganisha dini moja na nyingine kama kweli mnatutakia mazuri sisi Watanzania. Hivi sasa kanisa Tanzania linaelekea kuwa na tabia kama ya Kanisa lilivyokuwa Rwanda kabla ya Genodidee.

Lakini kuna maaskofu safi Zimbabwe, Phillipines, Bolivia, Venezuela, Kongo na nchi kama hizo. Mbona msiende kujifunza huko?

Kanisa na viongozi wa kanisa wakifanya hayo hapo juu tayari watakuwa wamempa Baba wa Taifa utakatifu ambao sio tu unakubalika hapa duniani bali pia mbinguni.

Haiwezekani watu amabo wameshndwa kuonesha ucha-Mungu wa kweli, haki, maadili ya hali ya juu na upendo kwa wote bila kujali wana imani yao au la kuwa ndio wanaofaa kumtawaza mtu ambaye kila aliye hai hapa Tanzania anajua afanywe au asifanywe MTAKATIFU yeye alishakuwa kwa vitendo vyake mwenyewe juu ya binadamu wa kawaida. Na Mwenyezi Mungu akamsafisha kabisa kwa kumpa ugonjwa hadi umauti wake ii asichafuliwe na dhambi nyingine tena hapa duniani. Nyerere tayari ni mtakatifu teena yuko kwenye daraja la juu sana peponi, na sisi hatuhitaji wanafiki kujidai wanamfanya mtakatifu hapa duniani.

Jisafisheni kwanza, mrudieni Mungu ili muwe na sauti ya kuwakemea viongozi na wananchi nao wakawasikilizeni! Na mwanzo mwema ni kutokubali kuyumbishwa na sera za Marekani na Wayahudi ambao kwa sababu wanazozijua wanataka kuwatenganisha wajukuu wa Ibrahim, yaani, Waislamu na Wakiriisto. Penda tusipende sisi ni ndugu katika vitabu vitakatifu, na itakuwa hivyo mpaka mwisho wa dunia. Kwanini tunashinwa kuwa na akili ya kuishi pamoja na kusaidia. Asijidanganye mtu akadhani sisi Wakiristo au wale Waislamu wanaweza kuwafanya watu wote duniani kuwa watu wa dini yao. Hilo haliwezekani ng'oo!

Twendeni India, Uchina, Russia na iliyo kuwa Ulaya ya Mashariki sote TUKAVUNE hao waliokuwa kabla ya sasa wakiamini kuwa hakuna Mungu na kwamba dini ni bangi tu! Au mnasemaje? Na hapa nyumbani tufanze hivi; LIVE AND LET LIVE!


Mjukuu wa Mtakatifu wa kweli,
Tanzania
 
Imetolewa mara ya mwisho: 15.10.2008 0001 EAT

• Mdahalo wa Nyerere UDSM mh!

Na Reuben Kagaruki
Majira

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na wasomi wengine, wameulaumu uongozi wa chuo hicho kwa kushindwa kuandaa mdahalo maalumu kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka tisa ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Wakizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi wa mikutano wa Nkurumah, chuoni hapo Dar es Salaam jana, baadhi ya wanafunzi walisema walifika asubuhi kushiriki mdahalo huo, lakini wakakuta ukumbi umefungwa na hakukuwa na maelekezo yoyote.

Mbunge wa Serikali ya Wanafunzi UDSM (DARUSO), Bw. Owawa Stephen, alisema kitendo hicho kimedhihirisha jinsi viongozi wa chuo hicho walivyoanza kumsahau Mwalimu Nyerere.

"Hii imedhihirisha kuwa chuo kinaelekea upande wa mabepari ndiyo maana wanaona hakuna umuhimu wa kumuenzi Nyerere," alisema Bw. Stephen na kuongeza kuwa inawezekana uongozi wa chuo hicho umeogopa kuandaa mdahalo huo kwa kuhofia hoja ambazo zingetolewa kutokana na vitendo vinavyoendelea nchini ambavyo Mwalimu alivikemea.

Mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Bw. Cosmas Makune, alisema ni aibu kwa wasomi kushindwa kumuenzi Mwalimu Nyerere katika kipindi hiki ambacho vitendo vya kifisadi vimekithiri.

"Leo wanatuzuia sisi wasomi, tunaosoma kwa kodi za wananchi tusipaze sauti zetu na kuongelea yanayoendelea nchini," alilalamika Bw. Makune na kuongeza kuwa mdahalo huo kama ungefanyika ungekuwa na maslahi makubwa kwa Taifa.

"Ni jambo la kushangaza kuona maprofesa wanaogopa hata kutoa nafasi kwa wanafunzi kutoa mawazo yao...hawa ni maprofesa gani wasioonesha vitendo?," alihoji Bw. Makune.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Kitivo cha Siasa za Sayansi (DUPSA), Bi Elizabeth Maginga, alisema viongozi wa chuo hicho wameanza kuzuia fikra za wasomi na imedhihirisha kuwa hawatambuliwi.

"Ni jambo la kushangaza, siku ambayo ni muhimu kuongelea masuala ya msingi, ukumbi unafungwa, wanachokifanya ni kutulazimisha tuanze kumsahau Mwalimu Nyerere," alisema.

Aliongeza kuwa yanayotokea sasa ndiyo ambayo Mwalimu Nyerere aliyapinga.

"Wamekimbia, wamejua mjadala utatoa changamoto nzito," alisema Bi Elizabeth na kuongeza kuwa DUPSA ilikuwa na mpango wa kuandaa mdahalo huo, lakini uongozi uliahidi kufanya hivyo, ahadi ambayo haikutekelezwa.

Katika mbao hakukuwa na matangazo yoyote yaliyoeleza chochote kuhusiana na jinsi wasomi watakavyomuenzi Mwalimu Nyerere.

Majira ilifika kwenye ofisi za baadhi ya viongozi wa chuo hicho kupata ufafanuzi, lakini wote hawakuwa chuoni hapo.

Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rweikaza Mukandala naye alipotafutwa kwa njia ya simu, haikuwa hewani.
 
Wadau Kuna Makala imetoka ktk Gazeti la English...lkn pia imetoka Nusunusu..

Unaweza kuipata hapa...Endelea..

It is a pity that Mwalimu Julius Nyerere did not reveal much of his early life in Dar es Salaam of 1950s of which he came to as a budding young politician fresh from Edinburgh University aged about 30 years old. Why Mwalimu Nyerere was secretive about his early days during the transformation of Tanganyika African Association (TAA) to Tanganyika African National Union (TANU) is now a rhetoric question because we can only speculate. Was Mwalimu trying to conceal something on his past or was that an innocent omission? The only time Mwalimu walked down memory lane was in 1985 at the Diamond Jubilee Hall where in an emotional farewell speech before he stepped down from the presidency he addressed Elders of Dar es Salaam who supported him during the struggle for independence. In that memorable speech flavored with Mwalimu’s oratory skills he walked back into history and paid tribute to Wazee wa Dar es Salaam (Dar es Salaam Elders) who supported him from day one since the founding of TANU in 1954. In his revelations Mwalimu Nyerere for the first time in public mentioned two other patriots forgotten in the history of Tanganyika. He said that in those difficult days the other young men with him were Abdulwahid Sykes and Dossa Aziz. Abdulwahid was TAA president in 1953 and was among the the four financiers of the movement along with his young brother Ally, Dossa and John Rupia. Abdulwahid died young in 1968 but Dossa went on to old age but both of them died the fruits of independence of which they had worked so hard having passed them by their names hardly associated with TANU, Nyerere or the independence movement. Dossa died a poor and lonely man at Mlandizi in 1997. One can write passages and passages on contributions and sacrifices made by the two Sykes brothers – Abdulwahid and Ally and Dossa; and the elders like - Mwinjuma Mwinyikambi, Kiyate Mshume, Jumbe Tambaza, Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir to mention only a few. In those days these names made up ‘who is who’ of the municipality. These were the rich and the famous of the town. But to understand the town, its elite and politics one has to revisit how colonialists demarcated Dar es Salaam.

....download a file...
 
samahani wakuu Makala hio imetolewa na mwandishi wa Historia ya Tanzania, Mohd Said....ilitolewa Jana/Juzi...The East African lakini imehaririwa hadi ikachujuka.....Muziki wenyewe halisi ndio huu.
 
nimefanikiwa kuliweka hilo file...lengo langu halikuwa kuongeza posts ....ila net ilikuwa inakata viuno!!!
 

Attachments

  • TRACING THE FOOTSTEPS OF MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE 2.pdf
    146.4 KB · Views: 168

Wanasiasa wote wanafiki lakini unafiki huzidiana. Ila kwa hakika
chama tawala nijinafiki babu K!

Tuachilie hayo mbali. Umeniuliza tumuenzi vipi hayati Baba wa Taifa
katika siku au wiki kama moja hivi ijayo.

Yapo mengi Huduma ya kumuenzi baba wa Taifa. Na baadhi yake:

i) Kwanza ni CCM kukiri kwa ulimi na moyo kuwa wanaipeleka pabaya
nchi ambayo kama Mzee angelikuwa hai leo isingediriki kufuata njia
hiyo.
ii. Pili chama hicho kiengue watu waliopewa nyadhifa ambazo
hawaziwezi na ama wanamshauri mwenyekiti au chama vibaya.
iii. CCM isifisadi tu na kupeleka kwenye matumbo yao bali pia
wawekeze kwenye Nyerere Foundation sasa walijitia unafiki wa nini
kama hawawezi kuisadia. Eti na kila anayeula anataka naye akiondoka
madarakani aanzishiwe Foundation yake. Hivi kweli wote nyie, ila
Mwinyi, hamjui kuwa mnajifananisha na mlima na nyie ni vichuguu.
Kweli hamu inaweza kuwepo moyoni ya kumpiku lakini hamna mlilolifanya
hadi wa leo la kuonesha mmekaribia hata kuwa kichuguu kikubwa! Nyie
wote ni waigizaji na wasanii, mmekuja, mnakuja, mtaondoka na
mtatuacha vilevile kwa kuwa sio watu wa fikira, hekima na busara
jambo ambalo kama kuwa mkubwa pia ni neema na baraka za Muumba kwa
amtakaye. Na hili haliji bila kumgeukia kwanza huyo aliyekuumba.
iv. Utu- hakuna anayejali tena utu wa mwingine katika nchi hii
kuanzia juu hadi chini. Hivi kwanini enzi za Nyerere tulikuwa
wastaabu na leo washenzi?
v) Usawa-Babu alipigana sana kuhakikisha tofauti ya kipato kati yetu
haiwi kubwa kiasi cha kutisha hivi. Matokeo yake sasa baada ya soko
huru la uraruaji wa mali ya umma na mali asili kuna wanaopata
kupindukia kiasi cha kufia kwenye mabichi kila wiki wakijaribu
kufyeka mabinti wanne au watano kwa siku. Tuangalie hili la
kudanganywa na mishahara ya kikoloni tukidhani eti tutaendelea kwa
kuwalipa walimu, madaktari, manesi, wahandisi, askari na kadhalika
mishahara ambayo haikidhi mahitaji yao ya kila leo. Kama ndivyo mbona
kwa miaka 50 hatujaendelea. Au tunaingia 50 nyingine! Naam, mishahara
mizuri kweli itakuja tukiwa kaburini lakini ndio hivyo basi wajemeni?
vi) Kujitegemea- inatia aibu kuona kwamba vitu tunavyoweza kufanya
sisi wenyewe bado tunatembeza bakuli hadi Marekani na Uingereza
[waliotuingiza katika hali tuliyo nayo] na kusahau kuwa kuna nchi
zenye nia na dhati ya kweli kutusaidia sisi na sio hao
tunaowalimbukia. Lakini ndio hivyo tumezoea kupewa samaki na kila
siku tutaendelea kurudi Marekani.
viii) Kujilimbikizia-sasa hivi hakuna mwenye siasa au mwelekeo wa
kumsaidia mwananchi bali ni mbio za ufahari kutaka huyu kumshinda
huyu kwa nyumba kubwa zaidi, gari kubwa zaidi, akiba nono zaidi
benki, watoto kwenda nje na wasisome shule za walahoi na waliwakodi.
ix) Siasa safi-tunahitji hili ili tuendelee liko wapi? Hebu katika
Nyerere day tujiulize- Kasi Mpya, Nguvu Mpya na Ari Mpya vimeishia
wapi?
x) Uongozi bora nao pia- hivi Kila waziri ana Visheni na Misheni ya
Wizara yake? Anajua anakotaka kweli kuipeleka sekta yake. Nini
mipango yao, nini mikakati yao na nini malengo yao kila baada ya
miezi mitatu, nusu mwaka, mwaka mmoja. Au wapowapo tu kwenye
heyakondisheni wakipoozwa maka.....(Malizia Makengeza)...... maana
iwe ni kukarabati njia mpaka Nani aseme, ....shule mpaka Bwamkubwa
aseme, .......kufufua michezo na ushindani nchini, ........mpaka Nani
aseme......usafi na mabustani na magadeni na maviwanja ya watoto wetu
wanaogongwa kwa kucheza barabarani.... au kufia kwenye disko bubu
zisizoizinishwa.... mpaka Nani aseme.......Kilimo na kuwawezesha
wakulima vijana......yuko Wapi waziri jina wa Vijana?
Haya, jamani, hawa ndio mawaziri wenu na wanamaliza miaka mitano na
huku walikotoka hatujaona walichokifanya japo kuna mapipa ya taka
hapa yamejaa ahadi tupu.

Naomba radhi kwa jazba na kuandika kitu kirefu kuliko nilivyotarajia.
Ni matumaini yangu hata hivyo, Ndugu yangu, Mwenzangu, Mlalahoi
mwenzangu Bw. Huduma huko visiwani uko nami na umenielewa natamani
kungelikuwa na Mtanganyika kama wewe Mzanzibari mwenye mapenzi ya
kweli na Mwalimu kama ulivyo wewe. Lakini simuoni. Hata kina Mzee
Mwanakijiji naona wamekwishatekwa na Greencard na siasa zinazojua
kutumia tu bila ya kuingiza kwa halali. Zitatupeleka wapi. Wakati
umefika kujiuliza tushirikiane na Mashariki au tuendelee kuwa


mwalimu jr , hii iweke kwenye gazeti ili umma ukasome
 
Back
Top Bottom