Nyerere alitoa wapi uwezo ule?


X-paster uliyashuhudia haya,achana na hawa waliosimuliwa makanisani mwao.
Kwenye hadhara akisema udini mbaya lakini akiwa ikulu hujisifu kwa kusema sikumchagua huyu kuwa waziri kutokana na uwezo wake katika siasa bali kutokana na imani yake (ukatoliki).

 
Bahati mbaya sana kuna watu hawaoni kitu ila kwa kutumia kioo cha udini. Kama kuna watu waliosaidiwa sana na Nyerere enzi za utawala wake kwenye upande wa elimu walikuwa waislamu. Nyerere alitaifisha shule zote za madhehebu ya dini na kuzifanya za umma. Nyingi kati ya hizo zilikuwa za kikristo. Kwani Kikwete alisoma shule gani?
 
Hakuna kiongozi dhalimu, kama nyerere. Baada ya uhuru alitumia madaraka yake kuhakikisha kuwa ukristo unapata nguvu katika Tanganyika na Tanzania ndo maana mnaona sasa hivi maaskofu wamekua na kauli na sauti ya juu kuliko hata serikali au raisi! Rejea kitabu cha Dr. Sivalon Kanisa katoliki na siasa ya Tanzania bara 1953 mpaka 1985 katika ukurasa 42
 

Mtu mwenye akili hazungumzi juu ya makanisa na misikiti kutetea hoja ya kisiasa kwani kwa Tanzania wakristo na waislam wamechanganyika kiasi kuna familia nyingi aidha zina baba mkristo, mama mwislam au kinyume cha hilo, ukiona mtu anazungumzia makanisa na misikiti basi jua mtu huyo siye
 
Kaka hayo ndio mawazo yangu finyu na huyo ndio Nyerere.... aliye wanyima Watanzania haki ya kutoa mawazo yao...!

Kilichomfanya mpaka akazuiya vyama vingi tulipo pata uhuru ni nini? Ndio zaidi ya jina la Mchonga, tulimwita Aambiliki, kwa sababu hakutaka kusikia mtu mwenye mawazo tofauti naye.

Sina uhakika kama unajuwa kilicho wapata baadhi ya wanasiasa kama vile Oscar Salathiel Kambona.
 
Na ilo ndio lilikuwa tatizo kubwa sana, aliwafumba macho wengi kwa kisingizio cha kutaifisha mashule ya dini, kumbe ilikuwa njia ya kuzipatia ruzuku toka serikalini, shule za kikatoliki zilifaidika sana kwa tendo ilo.
 
Sijui unazungumzia shule zipi za kikatoliki. Mimi ni mkatoliki na nilisoma shule ya St. Benedict Secondary School Kigonsera. Maisha yalikuwa mazuri sana wakati shule ilipokuwa inaendeshwa na Roman Catholic Church kutokea Peramiho. ilipofika mwaka 1970 ndipo tulipojua kuwa kuna kunywa uji na maharage na ugali kila mchana. Chai ya saa 4 na saa 10 ikafutwa. Vifaa vya michezo na hata walimu ikawa taabu sana kupata. Magari tuliyokuwa nayo hayakutengezwa na yalichakaa baadaye tukaletewa JaeFong ya Mchina iliyochoka kwelikweli. Maisha katika shule za serikali yalikuwa ni mateso matupu kama yalivyo leo hii kwenye shule za serikali na kata.
 
Alikuwa msafi na mkweli faraghani na hadharani!
Alikuwa msemaji mzuri kweli kweli, na hotuba zake zilivutia haswa, na aliyeweza kuutetea uongo ukafanana na kweli.

Alikuwa hodari sana, hizo sifa kweli alikuwa nazo, wala sipingi.
 
Nyerere alikuwa msomi bonafide, ingawa alikuwa plagiarist anayesema maneno ya watu wengine kama yake. Kama alivyoandika Jenerali Ulimwengu katika piece yake ya hivi karibuni, Nyerere alijikita katika ideas na intellectuallism (not always a good thing).

Pia miaka yake ya shule, hususan Edinburgh Scotland, aliitumia vizuri kujiimarisha katika Fabian Society iliyokuwa na discussions / debates deep sana kuhusu rhetoric, siasa, uchumi na historia. He was alright upstairs, not like these other half baked bird brained laggard losers quackery quoting niggard nincompoops.

Afadhali Nyerere alikuwa Fabian na katafsiri Shakespeare's "Merchants of Venice" kwenda Kiswahili, pamoja na kuandika kazi kadhaa zilizo solid, unaweza hata kuinarrow down "Nyerereism".

Mtu kama Kikwete hata huwezi kujua fikra zake zinaongozwa na nini apart from the party boilerplate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…