Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,436
- 4,429
Mleta mada huwa naheshimu sana michango yako, lakini huu wa leo umepotoka na kunikatisha tamaa. Mwalimu nyerere alishaweka wazi kabisa suala la HAKI na AMANI. Maandiko yake mengi amezungumza kwa upana sana mambo hayo akisema hayapaswi kutengana. Nakushauri usome maandiko ya mwalimu hasa vitabu kama Ujamaa ni Imani (2), Uhuru na Umoja, Uhuru na Kazi nk. Pia sikiliza hotuba zake, ikiwamo ile aliyoitoa ktk Bunge la Afrika Kusini miaka michache kabla hajafariki dunia.kwa ufupi, huwezi kumjua mwalimu kama husomi vitabu vyake au kama husikilizi hotuba zake. Mwalimu atabaki kuwa mwalimu sahihi aliyegusa kila nyanja ya maisha ya mwanadamu.