Nyaraka za Nangwanda Lawi Sijaona: Sijaona na Nyerere Wakiazimana Vitabu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,913
30,255
KUTOKA NYARAKA ZA LAWI NANGWANDA SIJAONA: MWALIMU ANAMWAGIZA MSAIDIZI WAKE JOAN WICKENS AMPELEKEE SIJAONA KITABU ''FALSE START IN AFRICA''

Adam Sijaona mtoto wa marehemu Nangwanda Lawi Sijaona amenifungulia nyaraka za baba yake nisome kama Ally Sykes alivyonifungulia nyaraka zake.

Hili ni jambo kubwa sana kwa mtafiti yeyote kuonyeshwa nyaraka za ndani chumbani wala si za uani za historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiandikiana na wale ambao alikuwanao kwanza katika kupigania uhuru wa Tanganyika miaka ya 1950 kisha katika kuendesha serikali miaka ya 1960 na kuendelea.

Adam Sijali Sijaona kaniandikia ananieleza kuwa katika nyaraka za baba yake kuna barua kutoka kwa Mama Wickens kwenda kwa baba yake kuhusu vitabu ambavyo Mwalimu akiazimana na Lawi Sijaona.

Adam akanifahamisha kuwa barua hizi anaziweka pembeni.

Mimi ile kusoma kuwa Nyerere akiazimana vitabu na Sijaona moyo umeanza kwenda mbio.

Kimoyomoyo naanza kumlaumu Adam kwa kule kusema kuwa barua hizo za Joan Wickens kwa baba yake anaziweka pembeni maana yake kuwa mimi hatanionyesha.

Adam kwake yeye kaona labda si muhimu kwangu.

Kanichokoza naweka hapa chini maneno niliyomwandikia rafiki yangu:

''Duu...

Baba akiazimana vitabu na Kambarage!
Hii kubwa kushinda Mlima Kilimanjaro.

Nipatie hizo barua kaka.
Sijali wewe unataka kufanya maskhara bwana.

Hii sijaona popote.

In Shaa Allah nitaandika jambo kuhusu Nyerere na vitabu tena kutoka kwa watu wake wa karibu sana.

Nyerere alikuwa na wazimu wa vitabu.''

Juma Mwapachu anaijua maktaba ya Mwalimu na kapata kunisifia kuhusu hazina iliyoko nyumbani kwa Mwalimu Butiama.

Adam akaniletea barua hizo na kwa uungwana wake akaniambia,''...kumbe hizi nyaraka sipaswi kutolea hukumu mimi nilibahatisha kukufahamisha sikujua utakuwa na shauku nazo kiasi hicho.''

Mtafiti gani ambae hatakuwa na shauku ya kusoma nyaraka za Joan Wickens au za Julius Nyerere mwenyewe?

Mimi nilitaka kujua Mwalimu akisoma vitabu gani?

Kwani kuna vitabu na vitabu.
Si kila kitabu ni kitabu.

Mzigo wa barua za Julius Nyerere kwa Joan Wickens, barua za Wickens kwa Lawi Sijaona na kadha wa kadha zikaingia.

Furaha yangu haielezeki.

Soma mwenyewe hapo chini barua ya Mwalimu kwa Lawi Sijaona.

Tusiandikie mate wakati kidau cha wino tunacho.

Sijali akawa kanipa ufunguo kwa kufungua kwanza ubongo wa baba yake Mzee Sijaona pili ufunguo wa kufungua ubongo wa Mwalimu Nyerere.

Kuna barua nyingine Mwalimu Nyerere anamuagiza Joan Wickens, Personal Assistant to the President kumpeleka Lawi Sijaona kitabu hiki, ''False Start in Africa,'' kilichaondikwa na Mfaransa Rene Dumont.

Kitabu hiki kilikuwa maarufu sana miaka ya 1960 na Mwalimu kakisifia anamwambia Sijaona kuwa kinafaa kwa maendeleo ya Tanzania.

Maneno haya Mwalimu kaandika mwaka wa 1966.

Nilipoona kitabu hiki cha Rene Dumont katika barua ya Mwalimu akili yangu ikarudi nyuma hadi mwaka wa 1972 niko nyumbani kwa Dome Okochi Budohi, Ruiru, Nairobi nimekwenda kumtembelea.

Dome Okochi Budohi kadi yake ya TANU ni. No. 6.

Naamini wengi mtashangaa mbona hamjapata kumsikia popote akitajwa katika ya TANU na uhuru waTanganyika?

Historia ya Dome Okochi Budohi katika siasa za TAA hadi TANU ni ndefu na nimemweleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

(Dome Budohi alikamatwa Dar es Salaam 1955 na kufungwa kisiwani Lamu, Kenya akishukiwa kuwa ni Mau Mau).

Kitabu hiki ''False Start in Africa,'' nilikikuta nyumbani kwa Dome Budohi Nairobi na nilianza kukisoma lakini sikuweza kukimaliza na Mzee Budohi akanipa kitabu hiki nikimalize kusoma Dar es Salaam.

Kwa miaka mingi kitabu hiki nilikuwanacho Maktaba lakini kimepotea.

Kitabu hiki kimesomwa na Julius Nyerere, Lawi Sijaona na Dome Budohi wote hawa wanachama wa TAA na waasisi wa TANU.

Hii inaonyesha vipi fikra za wazalendo hawa zilivyokuwa zinashabihiana katika kutafuta maendeleo ya nchi yao.

Nimeiona maktaba ya Hamza Mwapachu katika miaka ya 1970 iko vilevile kama alivyoiacha mwenyewe miaka mingi baada ya kufariki.

Wazalendo hawa walikuwa watu wa kusoma vitabu.

Picha: Barua ya Mwalimu Nyerere kwa Nangwanda Lawi Sijaona, Mwandishi na Dome Okochi Budohi na Adam Sijali Sijaona na baba yake Nangwanda Lawi Sijaona.

1685184314302.png

1685184366924.png

1685184416564.png
 
Mzee Mohamed Said, hii historia ni nzuri sana! Shukrani sana kwa kuendelea kutujuza!

Nje ya mada:
Wakuu mbona kwangu picha hazifunguki kabisa? Ni zaidi ya mwezi mzima sasa tangu tatizo hili litokee.

Naombeni ushauri wenu wa namna ya kupata ufumbuzi.
 
Ajabu nini hapo?

Baba yangu alikula ugali na mchicha na Nyerere Magomeni mwaka 1957 kabla hajaenda USA.

Labda wengi hawakumuelewa Nyerere.

Nyerere alikua Panafricanist hivyo alitumia kila Mwafrika kutimiza lengo.
 
Ajabu nini hapo?

Baba yangu alikula ugali na mchicha na Nyerere Magomeni mwaka 1957 kabla hajaenda USA.

Labda wengi hawakumuelewa Nyerere.

Nyerere alikua Panafricanist hivyo alitumia kila Mwafrika kutimiza lengo.
Stroke,
Ikiwa baba yako alikula ugali na mchicha na Nyerere mwaka wa 1957 hii peke yake ni historia muhimu kupita kiasi achilia mbali hilo la kwenda USA.

Mwaka wa 1957 Nyerere anavuma Tanganyika nzima kama kiongozi wa TANU akiongoza harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia ya Mwalimu Nyerere ndani ya TANU kwa miaka mingi ilikuwa haifahamiki vyema na sababu kubwa ni kuwa yeye mwenyewe hakutaka ifahamike.

Historia ya Mwalimu ilikujakufahamika baada ya mimi kuandikia kitabu cha Abdul Sykes ambacho kilieleza historia takriban yote ya kupigania uhuru wa Tanganyika na ikawataja wazalendo wengi ambao historia zilizokuwapo hazikuwataja popote.

Ikiwa baba yako mwaka wa 1957 anafahamiana na Nyerere kiasi cha kula chakula pamoja bila shaka wewe una historia ambayo itapendeza ikiwa utaieleza kwani itaongeza elimu katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Daisy Sykes aliandika makala na akaeleza yeye alivyokuwa akimuandalia Mwalimu chai nyumbani kwao alipokuwa anakuja kuonana na baba yake akitokea Pugu alipokuwa akifundisha:

''Lakini aliyeshika nafasi ya juu kabisa katika fikra zangu nikiwa mtoto alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na ni kupitia kwake ndipo tukapata kujua kwa mara ya kwanza kuwa kuna kabila linaitwa, ‘’Wazanaki.’’

Kila alipokuwa anakuja nyumbani kwetu kuja kwake kulikuwa jambo maalum kulikosababisha minong’ono watu wakizungumza kwa sauti za chini wakipeana taarifa kuwa, ‘’Nyerere anakuja au keshafika.”

Kwangu mimi hii ilikuwa ishara ya kutimiza kazi yangu kwani siku zote nilikuwa nikiambiwa kutengeneza kifungua kinywa cha chai na mayai kila alipokuja nyumbani akitokea Shule ya Mt. Francis, Pugu alipokuwa akisomesha.​

Nakumbuka katika akili yangu ya kitoto kumuona Mwalimu Nyerere akiishi nyumbani kwetu kwa muda katika nyumba yetu ya Mtaa wa Stanley baada ya kuacha kazi wakati marafiki zake wa karibu baba na Dossa Aziz walikuwa wanamtafutia nyumba ya kuishi.''

Naamini kipande hiki kimekuonyesha historia ya Mwalimu ambayo wewe hukuwa unaijua.

Hii ni miaka hiyo hiyo hiyo ambayo baba yako alikuwa anakula ugali na mchicha na Nyerere.

Bila wasiwasi wowote baba yako atakuwa mtu muhimu sana na yuko katika kundi hili la akina Abdul Sykes.

Mimi binafsi ningependa sana kujua historia hiyo ya baba yako.
 
Stroke,
Ikiwa baba yako alikula ugali na mchicha na Nyerere mwaka wa 1957 hii peke yake ni historia muhimu kupita kiasi achilia mbali hilo la kwenda USA.

Mwaka wa 1957 Nyerere anavuma Tanganyika nzima kama kiongozi wa TANU akiongoza harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia ya Mwalimu Nyerere ndani ya TANU kwa miaka mingi ilikuwa haifahamiki vyema na sababu kubwa ni kuwa yeye mwenyewe hakutaka ifahamike.

Historia ya Mwalimu ilikujakufahamika baada ya mimi kuandikia kitabu cha Abdul Sykes ambacho kilieleza historia takriban yote ya kupigania uhuru wa Tanganyika na ikawataja wazalendo wengi ambao historia zilizokuwapo hazikuwataja popote.

Ikiwa baba yako mwaka wa 1957 anafahamiana na Nyerere kiasi cha kula chakula pamoja bila shaka wewe una historia ambayo itapendeza ikiwa utaieleza kwani itaongeza elimu katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Daisy Sykes aliandika makala na akaeleza yeye alivyokuwa akimuandalia Mwalimu chai nyumbani kwao alipokuwa anakuja kuonana na baba yake akitokea Pugu alipokuwa akifundisha:

''Lakini aliyeshika nafasi ya juu kabisa katika fikra zangu nikiwa mtoto alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na ni kupitia kwake ndipo tukapata kujua kwa mara ya kwanza kuwa kuna kabila linaitwa, ‘’Wazanaki.’’

Kila alipokuwa anakuja nyumbani kwetu kuja kwake kulikuwa jambo maalum kulikosababisha minong’ono watu wakizungumza kwa sauti za chini wakipeana taarifa kuwa, ‘’Nyerere anakuja au keshafika.”

Kwangu mimi hii ilikuwa ishara ya kutimiza kazi yangu kwani siku zote nilikuwa nikiambiwa kutengeneza kifungua kinywa cha chai na mayai kila alipokuja nyumbani akitokea Shule ya Mt. Francis, Pugu alipokuwa akisomesha.​

Nakumbuka katika akili yangu ya kitoto kumuona Mwalimu Nyerere akiishi nyumbani kwetu kwa muda katika nyumba yetu ya Mtaa wa Stanley baada ya kuacha kazi wakati marafiki zake wa karibu baba na Dossa Aziz walikuwa wanamtafutia nyumba ya kuishi.''

Naamini kipande hiki kimekuonyesha historia ya Mwalimu ambayo wewe hukuwa unaijua.

Hii ni miaka hiyo hiyo hiyo ambayo baba yako alikuwa anakula ugali na mchicha na Nyerere.

Bila wasiwasi wowote baba yako atakuwa mtu muhimu sana na yuko katika kundi hili la akina Abdul Sykes.

Mimi binafsi ningependa sana kujua historia hiyo ya baba yako.
Mwaka 1960 mzee anapata degree yake ya kwanza.

Hii ni baada ya kupata scholarship akitokea Nairobi University alipokua akisoma uchumi.

Alirudi Nyumbani na Nyerere alikua akimtembeza kwenye maduka ya wahindi ili mzee apate nauli ya kwenda huko marekani masomoni.

Kwahiyo meeting point ilikua Magomeni wakiwa wanatafuta nauli kwenye maduka ya wahindi.

Mzee alisafiri kwa kutumia Passport ya Uingereza maana bado Tanganyika ilikua koloni.


Hakua mwanasiasa.

Ila alikua very bright.

Ni wanafunzi wa mwanzo mwanzo Ilboru secondary na Tabora boys.

Nyerere alikua binadamu.

Alikutana na wengi.
 
Mwaka 1960 mzee anapata degree yake ya kwanza.

Hii ni baada ya kupata scholarship akitokea Nairobi University alipokua akisoma uchumi.

Alirudi Nyumbani na Nyerere alikua akimtembeza kwenye maduka ya wahindi ili mzee apate nauli ya kwenda huko marekani masomoni.

Kwahiyo meeting point ilikua Magomeni wakiwa wanatafuta nauli kwenye maduka ya wahindi.

Mzee alisafiri kwa kutumia Passport ya Uingereza maana bado Tanganyika ilikua koloni.


Hakua mwanasiasa.

Ila alikua very bright.

Ni wanafunzi wa mwanzo mwanzo Ilboru secondary na Tabora boys.

Nyerere alikua binadamu.

Alikutana na wengi.
Stroke,
Historia nzuri lakini mwaka wa 1960 University of Nairobi ilikuwa bado.
Kama cheti cha baba unacho kiangalie.

Kuhusu pasi Waafrika wa Tanganyika walikuwa wakipewa pasi za Tanganyika zilizokuwa zinatolewa na Uingereza hawakuwa wanasafiri na pasi za Uingereza.

Kama pasi ya baba ipo iangalie utaona jina la Tanganyika.

Yawezekana baba ni kati ya wanafunzi wa mwanzo wa Ilboru kwani hiyo ni shule katika miaka ya 1940 ndipo ilipoanzishwa lakini Tabora School ni shule ya zamani sana toka 1920s.

Kuhusu utu wa Nyerere unajulikana sana hakuna asiyeujua.
Alipokelewa na wazee wetu na wakaishi na yeye hadi uhuru ulipopatikana 1961.

Angalia pasi za wakati wa ukoloni hapo chini:

1685301937671.jpeg
 
Stroke,
Historia nzuri lakini mwaka wa 1960 University of Nairobi ilikuwa bado.
Kama cheti cha baba unacho kiangalie.

Kuhusu pasi Waafrika wa Tanganyika walikuwa wakipewa pasi za Tanganyika zilizokuwa zinatolewa na Uingereza hawakuwa wanasafiri na pasi za Uingereza.

Kama pasi ya baba ipo iangalie utaona jina la Tanganyika.

Yawezekana baba ni kati ya wanafunzi wa mwanzo wa Ilboru kwani hiyo ni shule katika miaka ya 1940 ndipo ilipoanzishwa lakini Tabora School ni shule ya zamani sana toka 1920s.

Kuhusu utu wa Nyerere unajulikana sana hakuna asiyeujua.
Alipokelewa na wazee wetu na wakaishi na yeye hadi uhuru ulipopatikana 1961.

Angalia pasi za wakati wa ukoloni hapo chini:

Nairobi University ilianza 1956 kama Royal Technical college so he was right.
Pale hakumaliza alirudi Nyumbani baada ya kupata scholarship ili aende USA. Ndio kisa cha kukutana na Nyerere.

Passport ndio hiyo hiyo mkuu.

Blue kubwa imeandikwa British Passport Tanganyika Protectorate.

Ni kweli Tabora boys ni ya zamani.
 
Nairobi University ilianza 1956 kama Royal Technical college so he was right.
Pale hakumaliza alirudi Nyumbani baada ya kupata scholarship ili aende USA. Ndio kisa cha kukutana na Nyerere.

Passport ndio hiyo hiyo mkuu.

Blue kubwa imeandikwa British Passport Tanganyika Protectorate.

Ni kweli Tabora boys ni ya zamani.
Stroke,
Mwalimu 1957 alikuwa akiishi Maduka Sita, Magomeni.

Kabla ya nyumba yake ilikuwa nyumba ya Ramadhani Aziz mdogo wake Dossa Aziz.

Sababu ya rafiki zake kumtafutia nyumba hiyo ni kuwa hawakutaka awe peke yake walitaka awe pale jirani na Ramadhani Aziz.

Ikiwa ugali na mchicha baba alikula kwa Nyerere nyumba hiyo ilikuwa Maduka Sita.

Angalia picha hapo chini Mwalimu akiingia nyumbani kwake:

1685303405707.png

Nyumba ya Julius Nyerere Magomeni Maduka Sita​
 
Stroke,
Mwalimu 1957 alikuwa akiishi Maduka Sita, Magomeni.

Kabla ya nyumba yake ilikuwa nyumba ya Ramadhani Aziz mdogo wake Dossa Aziz.

Sababu ya rafiki zake kumtafutia nyuma hiyo ni kuwa hawakutaka awe peke yake walitaka awe pale jirani na Ramadhani Aziz.

Ikiwa ugali na mchicha baba alikula kwa Nyerere nyumba hiyo ilikuwa Maduka Sita.

Angalia picha hapo chini Mwalimu akiingia nyumbani kwake:

View attachment 2638736
Nyumba ya Julius Nyerere Magomeni Maduka Sita​
ml
Sawa mkuu itoshe kusema kwamba Mwalimu alikua na utu.

Alitaka kuona Taifa likiwa na wataalam wa kutosha.

Baada ya masomo mzee alirejea na kuwa mkufunzi vyuo mbali mbali hapa nchini akaoa Mwalimu pia.

Kwahiyo nimekua kwenye familia ya walimu.

Michezo Yangu nimefanya kwenye madawati na ubao za chuo.

Taifa letu Lina historia nyingi na nzuri ila hakuna utaratibu mzuri wa kuziweka katika kumbukumbu.
 
Sawa mkuu itoshe kusema kwamba Mwalimu alikua na utu.

Alitaka kuona Taifa likiwa na wataalam wa kutosha.

Baada ya masomo mzee alirejea na kuwa mkufunzi vyuo mbali mbali hapa nchini akaoa Mwalimu pia.

Kwahiyo nimekua kwenye familia ya walimu.

Michezo Yangu nimefanya kwenye madawati na ubao za chuo.

Taifa letu Lina historia nyingi na nzuri ila hakuna utaratibu mzuri wa kuziweka katika kumbukumbu.
Sasa ulitaka kupingana na mzee wako wewe kijana heshimu watu amekueleza vizuri mpaka umeelewa.wewe uliona baba yako kula ugali na mchicha na mwl ni kitu kidogo lakini umeelewa Sasa maana ya historia
 
Sawa mkuu itoshe kusema kwamba Mwalimu alikua na utu.

Alitaka kuona Taifa likiwa na wataalam wa kutosha.

Baada ya masomo mzee alirejea na kuwa mkufunzi vyuo mbali mbali hapa nchini akaoa Mwalimu pia.

Kwahiyo nimekua kwenye familia ya walimu.

Michezo Yangu nimefanya kwenye madawati na ubao za chuo.

Taifa letu Lina historia nyingi na nzuri ila hakuna utaratibu mzuri wa kuziweka katika kumbukumbu.
Stroke,
Kuhusu Mwalimu namjua vizuri sana.

Mwalimu alitaka zaidi ya hayo ya kuwa na wataalamu.

Maktaba yangu ni kati ya maktaba tatu zilizosifiwa na waandishi wa ''Nyerere Biography'' (2020) kwa kusheheni taarifa nyingi za Nyerere.

Kuhusu historia ya taifa hili soma kitabu cha Abdul Sykes kuna mengi ya kukushangaza.
 
KUTOKA NYARAKA ZA LAWI NANGWANDA SIJAONA: MWALIMU ANAMWAGIZA MSAIDIZI WAKE JOAN WICKENS AMPELEKEE SIJAONA KITABU ''FALSE START IN AFRICA''

Adam Sijaona mtoto wa marehemu Nangwanda Lawi Sijaona amenifungulia nyaraka za baba yake nisome kama Ally Sykes alivyonifungulia nyaraka zake.

Hili ni jambo kubwa sana kwa mtafiti yeyote kuonyeshwa nyaraka za ndani chumbani wala si za uani za historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiandikiana na wale ambao alikuwanao kwanza katika kupigania uhuru wa Tanganyika miaka ya 1950 kisha katika kuendesha serikali miaka ya 1960 na kuendelea.

Adam Sijali Sijaona kaniandikia ananieleza kuwa katika nyaraka za baba yake kuna barua kutoka kwa Mama Wickens kwenda kwa baba yake kuhusu vitabu ambavyo Mwalimu akiazimana na Lawi Sijaona.

Adam akanifahamisha kuwa barua hizi anaziweka pembeni.

Mimi ile kusoma kuwa Nyerere akiazimana vitabu na Sijaona moyo umeanza kwenda mbio.

Kimoyomoyo naanza kumlaumu Adam kwa kule kusema kuwa barua hizo za Joan Wickens kwa baba yake anaziweka pembeni maana yake kuwa mimi hatanionyesha.

Adam kwake yeye kaona labda si muhimu kwangu.

Kanichokoza naweka hapa chini maneno niliyomwandikia rafiki yangu:

''Duu...

Baba akiazimana vitabu na Kambarage!
Hii kubwa kushinda Mlima Kilimanjaro.

Nipatie hizo barua kaka.
Sijali wewe unataka kufanya maskhara bwana.

Hii sijaona popote.

In Shaa Allah nitaandika jambo kuhusu Nyerere na vitabu tena kutoka kwa watu wake wa karibu sana.

Nyerere alikuwa na wazimu wa vitabu.''

Juma Mwapachu anaijua maktaba ya Mwalimu na kapata kunisifia kuhusu hazina iliyoko nyumbani kwa Mwalimu Butiama.

Adam akaniletea barua hizo na kwa uungwana wake akaniambia,''...kumbe hizi nyaraka sipaswi kutolea hukumu mimi nilibahatisha kukufahamisha sikujua utakuwa na shauku nazo kiasi hicho.''

Mtafiti gani ambae hatakuwa na shauku ya kusoma nyaraka za Joan Wickens au za Julius Nyerere mwenyewe?

Mimi nilitaka kujua Mwalimu akisoma vitabu gani?

Kwani kuna vitabu na vitabu.
Si kila kitabu ni kitabu.

Mzigo wa barua za Julius Nyerere kwa Joan Wickens, barua za Wickens kwa Lawi Sijaona na kadha wa kadha zikaingia.

Furaha yangu haielezeki.

Soma mwenyewe hapo chini barua ya Mwalimu kwa Lawi Sijaona.

Tusiandikie mate wakati kidau cha wino tunacho.

Sijali akawa kanipa ufunguo kwa kufungua kwanza ubongo wa baba yake Mzee Sijaona pili ufunguo wa kufungua ubongo wa Mwalimu Nyerere.

Kuna barua nyingine Mwalimu Nyerere anamuagiza Joan Wickens, Personal Assistant to the President kumpeleka Lawi Sijaona kitabu hiki, ''False Start in Africa,'' kilichaondikwa na Mfaransa Rene Dumont.

Kitabu hiki kilikuwa maarufu sana miaka ya 1960 na Mwalimu kakisifia anamwambia Sijaona kuwa kinafaa kwa maendeleo ya Tanzania.

Maneno haya Mwalimu kaandika mwaka wa 1966.

Nilipoona kitabu hiki cha Rene Dumont katika barua ya Mwalimu akili yangu ikarudi nyuma hadi mwaka wa 1972 niko nyumbani kwa Dome Okochi Budohi, Ruiru, Nairobi nimekwenda kumtembelea.

Dome Okochi Budohi kadi yake ya TANU ni. No. 6.

Naamini wengi mtashangaa mbona hamjapata kumsikia popote akitajwa katika ya TANU na uhuru waTanganyika?

Historia ya Dome Okochi Budohi katika siasa za TAA hadi TANU ni ndefu na nimemweleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

(Dome Budohi alikamatwa Dar es Salaam 1955 na kufungwa kisiwani Lamu, Kenya akishukiwa kuwa ni Mau Mau).

Kitabu hiki ''False Start in Africa,'' nilikikuta nyumbani kwa Dome Budohi Nairobi na nilianza kukisoma lakini sikuweza kukimaliza na Mzee Budohi akanipa kitabu hiki nikimalize kusoma Dar es Salaam.

Kwa miaka mingi kitabu hiki nilikuwanacho Maktaba lakini kimepotea.

Kitabu hiki kimesomwa na Julius Nyerere, Lawi Sijaona na Dome Budohi wote hawa wanachama wa TAA na waasisi wa TANU.

Hii inaonyesha vipi fikra za wazalendo hawa zilivyokuwa zinashabihiana katika kutafuta maendeleo ya nchi yao.

Nimeiona maktaba ya Hamza Mwapachu katika miaka ya 1970 iko vilevile kama alivyoiacha mwenyewe miaka mingi baada ya kufariki.

Wazalendo hawa walikuwa watu wa kusoma vitabu.

Picha: Barua ya Mwalimu Nyerere kwa Nangwanda Lawi Sijaona, Mwandishi na Dome Okochi Budohi na Adam Sijali Sijaona na baba yake Nangwanda Lawi Sijaona.

Nyerere mwenyewe kumbe hakukifagilia kiswahili.
 
Nyerere mwenyewe kumbe hakukifagilia kiswahili.
Baada ya uhuru kiingereza kiliendelea kuwa lugha rasmi ya mawasiliano maofisini hadi miaka kadhaa baadaye. Nadhani 1967 baada ya azimio la Arusha ndio kiswahili kilirasmishwa.
 
Nyerere mwenyewe kumbe hakukifagilia kiswahili.
Vict...
Usidhani kwa kutumia Kiingereza Mwalimu hakukithamini Kiswahili.

Hiyo ni sababu ya nyakati.

Ndiyo kwanza nchi imekuwa huru na lugha ya serikali ilikuwa Kiingereza.

Taratibu nchi ilijitoa katika matumizi ya Kiingereza na kutumia Kiswahili.

Mwalimu akikipenda Kiswahili na alikuwa akiandika hata mashairi ya Kiswahili.
 
Vict...
Usidhani kwa kutumia Kiingereza Mwalimu hakukithamini Kiswahili.

Hiyo ni sababu ya nyakati.

Ndiyo kwanza nchi imekuwa huru na lugha ya serikali ilikuwa Kiingereza.

Taratibu nchi ilijitoa katika matumizi ya Kiingereza na kutumia Kiswahili.

Mwalimu akikipenda Kiswahili na alikuwa akiandika hata mashairi ya Kiswahili.
Kuna kingine pia kilichoitwa Africanization, kuwapatia watanganyika nyadhifa zilizokuwa zimeshikwa na wazungu.

Kutokana na uchache wa wasomi tuliokuwa nao, nasikia ni moja ya maeneo ambayo serikali iliharibu.

Kama katika tafiti zako ulipitia hili, naomba utushirikishe ujuzi wako.
 
KUTOKA NYARAKA ZA LAWI NANGWANDA SIJAONA: MWALIMU ANAMWAGIZA MSAIDIZI WAKE JOAN WICKENS AMPELEKEE SIJAONA KITABU ''FALSE START IN AFRICA''

Adam Sijaona mtoto wa marehemu Nangwanda Lawi Sijaona amenifungulia nyaraka za baba yake nisome kama Ally Sykes alivyonifungulia nyaraka zake.

Hili ni jambo kubwa sana kwa mtafiti yeyote kuonyeshwa nyaraka za ndani chumbani wala si za uani za historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiandikiana na wale ambao alikuwanao kwanza katika kupigania uhuru wa Tanganyika miaka ya 1950 kisha katika kuendesha serikali miaka ya 1960 na kuendelea.

Adam Sijali Sijaona kaniandikia ananieleza kuwa katika nyaraka za baba yake kuna barua kutoka kwa Mama Wickens kwenda kwa baba yake kuhusu vitabu ambavyo Mwalimu akiazimana na Lawi Sijaona.

Adam akanifahamisha kuwa barua hizi anaziweka pembeni.

Mimi ile kusoma kuwa Nyerere akiazimana vitabu na Sijaona moyo umeanza kwenda mbio.

Kimoyomoyo naanza kumlaumu Adam kwa kule kusema kuwa barua hizo za Joan Wickens kwa baba yake anaziweka pembeni maana yake kuwa mimi hatanionyesha.

Adam kwake yeye kaona labda si muhimu kwangu.

Kanichokoza naweka hapa chini maneno niliyomwandikia rafiki yangu:

''Duu...

Baba akiazimana vitabu na Kambarage!
Hii kubwa kushinda Mlima Kilimanjaro.

Nipatie hizo barua kaka.
Sijali wewe unataka kufanya maskhara bwana.

Hii sijaona popote.

In Shaa Allah nitaandika jambo kuhusu Nyerere na vitabu tena kutoka kwa watu wake wa karibu sana.

Nyerere alikuwa na wazimu wa vitabu.''

Juma Mwapachu anaijua maktaba ya Mwalimu na kapata kunisifia kuhusu hazina iliyoko nyumbani kwa Mwalimu Butiama.

Adam akaniletea barua hizo na kwa uungwana wake akaniambia,''...kumbe hizi nyaraka sipaswi kutolea hukumu mimi nilibahatisha kukufahamisha sikujua utakuwa na shauku nazo kiasi hicho.''

Mtafiti gani ambae hatakuwa na shauku ya kusoma nyaraka za Joan Wickens au za Julius Nyerere mwenyewe?

Mimi nilitaka kujua Mwalimu akisoma vitabu gani?

Kwani kuna vitabu na vitabu.
Si kila kitabu ni kitabu.

Mzigo wa barua za Julius Nyerere kwa Joan Wickens, barua za Wickens kwa Lawi Sijaona na kadha wa kadha zikaingia.

Furaha yangu haielezeki.

Soma mwenyewe hapo chini barua ya Mwalimu kwa Lawi Sijaona.

Tusiandikie mate wakati kidau cha wino tunacho.

Sijali akawa kanipa ufunguo kwa kufungua kwanza ubongo wa baba yake Mzee Sijaona pili ufunguo wa kufungua ubongo wa Mwalimu Nyerere.

Kuna barua nyingine Mwalimu Nyerere anamuagiza Joan Wickens, Personal Assistant to the President kumpeleka Lawi Sijaona kitabu hiki, ''False Start in Africa,'' kilichaondikwa na Mfaransa Rene Dumont.

Kitabu hiki kilikuwa maarufu sana miaka ya 1960 na Mwalimu kakisifia anamwambia Sijaona kuwa kinafaa kwa maendeleo ya Tanzania.

Maneno haya Mwalimu kaandika mwaka wa 1966.

Nilipoona kitabu hiki cha Rene Dumont katika barua ya Mwalimu akili yangu ikarudi nyuma hadi mwaka wa 1972 niko nyumbani kwa Dome Okochi Budohi, Ruiru, Nairobi nimekwenda kumtembelea.

Dome Okochi Budohi kadi yake ya TANU ni. No. 6.

Naamini wengi mtashangaa mbona hamjapata kumsikia popote akitajwa katika ya TANU na uhuru waTanganyika?

Historia ya Dome Okochi Budohi katika siasa za TAA hadi TANU ni ndefu na nimemweleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

(Dome Budohi alikamatwa Dar es Salaam 1955 na kufungwa kisiwani Lamu, Kenya akishukiwa kuwa ni Mau Mau).

Kitabu hiki ''False Start in Africa,'' nilikikuta nyumbani kwa Dome Budohi Nairobi na nilianza kukisoma lakini sikuweza kukimaliza na Mzee Budohi akanipa kitabu hiki nikimalize kusoma Dar es Salaam.

Kwa miaka mingi kitabu hiki nilikuwanacho Maktaba lakini kimepotea.

Kitabu hiki kimesomwa na Julius Nyerere, Lawi Sijaona na Dome Budohi wote hawa wanachama wa TAA na waasisi wa TANU.

Hii inaonyesha vipi fikra za wazalendo hawa zilivyokuwa zinashabihiana katika kutafuta maendeleo ya nchi yao.

Nimeiona maktaba ya Hamza Mwapachu katika miaka ya 1970 iko vilevile kama alivyoiacha mwenyewe miaka mingi baada ya kufariki.

Wazalendo hawa walikuwa watu wa kusoma vitabu.

Picha: Barua ya Mwalimu Nyerere kwa Nangwanda Lawi Sijaona, Mwandishi na Dome Okochi Budohi na Adam Sijali Sijaona na baba yake Nangwanda Lawi Sijaona.

False Start in Africa nilikisoma nikiwa Form 5. Nadhani kitabu hiki baadaye kilitafsiriwa kwa kiswahili na Profesa Gabriel Ruhumbika kama "Afrika inakwenda Kombo"
 
Stroke,
Mwalimu 1957 alikuwa akiishi Maduka Sita, Magomeni.

Kabla ya nyumba yake ilikuwa nyumba ya Ramadhani Aziz mdogo wake Dossa Aziz.

Sababu ya rafiki zake kumtafutia nyuma hiyo ni kuwa hawakutaka awe peke yake walitaka awe pale jirani na Ramadhani Aziz.

Ikiwa ugali na mchicha baba alikula kwa Nyerere nyumba hiyo ilikuwa Maduka Sita.

Angalia picha hapo chini Mwalimu akiingia nyumbani kwake:

View attachment 2638736
Nyumba ya Julius Nyerere Magomeni Maduka Sita​
Pisi kali
 
Baada ya uhuru kiingereza kiliendelea kuwa lugha rasmi ya mawasiliano maofisini hadi miaka kadhaa baadaye. Nadhani 1967 baada ya azimio la Arusha ndio kiswahili kilirasmishwa.
Hapo anamuandikia Lawi barua ya kibinafsi,si ya kiofice.
 
Back
Top Bottom