NYARAKA: Omar Nundu ni msafi...

Mkuu Kimbunga, mambo mengine wee acha tuu!.

Nimeuliza nani anaejua hao CCCC wamepatikanaje?, hakujatolewa tangazo lolote hata la EOI tuu achilia mbali tender!.

Laiti watu wangelimjua who is behind Mfutakamba, mtagundua Nundu ni mtu wa kuhurumiwa tuu!.

Nchi hii inajengwa na wenye moyo kama Nundu na inaliwa na wenye meno kama Mfutakamba!.
 
Last edited by a moderator:
Nimeshawahi kusema kwasasa Serikali ya JK nguo,zinaanza kudondoka mojamoja. Hatimaye itabaki uch *** hapo ndipo kwenye swali nani ataitupia TAULO Serikali ya JK ili isibaki uch***?
Ninachokiona hapa waliopo nje wanapiga ''jaramba'' na ''mataulo'' na waliopo ndani wako bize kupiga ''tikitaka'' na mataulo !! .......... Sasa kunoga !!!
 
Rushwa ilivyokithiri hujui nani mkweli kibaya zaidi tunaoathirika ni watanzania.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Sawa. Je, hao CMHC wakoje gharama zao? Na wakipewa Tender, CCCC watalipwa?
Kwanini hakubatilisha Tender na mkopo kutoka China Exim? Kuepusha mashtaka? Aliwasiliana na CCCC?
 
Ninachokiona hapa waliopo nje wanapiga ''jaramba'' na ''mataulo'' na waliopo ndani wako bize kupiga ''tikitaka'' na mataulo !! .......... Sasa kunoga !!!

Wanakwea minazi wakiwa wamevaa misuli bila kufuri!
 
Rushwa ilivyokithiri hujui nani mkweli kibaya zaidi tunaoathirika ni watanzania.

Chama
Gongo la Mboto DSM

Yaani huo ni ushahidi wa wazi kwamba mawaziri wetu (Deputy Ministers inclusive) wanakula rushwa kwenye miradi ya nchi hii. Hii ni aibu kwa serikali kwa kweli.
 
Rushwa ilivyokithiri hujui nani mkweli kibaya zaidi tunaoathirika ni watanzania.

Chama
Gongo la Mboto DSM
Naomba kutofautiana na wewe Mkuu, wana CCM hawaathiriki kwa lolote kwenye hizi Rushwa zilizokithiri maana kwa mwanaCCM ni kwamba hii nchi uchumi unapaa na ilani ya CCM inatimizwa vyema kabisa, na kwenye ule uchaguzi wetu wa ndani hii inaitwa takrima.

Acha unafki hiki ni kipindi ambacho either uko na sisi au uko na wao, huwezi kuishabikia CCM halafu ukadai eti kuna kitu kinakukera, huu ni wakati kwa Mzalendo wa kweli kuchaguwa upande wa kusimamia, usidhani inachezwa sindimba hapa, we mean Business.
 
Sawa. Je, hao CMHC wakoje gharama zao? Na wakipewa Tender, CCCC watalipwa?
Kwanini hakubatilisha Tender na mkopo kutoka China Exim? Kuepusha mashtaka? Aliwasiliana na CCCC?
Mkuu Kobelo, kwenye mikataba kuna mikataba inaitwa void na voidable, mkataba ukishakuwa void unaitwa "void ab initio" wakimaanisha hakuna mkataba hivyo kila mtu inakula kwake!.

Tatizo hapa ni hawa CCCC walikujaje mpaka kupata hiyo MOU?. Ikumbukwe MOU sio contract!.
 

Haya ni mawasiliano ya kawaida lakini inashangaza yanapopigwa muhuri wa 'SECRET'. Hii inaonyesha walikuwa na nia ya kuficha njama zao. Hii ni sawa na fisi kula utumbo wake!
 
Nimeufuatilia huu uzi kwa makini sana. Nimebaki na mihasira na kujiuliza hivi ni kwanini AK47 haziuzwi sokoni Kariakoo kama nyanya?
 
Kwa hiyo Nundu naye ni BANGUSILO tu.
Ingawa sikubaliani na uongozi wa kwenye vyombo vya habari kama alivyofanya jana lakini sasa nimeanaza kumuelewa alikuwa anatuma ujumbe gani.
 
still wonder how can this sht happen after all the 'history' we have on ufisadi bado magamba still add more salt in the wounds. pengine wengine wameshaona mwisho wa magamba hivyo wameamua kuongeza kasi ya kula?! pengine it is about time jeshi lichukue nchi, hatuna mda wa kudili na wevi kwene jumba la sanaa(bungeni) badala ya kuwapeleka wanapostahili (segerea + mahakamani). hii nchi inatia hasira sana.
 
Nashangaa iweje leo Athumani na Omar wanalumbana hadharani....anyway, hii nchi viongozi wamejisahau sana. JK na serikali yake wameshamzidi Mkapa kwa kupiga maana karibu kila sehemu nchi imefilisika.
 
HUjaeleweka mkuu

Unasafishaje mtu kwa barua moja

hivi huwa mnasoma na kuelewa maandishi? umeelezwa wazi hapo juu,kuwa ni mpaka upakuwe barua zote ndipo utaelewa ukweli husika,wewe huja pakuwa tayari umesha anza toa maoni yako


jana niliandika hapa kuwa

TANGU LINI MIRADI YA SERIKALI IKAFANYWA BILA TENDWA KUTANGAZWA?

kamati na menejimenti ya bandari wana lao
 
Jamaa hawana huruma hata kwa watoto wao wenyewe! Sijui wanajiona wao ndo watawala wa mwisho wa Tanzania?

Mwana miaka 45 unaijua? Mie ujanja wangu wote sijaifikisha. Mtu anaweza kuzaliwa leo, akaenda shule, chuo, akawa rais na kuwa rais mstaafu ndani ya miaka 45!

Voyager imekuwa launched 1977 kufikia 2011, takriban miaka 34 (miaka kumi na moja kabla ya kufikisha miaka 45) ilikuwa inatoka nje ya solar system.

Hivi miaka 45 tunaielewa? Tangu uhuru wetu ndiyo kwanza tumefikisha miaka 50. Miaka 45 ni awamu za Nyerere, Mwinyi na Mkapa tunataka kusaini mkataba wa miaka 45 kweli? Si tunarudi kwenye ukoloni tena tu hapa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…